Thursday, October 9, 2014

CHEKA NASI

..BUBU MMOJA ALIULIZWA JINA LAKE. AKAJIBU KWA ISHARA: AKASHIKA KOO NA MBOO. MKALIMANI AKASEMA "HUYU ANAITWA KO MBO". AKAULIZWA UNAKAA WAPI. BUBU AKAVUA NGUO NA KUONYESHA MKUNDU WAKE  MKALIMANI AKASEMA "HUYU ANAKAA HUKO KUNDUCHI". AKAULIZWA KWENU WANAONGEA LUGHA GANI.  BUBU AKASHIKA KISU NA AKAMSHIKA DADA MMOJA SEHEMU ZA SIRI,  DADA AKAWA MKALI NA KUTAKA KUPIGANA NA BUBU. MKALIMANI AKASEMA "HAPANA DADA HUYU ANA MAANA HUKO KWAO WANAONGEA KISU KUMA". CHEZEA BUBU WEWE!!

#######################

Mzee mmoja aliongozana na binti yake kwenda kwa mwanaume aliyempa mimba huku akitweta kwa hasira. Walipofika ilikua hivi: Mzee, wewe ndiye ulimpa mimba bint yangu?
KIJANA: Mzee ni kweli mimi nimempa mimba binti yako, ila akizaa dume nitakupa daladala kumi, sheli 3 na milioni 50 za mtaji. Akizaa jike, nitakupa supermarket 3, mashamba 6 na milioni 40.
BINTI AKADAKIA: Je mimba ikitoka?
MZEE: Nyamaza mshenz ww, si atakupa nyingine... N hatareee aisee.

Wednesday, October 8, 2014

SIMBA YAENDA KAMBI S.AFRICA KWAAJILI YA MAANDALIZI YA MECHI DHIDI YA YANGA

Kikosi cha Wekundu wa Msimbazi
kimebadili muelekeo na sasa
kinatarajia kuondoka nchini leo,
Jumatano kuelekea Afrika Kusini kwa
ajili ya kuweka kambi kujiandaa na
mechi ya mzunguko wa kwanza dhidi
ya watani wao jadi, Yanga
utakaochezwa Oktoba 18, mwaka huu
kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es
Salaam.
Awali NIPASHE ilifahamishwa kwamba
Simba ingekwea pipa kuelekea
Muscat, Oman kwa ajili ya kambi
hiyo, lakini ghafla ikabadili muelekeo
huo.
Kikao cha Wajumbe wa Kamati ya
Mashindano kilichokutana juzi jioni
ndicho kilichofikia maamuzi hayo
baada ya kuwa na mapendekezo
mawili ya kuipeleka timu Oman au
Afrika Kusini kujifua.
Akizungumza na gazeti hili jana,
kiongozi mmoja wa klabu hiyo yenye
makao makuu mtaa wa Msimbazi,
Kariakoo jijini, alisema kuwa timu
hiyo itaweka kambi ya siku 10 katika
jiji la Johanesburg.
Taarifa kutoka ndani ya klabu hiyo
zinaeleza kuwa awamu ya kwanza ya
wachezaji wataondoka jijini leo jioni
na kundi la pili ambalo litakuwa na
wachezaji walioko katika kikosi cha
timu ya Taifa (Taifa Stars) kitaondoka
Jumapili usiku.
Taarifa zaidi zinaeleza kwamba
huenda timu hiyo ikiwa Afrika Kusini
itacheza mechi moja ya kirafiki ya
kimataifa na klabu mojawapo
inayoshiriki Ligi Kuu ya nchi hiyo na
taratibu za kupata mchezo huo
zimeshaanza.
"Timu itaondoka kesho (leo) jioni na
itarejea siku moja kabla ya mechi,"
alisema kiongozi huyo.
Alisema kuwa wanaamini kambi hiyo
itasaidia kuimarisha kikosi chao na
sare walizopata hazijawakatisha
tamaa.
Simba ina pointi tatu baada ya kupata
sare tatu mfululizo katika mechi zake
zilizotangulia dhidi ya Coastal Union
ya Tanga, Polisi Morogoro na Stand
United kutoka mkoani Shinyanga.
Yanga yenyewe itashuka dimbani
ikiwa na kumbukumbu ya ushindi wa
mabao 2-1 walioupata dhidi ya JKT
Ruvu ya Pwani na Prisons, lakini
wakiwa na doa la kichapo cha 2-0
kutoka kwa Mtibwa Sugar ya
Manungu, mkoani Morogoro katika
mechi ya ufunguzi wa ligi hiyo.
Awali mechi hiyo ya watani wa jadi
ilipangwa kufanyika Oktoba 12 lakini
ikasogezwa mbele na Shirikisho la
Soka Tanzania (TFF) ili kupisha
maandalizi ya timu ya Taifa (Taifa
Stars) kuikabili Benin katika mchezo
wa kirafiki wa kimataifa.

