Tuesday, September 30, 2014

WAKAZI WA DAR WAPINGA MWEKEZAJI KUZIBA BARABARA

Wakazi wa eneo la Salasala wilayani
Kinondoni, Dar es Salaam wamepinga
uamuzi wa serikali kumpatia kibali
mwekezaji wa kampuni ya Mayfair na
kuziba barabara iliyokuwa ikitumika
kwa miongo miwili.
Mwenyekiti wa Kamati ya usimamizi
wa barabara hiyo, Seleman Magingi,
alisema hatua hiyo ya serikali
itawasababishi usumbufu wakazi
zaidi ya kaya 150 na viwanda.
Alisema mazingira ambayo kibali
hicho kimetolewa, yanaonyesha
viongozi wa Serikali ya Mtaa
kushawishiwa na rushwa.
“Kama mazingira hayo hayakuwa
rafiki mbona wananchi na wenye
viwanda hatukushirikishwa,ndiyo
maana mwekezaji huyo amepata
kiburi,” alisema Magingi.
Mmoja wa wakazi hao,Irene Shayo
alisema viongozi hao wanapaswa
kuangaliwa vizuri kupitia mwekezaji
huyo na kupoteza haki ya wananchi
kwa kununuliwa.
Alisema awali mwekezaji huyo
aliwarubuni kuwa atawaboreshea
miundombinu kama barabara,umeme
na maji wakati huduma hizo
zinapatikana kwa msaada wa viwanda
vilivyopo.
“Kufungwa kwa barabara hiyo
kutasitisha huduma zote za kijamii na
kiuchumi,”alisema.
Afisa Mtendaji wa Mtaa wa
Salasala,Ramadhan Ntai,eneo hilo
limefungwa baada ya mmiliki wa
kiwanja hichi kupata kibali kutoka
Wizara ya Ardhi,Nyumba na Makazi.
Alisema Wizara hiyo ilimtaka
Mwekezaji huyo kufanya marekebisho
ya ujenzi wa kubadilisha matumizi ya
kiwanja hicho ili barabara ipatikane.
Naye, Mmiliki wa Kampuni ya Mayfair
ambaye hakupenda jina lake
liandikwe alisema hayupo tayari
kuzungumza na vyombo vya habari.
“Siwezi kuongea na
waandishi,mtendaji anafahamu kila
kitu mtafuteni yeye,”alisema.
Diwani wa Kata ya Wazo, John Morro,
kupitia barua yake ya Oktoba mwaka
2013 yenye kumbukumbu namba
DSM/KN/2013/22, kwenda kwa
Mkurugenzi wa Ramani wa Wizara ya
Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya
Makazi ikiwataarifu kufufuliwa kwa
barabara hiyo.
Barua hiyo ilikitaka kiwanja namba
10/211 Becon YP 366, 362, 849, 847,
kuacha eneo la barabara kwa ajili ya
jamii.

KURA ZA HAPANA ZAENDELEA KURINDIMA BUNGENI

Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba,
akipiga kura wakati wa zoezi la
kupigia kura Rasimu ya Katiba
inayopendekezwa na bunge hilo mjini
Dodoma jana.Picha/ Khalfan Said.
Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba,
jana walianza kupiga kura kupitisha
Rasimu ya Katiba inayopendekezwa,
huku ikifanyika kampeni kali kusaka
theluthi mbili za wajumbe baada ya
suala la Mahakama ya Kadhi
kushindikana kuingizwa kwenye
rasimu hiyo.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda,
wajumbe watatu wanaowakilisha
madherhebu ya dini na Mwenyekiti wa
Kamati ya Uandishi, Andrew Chenge,
walipewa fursa ya kuzungumza na
kutoa kauli za kuwashawishi wajumbe
wakubali kuipitisha rasimu hiyo huku
suala kubwa likiwa ni Mahakama ya
Kadhi.
KAULI YA PINDA
Kabla ya hatua ya kupiga kura kuanza
jana alasiri, Waziri Mkuu, Mizengo
Pinda, alilazimika kutoa tamko la
serikali kufuatia taarifa kwamba
wajumbe hususan ambao ni waumini
wa dini ya Kiislamu, wamedhamiria
kuipigia kura ya `Hapana' rasimu
hiyo.
Msimamo wa kuipigia kura za
`hapana' rasimu hiyo ulitolewa
mwishoni mwa wiki na baadhi ya
wajumbe kwa nyakati tofauti bungeni
wakati wakihakiki Rasimu ya Tatu
iliyowasilishwa na Mwenyekiti wa
Kamati ya Uandishi, Andrew Chenge,
ambayo haijaingiza suala la
Mahakama ya Kadhi kama ambavyo
walitaka iwe.
Akitoa tamko hilo, Waziri Mkuu Pinda,
alisema linafuatia kikao cha
maridhiano cha pamoja kati yake na
Kamati ya Uongozi wa BMK ambacho
pia kiliwashirikisha pia viongozi wa
dini za Kiislamu na Kikristo.
Alisema suala la Mahakama ya Kadhi
ambalo lilianza tangu mwaka 2005,
lilifikia hatua nzuri kwa waumini wa
dini ya kiislamu kuanzisha mahakama
hizo mikoa yote nchini, mwaka
2011/12.
Hata hivyo, alisema tatizo ambalo
limejitokeza kwa sasa ni utekelezaji
wa maamuzi yanayofikiwa kwenye
mahakama hizo kwa upande wa
serikali.
Alisema: “Taifa hili ukiondoa ubaguzi
serikali na kama nchi tumejitahidi
sana kama serikali, tumejitahidi sana
kama nchi kutenganisha shughuli za
imani za dini na shughuli za serikali.”
Alisema huo ndiyo msingi muhimu
sana kwa sababu serikali haina
dini.“Serikali hii haina dini…nchi hii
haina dini, lakini kwa Mtanzania
mmoja mmoja, lazima tuheshimu sana
yale ambayo yeye anaamini kwa imani
yake,” alisema. Alisema kazi ya
serikali ni kuweka mazingira mazuri
ya kuhakikisha kila mmoja anapata
fursa nzuri ya kuamini imani yake.
Alisema nguzo hii muhimu imesaidia
sana kujenga umoja, amani, utulivu
na mshikamano wa taifa hili kwa
kipindi chote hicho na kwamba ni
matarajio ya Katiba mpya nayo italeta
mshikamano huo kwa miaka mingi
ijayo.
“Nawaombeni sana wote katika jambo
hili tusitetereke, tukatae hisia zozote
ambazo zitatuletea uvunjifu wa
amani,” alisema.Alisema baada ya
kikao chao cha Jumamosi, viongozi
hao wa dini waliitaka serikali kutoa
ahadi ni lini sasa wataboresha sheria
zake ili maamuzi yanayotolewa na
mahakama hizo yasiendelee
kupuuzwa yanapopelekwa serikalini.
Pinda alisema kwa kuzingatia
umuhimu huo, serikali itaziangalia
sheria zake mbili ambazo ni Sheria ya
Mahakama ya Mahakimu, Sura yua 11
na Sheria ya Kiislamu, sura ya 375, na
wataleta muswada bungeni ifikapo
Januari mwakani.
Alisema kabla ya kuwasilisha
muswada huo utawashirikisha wadau
wengi na ukifikishwa bungeni
wataangalia namna gani bora ya
kutekeleza maamuzi yao. Anasema
awali alikuwa mbumbumbu sana
katika eneo hilo, lakini baada ya
mazungumzo hayo ameelewa vizuri.
SHEIKH THABIT JONGO
Akizungumza baadaye Mjumbe wa
BMK, ambaye anatoka kundi la 201
(dini), Sheikh Thabit Jongo, alisema
wajumbe bungeni humo wanashukuru
kwa tamko lililotolewa na serikali
kupitia Waziri Mkuu.
“Wajumbe humu ndani wathamini
kauli ile iliyotolewa na Waziri Mkuu…
kitu nyeti na kinachoweza kuvuruga
amani ni suala la imani ya dini mtu.
Humu ndani suala la Mahakama ya
Kadhi lilitaka kutuvuruga,” alisema.
Alisema wapo Waislamu ambao
walikuwa hawaipendi mahakama hiyo