MAANDALIZI YA KUKABIDHI KATIKA MPYA KWA KIKWETE YAKAMILIKA

Wakati Maandalizi ya kuwakabidhi
Rais Jakaya Kikwete na Rais wa
Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein
Katiba inayopendekezwa, leo mjini
Dodoma, vyama vinavyounda Umoja
wa Katiba ya Wananchi (Ukawa),
vimesema havitashiriki tukio hilo kwa
madai kuwa maoni ya wananchi
yamechakachuliwa.
Vyama hivyo ni Chadema, CUF na
NCCR-Mageuzi.Katibu Mkuu wa
Chadema, Dk. Willibrod Slaa
(pichani), alisema wao hawatashiriki
kwa madai ya kwamba mawazo ya
wananchi yaliyokuwamo kwenye
Rasimu ya Katiba iliyowasilishwa na
iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya
Katiba, yalichakachuliwa.
“Sisi Chadema hatutashiriki kwa
sababu mawazo ya wananchi
yamechakachuliwa. Makundi
mbalimbali kama vile ya wakulima,
wafugaji yamekuwa yakichukuliwa
kwa makundi na kuambiwa
wakubaliane na katiba
iliyopendekezwa. Wananchi hao
hawana uelewa wa kutosha, hivyo
wanaamini kiongozi wao
anachokisema hata kama ni uongo.
Tunafanya usanii, sisi Chadema
hatuko tayari kushiriki usanii huo.”
Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James
Mbatia, alisema hawezi kusema
chochote kuhusu makabidhiano hayo,
kwa kuwa hawajapewa mwaliko
wowote.
Kwa mujibu wa Mbatia, ofisi yake
ingepewa mwaliko wa kuhudhuria
tukio hilo, angeweza kujua kitu gani
kilichomo kwenye barua na hivyo
kuweza kusema chochote kuhusu
tukio hilo linalotarajia kufanyika leo
katika Uwanja wa Jamhuri, mjini
Dodoma.
“Hatujaalikwa. Mimi kama mwenyekiti
wa chama, ningepata mwaliko,
ningeona maudhui na kujua la
kusema. Sasa nitawezaje kusema,
ikiwa hatujaalikwa na maudhui
siyajui?” Alihoji Mbatia.
Hata hivyo, alisema, wao hawawezi
kujihusisha kwenye tukio ambalo
halina maridhiano kwa madai ya
kwamba, dola inaendeshwa kwa
maridhiano huku akionyesha
kusikitishwa na hatua iliyofikiwa na
BMK ya kuwatukana viongozi wa dini
wakati zoezi la mwisho la kuipigia
kura katiba hiyo iliyopendekezwa na
bunge hilo wiki iliyopita.
“Nchi bado haijakaa vizuri, nami
siwezi kushiriki kupokea katiba
inayounganisha nchi ya namna hiyo.
Hivyo namshauri Rais, leo
azungumze namna ya kuliunganisha
taifa.”
Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa CUF,
Joran Bashange, alisema, wao
walishakataa baada ya kuona
mchakato wa upatikanaji wa katiba
mpya ulikuwa unaenda kinyume na
matakwa ya wananchi.
“Wamepanga utaratibu wao, sisi
tutakubalianaje? Sisi tulikataa kwa
sababu tuliona mchakato ulikuwa
unaenda kinyume cha matakwa ya
wananchi. Hivyo hatuwezi kwenda
kubariki uharamia.”
Naye mjumbe wa iliyokuwa Tume ya
Mabadiliko ya Katiba (TMK), Prof.
Mwesiga Baregu, alishauri tukio la
kukabidhi katiba inayopendekezwa,
lifanyike kimya kimya.
“Ninasikia kuwa kuna maandalizi ya
sherehe za kukabidhi Katiba hiyo
yanayoambatana na nyimbo mpya
zilizoandaliwa kwa ajili ya kuimbwa
kwenye tukio...mimi nashauri
makabidhiano yafanyike kimya
kimya,” alisema Prof. Baregu na
kuongeza:
“Ninashauri hivyo kwa sababu kwa
sasa inaonekana kwamba hatua ya
kupitisha katiba hiyo imekuwa kama
ni ushindi kwa wale walioipitisha na
kumbe sivyo.”
“Watanzania wanataka Katiba
inayowaunganisha na siyo
inayowatengenisha, hivyo kuruhusu
sherehe kwenye makabidhiano hayo
ni kuendeleza msuguano miongoni
mwa makundi yanayopingana kuhusu
katiba hiyo," alisema.
Prof. Baregu alisema kuwa cha msingi
ambacho kilikuwa kinatakiwa ni
maridhiano ili kupata kile wananchi
wanakihitaji, hivyo kushangilia ama
kusherehekea bila kuwa na
maridhiano ni kuongeza mpasuko
kwenye jamii.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk.
Rehema Nchimbi, alisema hadi jana
mchana, tayari mazingira ya uwanja
wa Jamhuri yalikuwa tayari
yameshaandaliwa.
Hata hivyo alipoombwa kutaja majina
ya viongozi wakuu waliothibitisha
kuhudhuria sherehe hizo, Dk. Nchimbi
alisema orodha ipo kwa Katibu wa
BMK kwani wao ndiyo wanaoratibu
shughuli hiyo.
Kwa mujibu wa tarifa za awali
zilizopatikana kutoka kwa ofisa
mmoja wa serikali, sherehe hizo
zinatarajiwa kuhuduriwa na wageni
takribani 3,000.
Kamanda wa Polisi mkoani hapa,
David Misime, alisema
wamejiimarisha kiulinzi na kwamba
kutakuwa na doria katika maeneo
mbalimbali yakiwamo ya mjini.
“Tunafuatilia taarifa mbalimbali kwa
ajili ya kuimarisha usalama, vijana wa
kufanya doria kwa miguu, farasi,
pikipiki na magari wapo muda wote
kuanzia sasa,” alisema Kamishna
Misime.