na wapo Wakristo pia ambao hawataki
mahakama hiyo.Lakini kutokana na
tamko lililotolewa na Waziri Mkuu
jana, anawaomba wale wote
waliokuwa na mipango ya kuipigia
kura ya hapana rasimu hiyo sasa
mipango hiyo waifute.
Sheikh Thabit alisema maadui wa
bunge hilo ni watatu ambao ni
kwanza kundi la Umoja wa Katiba ya
Tanzania (Ukawa) ambao wangependa
bunge hilo livunjike.
Alimtaja adui wa pili kuwa ni
aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya
Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph
Warioba, ambaye mara kwa mara
amesikika akilipinga bunge hilo na
hata kudai kuwa atakwenda mitaani.
Adui wa tatu kwa mujibu wa Sheikh
Thabit, ilikuwa ni suala la Mahakama
ya Kadhi, lakini kutokana na tamko la
serikali jambo hilo litashughulikiwa
ifikapo Januari mwakani kwa maana
ya kurekebisha sheria ili utekelezaji
wa maamuzi ya mahakama hizo
yaweze kushughulikiwa na serikali.
Sheikh Hamid Jongo
Kwa upande wake, Sheikh Hamid
Masoud Jongo, alisema kwa kuwa
tamko hilo limetolewa na ofisi ya
Waziri Mkuu kwa maana ya taasisi
basi utekelezaji wake usiwe na
kigugumizi tena kesho kutwa.
Alisema Waislamu hawana nia haswa
ya kuvuruga mchakato huo, lakini
akataka ahadi iliyotolewa na Waziri
Mkuu iheshimiwe.
ASKOFU MTETEMELA
Naye Askofu Mkuu Mstaafu wa Kanisa
la Anglikana Tanzania, Donald
Mtetemala, alisema suala la
Mahakama ya Kadhi kwa muda mrefu
lilileta wasiwasi kutokana na hofu ya
kusababisha mpasuko kwa jamii ya
Watanzania.
Alisema upo mpasuko wa kisiasa,
lakini mpasuko wa kidini ni mbaya
sana, hivyo ndiyo maana suala hilo
limechukua muda mrefu ili kulipatia
ufumbuzi.
“Nimeona roho ya kuvumiliana,
ukomavu katika tamko la Waziri Mkuu
Pinda. Alisema rasimu hiyo ina suala
la msingi kwamba serikali na nchi hii
kwa ujumla haina dini.Aliwaomba
waumini wa dini ya Kikristo kuelewa
suala hilo kwa mapana yake.
CHENGE
Mapema Mwenyekiti wa Kamati ya
Uandishi, Andrew Chenge,
akiwasilisha marekebisho ya Rasimu
ya Katiba inayopendekezwa alisema
rasimu hiyo imefuta na kuandika upya
Ibara ya 2(2) ambayo sasa itakuwa
ikisomeka kuwa, “Rais wa Jamhuri ya
Muungano atakuwa na mamlaka ya
kuigawa Jamhuri katika mikoa, wilaya
na maeneo mengine:
Alisema: “Isipokuwa kwa upande wa
Tanzania Bara, Rais atashauriana na
Rais wa Zanzibar kabla ya kuigawa
Tanzania Zanzibar katika mikoa,
wilaya au maeneo mengine.”
Kabla ya marekebisho hayo, rasimu
yake aliyoiwasilisha wiki iliyopita,
ilisema kwamba Rais wa Jamhuri
angekuwa na mamlaka ya kuigawa
mikoa, wilaya Tanzania Zanzibar,
lakini bila kushauriana na Rais wa
Zanzibar.
Aidha, alitaja marekebisho mengine
kuwa ni kuongeza Ibara mpya ya 44A
inayozungumzia Haki za wakulima,
wafugaji, wavuvi na wachimbaji
madini.
Pia, alisema rasimu imeongeza Ibara
mpya 48A kuhusu Haki ya afya na
maji safi na salama na Ibara ya 55
imefanyiwa marekebisho na kuweka
haki kwa wazee.Alisema Ibara
nyingine iliyoongezwa ni ya 100A
inayohusu Makamu wa Kwanza wa
Rais kushindwa kumudu majukumu
yake.
Kuhusu idadi ya mawaziri alisema
rasimu imeweka ukomo kwamba sasa
imeweka idadi ya mawaziri na
manaibu wao wasizidi 40.
Alisema rasimu pia imeunda Tume ya
Uratibu na Uhusiano ya Muungano
ambayo itakuwa ikishughulika na
usuluhishi wa migogoro kati ya pande
mbili za Muungano kabla ya kufikisha
migogoro hiyo Mahakama ya Juu.
Ibara nyingine mpya ni 208A ambaye
inazungumzia Tume za Kisekta
ambayo itakuwa na tume mbalimbali
za huduma. Kadhalika, alisema
rasimu imeongeza ibara nyingine
mpya 242 kuhusu Udhibiti wa rushwa.
UPIGAJI WA KURA
Zoezi la upigaji kura lilianza kwa
kusuasua baada ya baadhi ya
wajumbe hasa wa kutokea upande wa
Zanzibar, kuikataa kwa kupiga kura za
wazi.
Hatua ya baadhi ya wajumbe kutoka
Zanzibar kupiga kura ya hapana,
ilitarajiwa kutokana na msimamo wao
wa awali waliouonyesha baada ya
suala la Mahakama ya Kadhi
kutoingizwa kwenye Rasimu hiyo.
Wajumbe hao bila woga walipiga kura
ya wazi na kutamka kuwa hawaungi
mkono ibara zote za Rasimu hiyo.
Hata hivyo, wapo baadhi ya