Saturday, October 4, 2014

AUTHOR SOPHIE KINSELA: 10 tips of being a best-selling author

Here are Kinsella's top 10 tips for
being a bestselling author.
1. Always carry a notebook
Carry a notebook everywhere and
write down everything that springs to
mind, even if it doesn't seem relevant
at the time. You can do a lot with a
passing thought or a little bit of
overheard dialogue.
Get into the habit of looking at life
like a writer and writing it all down.
Don't worry about what "it" is going
to be yet, just write it down as a
habit. Because then, when you do
have your big idea and want to write
a book, you'll already be used to that
process and have material to work
with.
2. Think "what if" and read
Start to see the world in a "what if"
way and keep your possibilities for a
story. Teach yourself to take a tiny
little nugget of substance and
extrapolate and tease it out into
something else, have fun with it and
see the potential.
It can seem tiny and insignificant but
if you can sense the grain of a story
there and keep your mind open to
those possibilities, you will
constantly come up with new ideas.
Reading is vital if you want to be a
writer, it's essential. I've been a
bookworm ever since I was a child, I
was the type who would read a cereal
packet over and over rather than
make conversation at breakfast!
3. Write the book that you want to
read.
People often think that they should
write to please someone else,
whether it is to please the audience,
or critics, or a readership. My instinct
has always said that you can't
second guess anybody else.
'What you have to do is find your
story and find your voice,' says
Sophie Kinsella
What you can do, is think if you were
a reader, what would you want to
read? One way to visualise that is to
go into a shop and imagine the book
that would make you want to grab it
off the shelf.
The chances are that if you would
grab it off the shelf and be excited to
read it. then other people would too.
So always start with yourself, write
something that will please you.
4. Don't talk about what you're
writing
I am very secretive when I'm writing a
new book. I think that writers are very
fragile, they're like butterflies or
perhaps moths; they can be easily
crumpled. If you're very sensitive,
which I am, it only takes a raised
eyebrow or a chance remark about an
idea for you to lose confidence in it.
I think it's much better to let these
things gestate in private, that way
you can be free to try stuff out
without any fear of being judged or
worrying whether it might not work.
The minute you put it out there and
ask for opinions from other people, it
will just get in the way of your
creativity.
The only person I let read my work
when I'm writing is my husband and
we've had this arrangement long
enough that he knows what not to
say! I think a work in progress is a
very precious and nebulous thing and
it can be easily destroyed so protect
it!
5. Forget about genre to find your
voice
I think that one of the hardest things
as a writer is to find your voice. See
what you enjoy writing, because let's
face it, you're going to be spending a
long time in this zone, it had better
be something you enjoy and
something which you can do.
Don't be afraid of a few false starts. I
once tried to write a thriller and I
remember my agent saying that the
plot was ok but that all the characters
were far too nice. I'd written about all
these nice middle class people
walking around killing each other!
Don't sit there thinking what genre
should I write in, perhaps you'll
invent a whole new one! Instead,
start off by thinking I'm going to write
a story and wait for other people to
put it in a genre. What you have to do
is find your story and find your voice.
6. Just get to the end
It's the hardest thing and it's the
most important thing because so
many of us have ideas for books. The
first stage is actually write it instead
of just talking about it, and the next
stage is to keep going until you get
to the end.
Everybody, no matter who they are
gets to the middle of a book and
thinks crikey, I've had enough of this.
You get bored with your story and
your characters, you hate them all,
you can't think why you started this
wretched story in the first place.
The truth is, every book is hard to
write, everybody reaches a wall,
whether it is a plot hole or a scene
that you can't get past. So you've
just got to get to the end. Even if it's
not the greatest draft, if it needs
rewriting fine, at least you have a
book to rewrite.
7. Walk and drink cocktails!
Everybody gets stuck. I find cocktails
very helpful! And that's the truth, if I
get stuck, I'll go out with my
husband and we'll order cocktails
and talk while we drink them. By the
end of the evening, we've always
ironed out the knot.
I find it loosens you up and also it
turns it into a fun project, there's
nothing worse than sitting grimly
staring at a screen, you must get out.
The other thing to do is go for a
walk, walking seems to free up the
cogs of the brain like nothing else.
You can sit at your desk for two
hours, feeling wretched because you
can't find the solution, then you give
up and go for a walk and it comes to
you straight away.
8. Plan your books
For me, the planning stage is vital
and it takes months, if not years.
When I'm writing a book, I do it in my
office, but when I'm planning a book I
like going and sitting in coffee shops.
I like the buzz and I like being
surrounded by people, but remaining
anonymous.
I write my plot points on file cards
and Blu Tac them to the wall. Then I
stand back and look at the terrain of
the story and decide whether I like it
and if not I can just move them
around. I find that very satisfying -
it's a bit like doing a crossword
puzzle!
The truth is you can plan and plan
but during the story, something will
change, that's just the way it is. But I
find starting off with structure and a
beginning, a middle and an end is
vital.
9. Get a great agent and consider a
pseudonym
I think I've written 20 books in total
now and I've always had the same
agent. Having an agent, for me is the
best thing I've ever done, because
she's guided me, she's been a friend,
she's dealt with all the business side
of what I do and I wouldn't have
known where to start without her.
There are lots of advantages to
having a pseudonym. It gives you a
bit of privacy so you can have an
official name and a home name. And I
don't think there are many careers
where you can just completely
reinvent yourself every so often - it's
wonderful.
10. Write the next you
Everyone has got a story to tell and
everyone can learn and improve their
writing. There are some elements of
writing which can definitely be
taught, a sort of craft and you should
always try to learn and improve. I am
still learning with every book.
I don't see why anybody shouldn't
write a book. There is nobody who is
not interesting in this world, so why
shouldn't they tell their story?
You write what you write. You can't
decide to write a certain book, I
believe your writing finds you. So
don't go thinking, I'm going to write
the next Da Vinci Code or the next
Stephen King. Write the next you.
You are going to be the next big
thing!

RAIS MWANZILISHI WA HAITI (JEAN-CLAUDE

Duvalier was just 19 when in 1971 he
inherited the title of "president-for-
life" from his father, the notorious
Francois "Papa Doc" Duvalier.
He was accused of corruption, human
rights abuses and repression in his
rule, which ended in a 1986 uprising.
After years of exile in France, he
returned to Haiti in 2011.
His death was announced by Haiti's
health minister, and the ex-leader's
attorney Reynold Georges confirmed
he died at home on Saturday.
Lavish wedding
At the time of his swearing in, Jean-
Claude Duvalier was the youngest
president in the world.
Initially it seemed that there could be
a significant move away from his
father's harsh regime, underpinned as
it was by Haiti's notorious secret
police, the Tontons Macoutes, says
BBC world affairs correspondent Mike
Wooldridge.
For some time, Jean-Claude Duvalier
was the youngest president in the
world
He moved closer to the Americans,
from whom his father had been
estranged. US businesses moved in
and he allowed limited press freedom.
But Jean-Claude Duvalier lived
lavishly. His state-sponsored
wedding reportedly cost $5m in 1980,
while most of the people in his
ravaged nation endured the worst
poverty in the Western hemisphere.
Repression continued, too, and amid
massive unrest in 1986 he fled to
France.
Human rights groups say thousands
of political prisoners were tortured or
killed under his rule, and he was
accused of massive corruption.
He described his return to Haiti - a
year after it was devastated by a
major earthquake, as a gesture of
solidarity to the nation.
His unexpected return to Haiti saw
him arrested and charged, but the
case against him stalled
But he was arrested and charged, and
although released he finally appeared
in court in February 2013, where in an
emotionally-charged hearing in front
of some of his alleged victims, he
denied responsibility for abuses
carried out during his time as
president.
Judges ruled he could face crimes
against humanity charges, but the
case had stalled some time before he
died.
Jean-Claude 'Baby Doc' Duvalier
Jean-Claude Duvalier, pictured here
in 1980, ruled Haiti with an iron fist
for 15 years
Took over presidency aged just 19
when his father, Haiti's
authoritarian leader Francois "Papa
Doc" Duvalier, died in 1971
Called himself "president-for-life"
and ruled with an iron fist, aided
by a brutal private militia known
as the Tontons Macoutes
Accused of corruption and human
rights abuses that prompted more
than 100,000 Haitians to flee the
country during his presidency
Ruled for 15 years before outbreak
of popular protests led him to flee
to France in 1986
Asked Haitian people for
forgiveness for "errors" made
during his rule in a 2007 radio
interview
Returned to Haiti in 2011 as it was
supposed to hold run-off elections
to choose successor to outgoing
President Rene Preval

PHIL AAHIDI MABADILIKO YA SIMBA

Simba itakayoingia Uwanja wa Taifa
kucheza mechi yake ya tatu ya ligi
kuu ya Bara dhidi ya Stend United leo
baada ya sare mbili mfululizo itakuwa
kama mpya, kocha Patrick Phiri
amesema.
Akizungumza na gazeti hili jana, Phiri
alisema katika mchezo wa leo
atafanya mabadiliko kwenye kikosi
chake ili kuweka uwiano kati ya ulinzi
na mashambulizi kwenye kikosi.
Phiri alisema "Tumechoshwa na
matokeo ya sare" na kwamba
amefanya marekebisho kwenye kikosi.
"Kama utakuwepo uwanjani utaona.
Lengo ni kuiimarisha timu ili kuleta
ushindi."
Kocha huyo Mzambia alisema ushindi
kwenye mchezo wa leo utawarudisha
wachezaji wake 'kwenye njia' baada
ya sare za nyumbani za 2-2 dhidi ya
Coastal Union na 1-1 dhidi ya Polisi
Morogoro.
"Baada ya mchezo dhidi ya Stand
United tutakutana na wapinzani wetu
(Yanga)... nimewaambia wachezaji
tunahitaji ushindi kabla hatujakutana
nao."
Simba ambayo inapewa nafasi kubwa
ya kufanya vizuri msimu baada ya
kumridisha Phiri aliyeipa ubingwa bila
kupoteza mechi mwaka 2010, ipo
pointi nne nyuma ya timu mbili
viongozi mabingwa watetezi Azam na
Mtibwa Sugar.
Aidha, aliwataka mashabiki wa timu
hiyo kutokata tamaa na timu yao
kwani Simba ni timu nzuri na makosa
ya yanayoonekana yanarekebishika na
kuomba kupewa muda kwa wachezaji
wake.

KLA

Klabu za ligi kuu ya Bara zinakusudia
kupeleka katika mkutano mkuu wa
shirikisho la soka (TFF), hoja ya
kutokuwa na imani na rais Jamal
Malinzi.
Klabu hizo, kupitia kwa wakili Dk.
Damas Ndumbaro, zilisema jijini jana
kwamba zitakusanya theluthi mbili ya
kura za wanachama wa TFF ili
kuitisha mkutano mkuu na kupeleka
hoja mbili, ikiwemo hiyo ya
pendekezo la kumng'oa rais
madarakani.
Mkutano mkuu wa TFF una madaraka
ya kumuondoa rais madarakani
kikatiba.
Mbali na hoja ya kutokuwa na imani
na Malinzi, pia klabu zitawasilisha
hoja ya kutaka kufanyike ukaguzi wa
hesabu za fedha za TFF zinazotolewa
na wadhamini wa ligi kuu tangu
kuingia madarakani kwa Malinzi,
Ndumbaro alisema.
Hatua hizo zinafuata baada ya klabu
hizo kuiagiza Bodi ya Ligi Kuu (TPLB)
kutokubali makato ya ziada ya
asilimia tano ya fedha za wadhamini.
TFF imedai inataka kupeleka fedha
hizo kwenye mfuko wa TFF wa
maendeleo ya soka ya vijana.
Akizungumza na waandishi wa habari
jijini jana, Ndumbaro alisema klabu
hazikubali makato ambayo TFF
imeagiza.
"TFF inapata fedha nyingi zaidi ya
vilabu kwa mwaka," alisema
Ndumbaro. "Kwa mfano katika
udhamini wa Azam TFF peke yake
inaingiza zaidi ya milioni 400 huku
vilabu vikiingiza milioni 331.
"Lakini bado katika fedha hizo ndogo
wanazopata vilabu TFF wanataka
kuzikata... kimsingi wateja wangu
(klabu) hawakubali na wanalipinga
suala hili."
Aidha, Ndumbaro alisema kukatwa
Sh. 1000 kabla ya kodi katika mapato
ya kila tiketi iliyotumika kuingia
uwanjani ni hujuma inayofanywa na
TFF kwa serikali, klabu na chama cha
mapinduzi kinachomiliki viwanja vingi
vya soka nchini.
Alisema serikali inadhulumiwa kwa
kodi kutolipwa kwa Mamlaka ya
Mapato (TRA) na hivyo kurudisha
nyuma maendeleo ya nchi na ya klabu
za ligi kuu.
Ndumbaro alisema kugomea kucheza
ligi kuu ni moja ya njia ambazo klabu
zimepanga endapo muafaka
hautapatikana.
Ndumbaro alisema klabu zipo tayari
kukutana na TFF kwa muzungumzo.