Saturday, September 27, 2014

HUNA HAJA YA KURUDIA RUDIA WIMBO MPYA WA CHRISS BROWN (NEW FLAMES)..LYRICS ZAKE HIZI HAPA

There can be one only you
And, baby, God can never make two
And I know you came here with your
crew
But I promise you that it feels like it's
just us two, aha.
[Bridge: Chris Brown:]
Oh, I don't know what you had
planned to do tonight
But I just wanna be the one to do
you right, right
And we're standing here looking at
each other, baby, eye to eye
And I'm hoping that you're thinking
about leaving with me tonight
[Hook: Chris Brown:]
Who said you can't find love in the
club?
'Cause I wanna tell them they're
wrong
Come on, just, baby, try a new thing
And let's spark a new flame
You gon' be my baby
Love me, love you crazy
Tell me if you're ready
Baby, come and get it
Try a new thing
And let's spark a new flame
[Verse 2: Usher:]
I can't believe you came here all
alone, baby girl, where's your lover?
Oh, it don't really matter 'cause I got
plans to get to know you better,
yeah.
Baby, baby, baby, baby, let's make
what we got here last forever
Girl, 'cause I don't wanna let you go,
never
[Bridge:]
Oh, I don't know what you had
planned to do tonight
Girl, I just wanna be the one to do
you right, right
And we're standing here looking at
each other, baby, eye to eye
Baby, I hope that you're thinking
about leaving with me tonight
[Hook:]
Who said you can't find love in the
club?
'Cause I wanna tell them they're
wrong
Come on, just, baby, try a new thing
And let's spark a new flame
You gon' be my, baby
Love me, love you crazy
Tell me if you're ready
Baby, come and get it
Try a new thing
And let's spark a new flame
[Verse 3: Rick Ross:]
Home plate, world series, our nigga
sliding in her
Baby, I'm a boss, I'm talking George
Steinbrenner
Panamera, Yogi Berra, my two-seater
Derek Jeter
Got more stripes than all these niggas
Babe Ruth balling in a Beamer
Collar on my Polo, kisses on my
necklace
All my diamonds watching, now my
watches getting jealous
Smoking on a bomb in my autograph
Lebron's
Yeah, she told me I'm the one, that's
when I only hit it once
[Hook: Chris Brown:]
Who said you can't find love in the
club?
'Cause I wanna tell them they're
wrong
Come on, just, baby, try a new thing
And let's spark a new flame
You gon' be my, baby
Love me, love you crazy
Tell me if you're ready
Baby, come and get it

COUNTINHO,JERRY TEGETE KUONGOZA KESHO

Mbrazili Coutinho na Jerry Tegete
watakuwa miongoni mwa wachezaji
wa Yanga watakaoanza pambano la
kesho la ligi kuu ya Bara dhidi ya
Prisons, kwenye Uwanja wa Taifa,
kocha Marcio Maximo amesema.
Akizungumza na Nipashe jana,
Maximo alisema anataraji wachezaji
hao wataleta mabadiliko ya kiuchezaji
Yanga na kupata ushindi baada ya
kuanza kwa kufungwa na Mtibwa
Sugar wiki iliyopita.
"Nimefanyia kazi mapungufu
niliyoyaona (katika mchezo wa
kwanza) lakini furaha yangu ni
kurejea kwa washambuliaji Tegete na
Coutinho ambao naamini wataongeza
nguvu na kutuletea ushindi kwenye
mchezo wa Jumapili (kesho),"
alisema Maximo.
Uwepo wa Coutinho, Tegete na
Mbrazili mwingine 'Jaja' kwenye safu
ya ushambuliaji na kucheza kwenye
Uwanja wa Taifa kunampa Maximo
moyo wa kuibuka na ushindi wake wa
kwanza nchini kama kocha wa klabu
ya ligi kuu ya Bara.
Maximo ambaye alikuwa mwalimu wa
Taifa Stars kwa miaka minne tangu
mwaka 2006, amesema beki wa
kushoto Oscar Joshua aliyeumia
kwenye mchezo dhidi ya Mtibwa na
mshambuliaji Hussein Javu
hawatacheza.
Wote wanauguza maumivu ya nyama
za paja.
"Wachezaji wengine wote wapo katika
hali nzuri na naamini wataniletea
ushindi."
Kukosekana kwa Joshua kunatarajiwa
kumfanya Maximo amrudishe Mbuyi
Twite kucheza beki ya kushoto.
Maximo ambaye pamoja na timu yake
wanapewa nafasi kubwa zaidi ya
kutwaa ubingwa wa Bara msimu huu,
alishindwa kuzuia mwendelezo wa
rekodi mbaya dhidi ya Mtibwa kwenye
uwanja wa Jamhuri kwa miaka ya
karibuni timu yake ilipofungwa 2-0.