BUNGE LA KATIBA MSHTUKO

Uamuzi wa baadhi ya wajumbe wa
Bunge Maalum la Katiba kupiga kura
ya hapana kwa ibara zote za rasimu
mpya ya katiba inayopendekezwa
imeibua mkanganyiko na sasa Kamati
ya Mashauriano imeundwa kukutana
na waliopiga kura hizo.
Juzi wajumbe walianza kupiga kura
kupitisha sura na ibara moja baada ya
nyingine, kwa wazi au siri, huku
wengi wakisema kuwa wanaunga
mkono, lakini pia wakiwamo
wachache waliosema hapana kwa
sura zote 10 na ibara zote kuanzia ya
kwanza hadi ya 157.
Jana Mwenyekiti wa Bunge hilo,
alitaja kamati hiyo kuwa inaundwa na
Makamu Mwenyekiti wa BMK, Samiah
Hassan Suluhu, Rashid Mtuta, Shamsi
Vuai Nahodha, Omari Yusuph Mzee,
Andrew Chenge, Asha-Rose Migiro,
Dk. Francis Michael, Brigedia Jenerali
Mstaafu Hassan Ngwilizi na
Mohammed Aboud.
Bunge hilo limefikia hatua ya kupiga
kura ambayo ni nyeti zaidi kwani
zitahitajika theluthi mbili kutoka kila
upande wa Jamhuri wa Muungano wa
Tanzania ili kufanikisha upitishwaji
wa rasimu hiyo.
Kulingana na mahudhurio
yaliyokuwako juzi kabla ya kuanza
kwa kazi ya upigaji kura, wajumbe
kutoka Tanzania Bara walikuwa 295,
huku kutoka Zanzibar wakiwa ni 142.
Kulingana na hesabu hizo, zitahitajika
kura 140 kutoka Zanzibar na kura 280
kutoka Tanzania Bara ili kupitisha
ibara hizo.
Kwa mahudhurio ya juzi, Zanzibar
ilikuwa na wajumbe wawili zaidi ya
idadi ya theluthi mbili inayohitajika
huku bara kukiwa na wajumbe 15
zaidi ya theluthi mbili ya kura
zinazohitajika.
Hata hivyo, siyo wajumbe wote
walipiga kura za ndiyo na hata
waliopiga za ndiyo wapo waliokataa
baadhi ya ibara. Walikuwapo
waliokataa huku wengine wakipiga
kura za siri, ambazo haijulikani
waliamua nini.
Hali hii inatafsiriwa kama juhudi za
kusaka theluthi mbili ya kura za
wajumbe kutoka Zanzibar, kwa ajili
yakupitisha Rasimu hiyo.
Mwenyekiti wa Bunge hilo juzi
alisema kwa kuzingatia idadi ya
wabunge waliokuwamo bungeni kwa
wakati huo, upande wa Zanzibar
ulikuwa na wajumbe wawili tu
wanaozidi idadi ya inayotakiwa
kupata theluthi mbili, hivyo
akawaomba wote wapige kura ya
ndiyo ili kutimiza matakwa ya
kisheria.
Hata hivyo, zoezi la kupiga kura
lilipoanza, wabunge saba kutoka
Zanzibar walipiga kura ya wazi ya
hapana, huku wengine zaidi ya 20
wakipiga kura ya siri.
Hali hiyo imelifanya BMK kushtuka
kutokana na kuwapo kwa dalili ya
kukosekana kwa theluthi mbili ya kura
za ndiyo kutoka Zanzibar, hivyo
kuufanya uongozi wa Bunge hilo
kuanza kuhangaika kuweka ‘mambo
sawa’.
Kamati ya mashauriano iliundwa kwa
ajili ya kuwasikiliza wajumbe
waliopiga kura ya hapana dhidi ya
rasimu nzima.
Akizungumza saa 5:50 wakati wa
kipindi cha Matangazo jana,
Mwenyekiti wa BMK, alisema kuwa
uongozi umeshtushwa na uamuzi wa
wajumbe hao kupiga kura ya hapana
kwa rasimu nzima huku wakiwa
wametumia muda mwingi kuijadili
jambo ambalo siyo la kawaida.
Alisema kuwa kutokana na hali hiyo,
ameamua kuunda Kamati ya
Mashauriano kwa ajili ya kuwasikiliza,
huku akidai kuwa wajumbe wawili
kati ya waliopiga kura ya kuipinga
rasimu hiyo waliomba kusikilizwa.
Alisema kuwa kanuni ya 54, kanuni
ndogo ya nne inasema kwamba
‘Mwenyekiti baada ya kushauriana na
Kamati ya Uongozi anaweza kuunda