PATA BRAND NEW VIDEO YA CHRISS BROWN FT. RICK ROSSAY &USHER RAYMOND

DOWNLOAD VIDEO

KAMA HUJAIPATA AUDIO TRACK MPYA YA MAVOCKO PACHA WANGU...DOWNLOAD HAPA

DOWNLOAD

Thursday, September 25, 2014

NEW TRACK: MKUBWA NA WANAWE-MSAMAHA

BOFYA HAPA KUI DOWNLOAD

BRAND NEW TRACK BY MKUBWA NA WANAWE-BORA KIJIJINI

DOWNLOAD

BRAND NEW VIDEO BY RICH MAVOCKO-PACHA WANGU

MSANII ALIEKUA KIMYA KWA MUDA MREFU KIDOGO BAADA YA KUACHIA WIMBO WAKE WA ROHO YANGU SASA ADONDOKA NA TRACK NYINGINE INAYOENDA KWA JINA LA PACHA WANGU

   BOFYA HAPA KUICHEK NA KU DOWNLOAD

PATA LYRICS ZA NYIMBO MBALIMBALI KUANZIA SASA TUNAANZA NA WIMBO WA TYGA-FADED

Faded"
(feat. Lil Wayne)
(Intro)
I don't give a fuck
{Tyga tyga tyga nice to see you}
[Tyga]
Young Nino, fuck a bitch in a pea
coat
Carlito, Scarface, AL Pacino
Bun B do, Pimp C, R-PIDO though
I goes deep in that pussy, Dan
Marino
She wanna be the one, fuck her to my
own single
Break a bitch heart, no future miss
cleo
Snap back, au-au-automatic reload
Flyer than a fucking beatle, you can't
beat 'em
Vampire fuck up your evening
I pop up and eat lunch, leave you in
the cement
Don't believe it, stripe like a fucking
Adidas
The gun selena, give a nigga bieber
fever
Real fucking hot, put it in park
Take a shot, higher than a tube sock
You a bop, give me top top, as I load
the guap
Man these niggas say I'm fly but to
her I'm god
[Hook]
I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
And I don't give a fuck
[Tyga]
Fuck is up, nigga's stomping in my
chucks
Yeah, I make it rain, dear, cause I'm
all about my bucks
Use the butt I'm in the front, dick up
in her cunt
And I put it in her hole, hole in one,
putt putt (wahhhhhh)
Super McNasty, why you McLoving
When the bitch call me daddy
Pimp no caddy, she wish she never
had me
Treat her like a dog, called the bitch
lassy
Young savvy, bang her like Cincinnati
Above average, fly like I'm Aladdin
They bend backwards, throw the
pussy at them
I'm Ben Wallace, dunk up in your
basket
Balls in the air, no games,
I'm serious, double dare
There's too many bitches,
Why these niggas wanna stare
Patron up in here
Nigga this ain't no beer
[Hook]
I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
And I don't give a fuck
[Lil' Wayne]
Mama, there go that monster
Abracadabra, magic Johnson
My motherfucking doctor
Said I need a doctor
So I called house,
Now I am a pill popper
Faded like skinnys
Young money we winning
I told her if I change
She won't get a penny
Milking that shit, pregnant bitch
titties
Bringing home the bacon
I'm fucking miss piggy
Loaded like a semi, semi-naked
pictures
She knows my dick, she call it nigga
Richard
Prior to me cummin, I had to stick my
thumb in
Her ass one time, smell my finger
make you vomit
Flyer than a hornet, the shoe fit I
worn it
She tried to jack me off, can't beat it,
join it
Tunechi, coochie that what she call
it,
Flag Scarlett, I killed it, mourn it
[Hook]
Faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
[Lil Wayne:] Young Moolah baby!
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
And I don't give a fuck