kamati ya mashauriano pale anapoona
linajitokeza suala linalohitaji
mashauriano’.
“Nina suala mbele yangu linalohitaji
mashauriano kutokana na baadhi ya
wabunge wenzetu ambao jana (juzi)
walipiga kura ya hapana kwa ibara
zote kitu ambacho si cha kawaida
kwa sababu haiwezekani kuwa hivyo,”
alisema Mwenyekiti huyo.
“Tunaomba Kamati hii ifanye kazi leo
(jana) na sisi tutapokea matokeo
baadaye na kuyaleta ndani ya Bunge
hili kwa wakati unaofaa,” alieleza
Mwenyekiti huyo.
Alisema kuwa ingawa wajumbe wawili
kati ya waliokataa Rasimu hiyo juzi
walimuomba kusikilizwa pia milango
ya kamati hiyo itakuwa wazi hata kwa
wajumbe wengine ambao hawajaomba
ili ieleweke kwanini wakae wakati
walikaa kipindi chote bungeni kisha
waikatae rasimu yote.
Baadhi ya wajumbe wa BMK
waliozungumza na NIPASHE jana
mjini Dodoma walielezea
kutoridhishwa na hatua hiyo,
wakiamini kanuni ililenga kuundwa
kwa kamati wakati wa vipindi vingine
vya uhai wa BMK, lakini siyo katika
kipindi hiki cha upigaji kura.
Walisema kuwa kitendo cha kuundwa
kamati hiyo katika kipindi cha kupiga
kura, wanakitafsiri kuwa ni kuingilia
uhuru wao wa kufanya maamuzi.
Dk. Alley Nassoro, alisema yeye siyo
miongoni mwa walioelezwa na
Mwenyekiti wa BMK, kuwa wameomba
kusikilizwa na kwamba hajutii kupiga
kura ya hapana kwa rasimu yote kwa
sababu ana amini ndiyo msimamo
halisi alionao juu ya kazi yote
aliyofanya tangu BMK lilipoanza.
“Sababu zangu kuu ni mbili tu
ambazo zimesababisha nipige kura ya
hapana, ya kwanza ni imani na uzawa
wangu; nikimaanisha dini ya kiislamu
kunyimwa haki ya Mahakama ya Kadhi
kutambuliwa na kuheshimiwa kikatiba
lakini ya pili ni maslahi ya nchi yangu
Zanzibar, kutozingatiwa na Katiba hii
kwa kiwango cha kukidhi matarajio
yangu,” alisema Dk. Alley.
Alisema hata ahadi iliyotolewa
bungeni na Waziri Mkuu, Mizengo
Pinda, wakati wa mijadala ya
kuboresha Rasimu hiyo ya Katiba
inayopendekezwa, kwamba Mahakama
ya Kadhi itatungiwa sheria haafikiani
nayo kwa sababu siyo mara ya
kwanza kwa serikali kutoa ahadi juu
ya jambo hilo.
Alisema kwamba hata ikitungwa
sheria ya aina hiyo, utekelezaji wake
unaweza usifanyike kwa sababu
utategemea zaidi uongozi
utakaokuwa madarakani tofauti na
kama haki hiyo ingewekwa kwenye
Katiba ambayo ndiyo sheria mama.
“Hii Katiba inayopendekezwa kwa
jinsi ilivyowekwa ni dhahiri hata
kama ikitungwa sheria ya kuanzisha
Mahakama ya Kadhi, utekelezaji wake
utakuwa mgumu kwa sababu baadhi
ya watu wanachukulia baadhi ya
masharti katika imani yetu kuwa ni
yenye chembe za kibaguzi hususan
katika umiliki wa mali baina ya
mwanamke na mwanaume,” alieleza
Dk. Aley.
Suala la kupata theluthi mbili ya kura
za upande wa Zanzibar linakuwa tete
kutokana na wabunge wa Chama cha
Wananchi, CUF pamoja na wale wa
kundi la 201 ambao waliungana na
kundi la Umoja wa Katiba ya
Wananchi (Ukawa) na kuondoka
bungeni, hali inayosababisha idadi ya
wajumbe waliobaki kupata wakati
mugumu kutimiza matakwa ya
kisheria ya kuhakikisha Rasimu hiyo
inapitishwa na theluthi mbili ya kura
za wajumbe wote kutoka katika kila
nchi washirika.
Imeandaliwa na Emmanuel Lengwa,
Editha Majura, John Ngunge na
Jacqueline Massano, Dodoma.