WASANII WAHAMASISHWA KUSHIRIKI KWENYE SIKU YA SANAA

Viongozi wa mashirikisho ya filamu
na sanaa za ufundi wamewataka
wasanii wa fani mbalimbali kujitokeza
katika kushiriki semina
zitakazoendeshwa katika Siku ya
Msanii Tanzania.
Semina ya Siku ya Msanii inatarajiwa
kufanyika Oktoba 22 na 23 mwaka huu
katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere
(Makumbusho Posta) na wasanii
watafundishwa mambo
mbalimbali.Rais wa Shirikisho la
Sanaa za Ufundi, Adrian Nyangamale,
alisema wasanii wanapaswa
kujiandikisha kwenye semina hizo ili
kupata ujuzi wa mambo mbalimbali.
“Semina hizi ni muhimu kwa sababu
kutakuwa na wataalamu kutoka katika
sekta mbalimbali ambao watakuja
kutoa mafunzo kwenye semina hizo,
jambo ambalo litachangia uelewa na
elimu ya wasanii, tumekuwa
tukilalamika kuwa hatupati fursa za
elimu lakini Siku ya Msanii imetupa
hiyo nafasi sasa tuitumie,” alisema.
Naye Makamu wa Rais wa Shirikisho
la Filamu, Selemani Ling’ande alisema
wasanii wajitokeze kwenye semina
hizo lakini pia aliwataka wananchi
kujitokeza kwa wingi katika kupiga
kura za kupata watu watakaowania
tuzo za Siku ya Msanii.
“Semina ni muhimu lakini kuna suala
la kutambulika mchango wa wasanii,
hapa ndiyo Watanzania
wanapotakiwa kufanya mapendekezo
yao, kuna fomu zinatolewa kwenye
magazeti na mitandao juu ya Tuzo za
Humanitarian Award na Life Time
Achievement ambazo wasanii wote
wanaweza kushindanishwa,” alisema.
Naye Mkurugenzi wa Kampuni ya
Haak Neel Production, Godfrey Katula,
ambaye kampuni yake ndiyo imepewa
jukumu la kusimamia Siku ya Msanii,
alisema Watanzania wajitokeze
kupendekeza majina ya wasanii
wanaostahili kupata tuzo na Kamati
ya Utafiti itakwenda kuhakiki taarifa
zote zilizowasilishwa kwao.
“Kazi za wasanii zinaanza
kutambulika hapo, wananchi
wanawajua hivyo ni fursa yao
kuonyesha kuthamini kazi zao, lakini
pia tunawataka wasanii wajitokeze
kwenye semina ambazo zitafanyika
kwa siku mbili ili kupata elimu
sahihi,” alisema.
Siku ya Msanii inaandaliwa na
Kampuni ya Haak Neel Production
kwa kushirikiana na Baraza la Sanaa
la Taifa (BASATA).

CHADEMA NA POLISI WAENDELEA KUZOZANA

Jeshi la Polisi limeendelea
kusuguana na Chama cha Demokrasia
na Maendeleo (Chadema) wakati
wafuasi wa chama hicho wakitaka
kuandamana huku polisi
wakiwadhibiti.
Mkoani Kagera, Jeshi la Polisi
limepanga askari wake kila mtaa
katika manispaa ya Bukoba kwa lengo
la kudhibiti maandamano hayo.
Kaimu Kamanda wa polisi mkoani
Kagera, Gilles Muroto, alisema
kupangwa kwa askari hao
kumetokana na kutoeleweka
maandamano ya wafuasi wa chama
hicho yataanzia katika mtaa upi.
“Tunafahamu siku ya kwanza tutapata
changamoto kutokana na askari
wengi kupangwa kudhibiti
maandamano hayo, lakini kadri
tunavyoendelea tutajipanga vizuri
hakuna shughuli ya kuhudumia
wananchi itakayokwama,” alisema
Muroto.
Alisema kuwa Septemba 22 mwaka
huu walipokea barua ya Chadema
wakiomba kuandamana kesho yake
kuanzia saa 3:00 asubuhi, lakini
maombi hayo hayakukubaliwa
kutokana na kupigwa marufuku na
makao makuu ya jeshi hilo.
Jijini Dar es Salaam, jana polisi
walizizingira ofisi za Chadema makao
makuu kudhibiti wafuasi wa chama
hicho wasiandamane.Askari hao
wakiwamo wa Kikosi cha Kutuliza
Ghasia (FFU), walikuwa katika doria
wakiwa kwenye magari mawili aina ya
Land Rover pamoja na silaha za moto.
Hali hiyo iliwafanya wafuasi wa
Chadema kukaa katika vikundi
wakijadili hali ilivyo katika maeneo ya
kuingilia katika makao makuu ya
chama hicho.Afisa Habari wa
Chadema, Tumaini Makene alisema
wanalishukuru jeshi hilo kwa
kuwasaidia kuandamana katika
maeneo mbalimbali ya nchi.
Aliongeza kuwa wana njia 198 za
kuandamana ikiwa ni pamoja na
kuwatumia ujumbe mfupi viongozi wa
Bunge Maalumu la Katiba kuwaeleza
kuwa hatufurahishwi na
kinachoendelea bungeni.
Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es
Salaam, Suleman Kova, alisema
wamejipanga kudhibiti fujo
zitakazotokea. Jijini Mwanza,
Mwenyekiti wa Chadema wa mkoa wa
mwanza, Adrian Tizeba, jana alitiwa
mbaroni na Polisi, baada ya kufanya
mkutano wa waandishi wa habari
kuzungumzia maandamano.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa huo,
Valentino Kilowoko, alithibitisha
kukamatwa kwa Tizeba na kusema
walikuwa wanaendelea kumhoji.
Kabla ya kukamatwa, Tizeba alilitaka
Jeshi la Polisi mkoani humo
kushirikiana nao katika maandamano
ya amani yatakayofanyika leo kupinga
Bunge la Katiba linaloendelea mjini
Dodoma.
Alisema licha ya polisi wilaya zote za
mkoa wa Mwanza kukataa barua za
taarifa za kuwapo maandamano hayo,
lakini wamekusudia kuandamana na
kuwaomba polisi nao washiriki.
“Haya ni maandamano ya amani,
tunaomba hata polisi washiriki nasi
kesho (leo) ili kufikisha ujumbe wa
matumizi mabaya ya pesa za umma
katika bunge hilo linaloendelea
Dodoma hivi sasa,” alisema Tizeba.