KESI YA MWANAFUNZI ALIYELAWITIWA YAFUTWA

Kesi ya mwanafunzi wa darasa la tatu
(jina linahifadhiwa) katika Shule ya
Msingi Ukombozi iliyofunguliwa
katika Kituo cha Polisi cha Urafiki,
jijini Dar es Salaam baada ya kudaiwa
kulawitiwa imefutwa.
Kesi hiyo ambayo ilifunguliwa
Septemba 15, mwaka huu kituoni
hapo, ikimkabili mtuhumiwa
aliyetajwa kwa jina moja la Enock,
imefutwa jana na mtu huyo kuachiwa
huru kwa madai kuwa, imekosa
ushahidi.
Mama wa mtoto huyo (jina
linahifadhiwa), aliliambia gazeti hili
kuwa, mpelelezi wa kesi hiyo
aliyemtaja kwa jina moja la Suzana
aliiambia familia hiyo kuwa, baada ya
jalada la kesi kupelekwa kwa
mwanasheria na kulipitia, alikosa
ushahidi wa kulipeleka shauri hilo
mahakamani.
Alisema baada ya kuripoti tukio hilo
kituoni hapo alipewa RB/
Urafiki/7627/2014.
Aidha, mama huyo alisema mjomba
wa mtoto alipofuatilia kesi hiyo jana
kituoni hapo alirudi na majibu kuwa
imefutwa.
Alisema kuwa baada ya kukutana na
mpelelezi wa kesi hiyo, alimweleza
kuwa jalada la kesi limerudi kutoka
kwa mwanasheria na mtuhumiwa
anaachiwa huru kutokana na
kukosekana ushahidi.
Alisema baada ya maelezo ya
mpelelezi, aliomba kuonana na Mkuu
wa Kituo hicho, ambaye naye
alimweleza kuwa, majibu ya daktari
yalionyesha hajalawitiwa.
Pia alisema mkuu huyo wa kituo
alimweleza kuwa alichokieleza mtoto
kuhusu mazingira ya nyumbani kwa
mtuhumiwa yalikutwa tofauti.
Siku ya tukio mtuhumiwa huyo
alikamatwa baada ya mama
kuambatana mtoto wake siku ambayo
kijana huyo alikuwa na miadi ya
kukutana na mwanafunzi huyo.
Kabla ya kukamatwa kwake, kijana
huyo ilidaiwa alishamfanyia vitendo
hivyo mtoto huyo zaidi ya mara moja
na alikuwa akimpa fedha kati ya Sh.
2000 na Sh. 7000 lakini siku ya
kukamatwa alimpa Sh. 200.
Awali, Mwalimu Mkuu wa shule hiyo,
Biamina Swai, aliliambia gazeti hili
kuwa, kwa mwaka huu jumla ya
matukio manne ya watoto kufanyiwa
vitendo hivyo yalitokea lakini hilo
moja ndilo mtuhumiwa wake
alikamatwa baada ya kushirikiana na
mzazi wake.
Alisema matukio mengine baada ya
wazazi kupewa taarifa za ulawiti wa
watoto wao, pindi waendapo mitaani
huvujisha siri na kusababisha
wahusika kukimbia.

WANAUME 400,0

Serikali imesema jumla ya wanaume
400,000 kutoka mikoa minne nchini,
wamefanyiwa tohara katika kampeni
iliyomalizika hivi karibuni.
Katika hotuba ya Waziri wa Afya na
Ustawi wa jamii, Dk, Seif Tashid,
iliyosomwa na Naibu Katibu Mkuu wa
Wizara hiyo, John Michael, wakati wa
ufungaji wa kampeni hiyo jijini Dar es
Salaam jana, alisema mikoa
iliyohusika na kampeni hiyo ni Iringa,
Njombe na Tabora.
Zoezi la kuwafanyia tohara wanaume
lililofahamika kama `tohara ya
kitabibu ya wanaume’ (VMMC)
iliendeshwa kwa ushirikiano kati ya
Serikali ya Tanzania, Marekani na
Shirika la Jhpiego.
Alisema zoezi hilo limesaidia
kupunguza kasi ya maambukizi ya
virusi vinavyosababisha Ukimwi
(VVU) nchini, kitu kinachoonyesha
lengo la kufikia maambukizi ya
asilimia 0.16 hadi mwaka 2018
linaweza kufikiwa.
Baada ya kuonekana kwa mafanikio
hayo, mikoa mingine 12 ambayo
wanaume wake wapo nyuma katika
kufanyiwa tohara imeteuliwa
kuendelea na zoezi hilo.
Kiasi cha Dola za Marekani Milioni 34
zimetengwa kwa ajili ya kuendesha
kampeni hiyo.
Dk. Rashid alisema lengo ni kuwafikia
watu milioni 2.1 walio na umri kati ya
miaka 10 hadi 34 kufikia mwaka 2017.
Awali, Naibu Mkurugenzi wa Shirika
la Misaada la Marekani nchini (USAID)
, Timoth Donny, alisema katika tafiti
mbalimbali zinaonyesha kwamba
wanaume waliofanyiwa tohara
wanaondokana na hatari ya
kuambukizwa VVU kwa silimia 60,
hivyo kuna wajibu wa kuhakikisha
elimu inatolewa sehemu zote nchini.
Alisema nchi yake ipo tayari kusaidia
katika kupambana na hali hiyo katika
nyanja ya kujengea uwezo wa
mafunzo na vitendea kazi kwa watoaji
huduma.
Naibu Rais wa Shirika la Jhpiego,
Alain Damiba, pamoja na kuishukuru
serikali kwa kutoa msaada mkubwa
katika kutekeleza mkakati huo, shirika
lake kwa kushirikiana na washirika
mbalimbali litaendelea kufanya kazi
kwa ajili ya kuboresha afya za
wananchi na kuongeza kasi ya
maendeleo.