ZITTO KABWE KUWAPATANISHA DIAMOND NA ALI KIBA

Mbunge wa Kigoma Kaskazini
(Chadema), Zitto Kabwe, amejitosa
kusuluhisha ugomvi wa muda mrefu
wa wasanii wawili wa muziki wa
kizazi kipya nchini, Ali Kiba na
Nasibu Abdul 'Diamond'.
Zitto alitoa kauli hiyo juzi wakati
akihojiwa katika Kipindi cha Mkasi
kinachorushwa na Kituo cha
Televisheni cha EATV baada ya
kuulizwa kuwa ni jitihada gani
amezifanya kusuluhisha ugomvi wa
wasanii hao akiwa kama mlezi wa
wasanii wanaotoka mkoani Kigoma.
Alisema anafahamu kuwapo kwa
ugomvi wa kutoelewana kati ya
wasanii Ali Kiba na Diamond na
kwamba alishawahi kufanya jitihada
za kuwaita kila mmoja kwa nyakati
tofauti.
Alifafanua kuwa katika kuhakikisha
anawasuluhisha wasanii hao,
anaifanya kazi hiyo kwa umakini kwa
sababu hataki kuonekana anaingilia
maisha ya watu na kwamba ana imani
atafanikiwa kuwapatanisha.
Kuhusu madai kwamba ana uhusiano
wa kimapenzi na msanii Mwasiti
Almas, alisema ni kweli kumekuwapo
na uvumi huo lakini kimsingi hana
uhusiano wowote wa kimapenzi na
msanii huyo.
"Nasikitishwa na madai hayo
yanayotolewa na baadhi ya watu,
Mwasiti ni kama dada yangu ambaye
nimekuwa nikimsaidia katika kazi
zake, kuhusishwa naye kimapenzi ni
jambo linalonisononesha,"alisema.
Zitto alisema wanaomhusisha katika
suala la mapenzi na msanii huyo ni
kwa sababu Mwasiti ameimba wimbo
ambao amemtaja yeye (Zitto) lakini
kiukweli hana uhusiani naye wa
kimapenzi.
Alipoulizwa ni lini ataoa, alisema
bado 'yupo yupo' na kwamba kuna
mwanamke aliyemtaja kwa jina la
Jack ambaye amezaa naye mtoto
ambaye kwa sasa miaka nane na
anasoma darasa la pili nchini Uganda.
KAMPUNI YA LEKA DUTIGITE
Kuhusu Leka Dutigite inayounganisha
wasanii wa Kigoma All Stars, alisema
ni kampuni ambayo kila msanii
anayetoka mkoani Kigoma ana hisa
na ikipata faida wanagawana.
Zitto alisema Leka Dutigite pia
inamiliki kampuni nyingine ambayo
imekuwa ikipata kazi mfano katika
Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa) na
yeye kama mlezi amekuwa akitoa
fedha zake kusaidia.