Friday, October 3, 2014

WAKAZI JIJINI MBEYA WAHAURIWA KUTUMIA VIZURI FURSA

Mlezi na mshauri wa asasi ndogo
ndogo la kifedha (Vicoba) mkoani
Mbeya, Dk. Stephen Mwakajumilo,
amewataka wananchi wa mkoa huo
kutumia fursa mbalimbali
zinazowazunguka ili kujitegemea
kiuchumi na kuacha kutegemea
wafadhili.
Dk. Mwakajumilo aliyasema hayo
alipokuwa akitoa elimu ya ujasiriamali
kwa waumini wa Kanisa la Kiinjili la
Kilutheri Tanzania (KKKT) katika mtaa
wa Lwambi, Usharika wa Itete
Halmashauri ya Busokelo wilayani
hapa.
Dk. Mwakajumilo ambaye ni pia
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Teofilo
Kisanji (Teku) cha jijini Mbeya,
alisema wilaya hiyo ni miongoni mwa
wilaya zenye utajiri mkubwa ambao
kama wananchi watautumia vizuri,
watakuwa na fursa nzuri ya kusukuma
gurudumu la maendeleo katika
maeneo yao.
“Nimeelezwa kuna vijana kadhaa
ambao wamemaliza vyuo vikuu kwa
taaluma mbalimbali hapa usharikani,
hakikisheni mnawatumia vijana hao
vyema kwa kuwapeni mbinu za
kufanya katika kutumia vizuri
rasilimali zilizopo ndani ya
halmashauri hii kwa manufaa ya jamii
hii na taifa kwa ujumla,” alisema.
Alieleza kuwa huu siyo muda wa
kuendelea kutegemea wafadhili katika
kuchangia shughuli za kimaendeleo,
wakati wananchi hao wana rasilimali
za misitu na ardhi ambayo ina rutuba
ya kutosha kwa kilimo cha mazao na
nyingine nyingi, hivyo kinachohitajika
ni elimu tu na kukubali kujitoa
kutumia fursa hizo.
“Mfano mzuri ni misitu tuliyonao hapa
kwetu tukiamua kwa dhati
kutengeneza mizinga ya nyuki kadhaa
katika usharika huu, nina hakika
tutaondokana kabisa na suala la
harambee za kila mara kuita watu
kutuchangia kwani tutapata fedha
nyingi ndani ya muda mfupi na
kutimiza malengo yetu,” alisema Dk
Mwakajumilo.
Aidha, alitoa mizinga mitatu na fedha
taslim Shilingi milioni moja kwa ajili
ya kuchonga mizinga mingine ili
kuwahamasisha waumini hao kuanza
rasmi shughuli ya ufugaji wa nyuki
huku akiahidi kupeleka mtaalam wa
nyuki kutoa elimu juu ya utunzaji na
uvunaji bora wa asali.

WATANZANIA WANG'ARA KATIKA CHAGUO LA VIONGOZI WACHUMI WA KESHO AFRI

Watanzania watano wamechaguliwa
kuingia katika orodha ya viongozi
wachumi wa kesho 100 akiwemo
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya
Mohammed Enterprises Tanzania
Limited (MetL), Mohammed Dewji.
Dewji ambaye pia ni Mbunge wa
Singida Mjini, alishika nafasi ya pili
kupitia utafiti wa kila mwaka
uliofanywa na Taasisi ya Choiseul ya
Ufaransa inayojishughulisha na
uchambuzi wa masuala ya kisiasa,
kiuchumi na utamaduni kimataifa.
Watanzania waliongia kwenye orodha
hiyo ma kampuni zao katika mabano
ni Genevieve Sangudi (Carley Group),
Elsie Kanza (Mkuu wa World
Economic Forum-Afrika), Patrick
Ngowi (Helvetic Group) na Denis
Dilllip ambaye ni Mwenyekiti wa
Canaco Tanzania.
Viongozi hao wamechaguliwa na
taasisi hiyo kwa kuangalia michango
ambayo wametoa katika mataifa yao
na Bara la Afrika kwa ujumla
yakiwamo kutoa ajira, uwekezaji wa
ndani na nje na uinuaji wa uchumi
kupitia biashara wanazofanya.
Katika orodha hiyo nafasi ya kwanza
imeshikwa na Igho Sanomi (Nigeria),
Mohamed Dewji ya pili, , Hisham El
Khazindar wa Misri (3), Isabel Dos
Santos wa Angola (4), Tidjane Deme
wa Senegal (5), Nomkhita Nqweni wa
Afrika Kusini (6), Mehdi Tazi wa
Morocco (7), Marlon Chigwende wa
Zimbabwe (8) huku nafasi tisa ikienda
kwa Ashish Thakkar wa Uganda
wakati ya kumi imechukuliwa na
Janine Diagouwodie wa (Ivory Coast)

TAMBWE AMTANGAZIA VITA KAVUMBAGU

Mfunguji bora wa Ligi Kuu ya
Vodacom Tanzania Bara (VPL) msimu
uliopita, Amissi Tambwe amesema
ataanza 'kumshika' kinara wa mabao
kwa sasa Didier Kavumbagu kesho
wakati Simba itakapoivaa Stand
United kwenye Uwanja wa Taifa jijini
Dar es Salaam.
Kavumbagu, mshambuliaji wa Azam
FC na timu ya taifa ya Burundi
'Entamba Murugamba', anaongoza
safu ya wafumani nyavu akiwa
amefunga mabao manne katika mechi
mbili za mwanzo ambazo mabingwa
hao watetezi walishinda 3-1 dhidi ya
Polisi Morogoro na 2-0 dhidi ya Ruvu
Shooting.
Hata hivyo, Tambwe katika mahojiano
na chanzo chetu  jijini Dar es Salaam jana
alisema zawadi ya mfungaji bora
itatua tena kwake na ataanza
kufukuzana na Kavumbagu katika
mechi ya kesho.
"Ninaona ametangulia tu, Simba kwa
sasa imeimarika, ninaamini tutaanza
kushinda kwa magoli mengi kuanzia
mechi inayokuja," alisema.
"Kikosi chetu kimeanza vibaya
kutokana na matatizo kidogo ambayo
tuliyazungumza kwenye kikao na
uongozi jana (juzi). Kazi yangu ni
kufunga, nitafunga zaidi yake,"
alisema zaidi Tambwe.
Raia huyo wa Burundi anayesifika kwa
kufumania nyavu, alijiunga na Simba
Agosti mwaka jana akitoka kuipa
ubingwa wa Kombe la Kagame klabu
ya Vital'O ya kwao, Burundi.