WAREMBO WA MISS TANZANIA WATALII MTO WA MBU

Warembo wanaotarajia kushiriki
shindano la urembo la taifa mwaka
huu "Redd's Miss Tanzania 2014" leo
wanatarajia kutembelea eneo la Mto
wa Mbu kushuhudia maajabu yaliyoko
kwenye mto huo ulioko Karatu
mkoani Arusha ikiwa ni sehemu ya
kufanya utalii wa ndani
Akizungumza na gazeti hili jana kwa
njia ya simu, Ofisa Habari wa Kamati
ya Miss Tanzania, Haidan Rico,
alisema kuwa wakiwa eneo hilo,
warembo walipewa maelezo muhimu
kuhusiana na mto huo na dhumuni la
kuwatembeza warembo hao katika
vivutio mbalimbali ni kutaka
kushawishi jamii kufanya utalii
Rico alisema kuwa wanaamini
warembo hao watafikisha ujumbe
katika familia zao na kubadili mawazo
kwamba utalii ni kwa ajili ya wageni
pekee.
Alisema kuwa kesho Jumanne
warembo hao wataelekea Ngorongoro
Crater kuona jinsi eneo hilo
lilivyobonyea kufuatia mlipuko wa
volkano.
Alisema kuwa tayari warembo hao
wameshatembelea katika lango la
kupanda mlima Kilimanjaro na
kuelezwa mazingira yanayozunguka
eneo hilo, Tarangire na kufanya kazi
za kijamii kwenye hospitali za Kilema
na Marangu ambapo walitoa misaada
ya sabuni, vyandarua, dawa ya meno,
miswaki na mafuta ya kujipaka kwa
watoto na wanawake waliolazwa
kwenye hospitali hizo.
Pia washiriki hao walitembelea
Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa
Kilimanjaro (KIA) na wakiwa hapo
walijifunza mbinu ambazo askari
wanatumia kukagua abiria ambao
wanasafiri na bidhaa zisizoruhusiwa
kama vile dawa za kulevya.
Pia alisema washiriki watamtembelea
Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mjini na
baadaye Hifadhi ya Mbuga ya Arusha.
Warembo hao 30 kutoka mikoa
mbalimbali nchini ambao wako katika
ziara hiyo ni pamoja na Dorice Mollel,
Sofia Masey, Lilian Timothy, Junes
Ndalima, Maureen Godfrey, Martha
John, Naba Magambo, Raisa Julius,
Happiness Samuel, Evelyn Baasa,
Lilian Kamazima, Elizabeth Tarimo,
Nidah Katunzi, Lucy Diu, Mariam
Hussein, Maria Shilla, Camilla John,
Queen Latifa Hashim na Dorren Beno.
Warembo wengine ni Sitti Mtemvu,
Salama Saleh, Patricia Pontain,
Rachel Clavery, Mary Emmanuel,
Nicole Sarakikya, Dorren Robert,
Jihan Dimachk, Nasreen Abdul,
Sabina Thomas na Happinness
Sosthenes.
Happiness Watimanywa kutoka
mkoani Dodoma ndiye mrembo
anayeshikilia taji hilo la taifa na
baadaye mwaka huu ataiwakilisha
nchi kwenye fainali za urembo za
dunia.

TANZANIA YASHUKA VIWANGO FIFA

Tanzania imeporomoka tena kwenye
viwango vya soka vinavyotolewa kila
mwezi na Shirikisho la Soka la
Kimataifa (Fifa), baada ya kuanguka
kwa nafasi tano katika viwango
vilivyotolewa jana.
Tanzania, ambayo ilifungwa 2-0 na
Burundi katika mechi ya kimataifa ya
kirafiki iliyopita, sasa inakamata
nafasi ya 115 duniani na 33 barani
Afrika ikiwa nyuma ya Uganda
wanaoongoza Afrika Mashariki
wakiwa nafasi ya 79 duniani na 19
Afrika, Rwanda walioko nafasi ya 93
duniani na 25 Afrika na Kenya
walioporomoka kwa nafasi saba
wakiwa nafasi ya 30 Afrika na 111
duniani.
Aligeria waliopanda kwa nafasi nne,
wanaongoza barani Afrika wakiwa
nafasi ya 20 duniani wakifuatwa na
Ivory Coast walioshuka kwa nafasi
tatu baada ya kukubali kichapo cha
mabao 4-1 kutoka kwa Cameroon
waliopanda kwa nafasi 12 na
kukamata nafasi ya nane Afrika na 42
duniani.
Nafasi ya tatu barani Afrika inakaliwa
na Tunisia (31) wakipanda kwa nafasi
11 wakifuatwa na Ghana (33), Senegal
(36), Nigeria (37) na Cape Verde (41).
Guinea waliopanda kwa nafasi 16
wanakamata nafasi ya tisa barani
Afrika na 48 duniani huku Burkina
Faso waliopanda kwa nafasi 10
wakifunga pazia la 10 bora barani
Afrika wakifungana na Guinea katika
nafasi ya 48 duniani.
Uganda pia ni wa kwanza katika
Ukanda wa Cecafa wa Afrika Mashariki
na Kati wakifuatwa na Rwanda,
Kenya, Tanzania, Burundi, Ethiopia
(39, 132), Sudan (40, 133), Shelisheli
(47, 172), Sudan Kusini (50, 185),
Eritrea (52, 202), Somalia (53, 204)
huku Djibouti wakifunga mlango
Cecafa na Afrika wakiwa 54 Afrika na
205 duniani.
Mabingwa wa dunia, Ujerumani
wanaongoza 10 bora ulimwenguni
wakifuatwa na Argentina, Colombia
waliopanda kwa nafasi moja
wakiwashusha Uholanzi, Ubelgiji,
Brazil, Uruguay, Hispania, Ufaransa
na Uswis.

Wednesday, September 24, 2014

OKWI ADAI KUA YANGA WATATULIA TU

Licha ya kupika mabao yote ya Simba
katika mechi yao ya kwanza ya Ligi
Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL)
msimu huu waliyotoka 2-2 dhidi ya
Coastal Union kwenye Uwanja wa
Taifa, Dar es Salaam juzi,
mshambuliaji Emmanuel Okwi
amesema hakuwa katika kiwango
chake.
Okwi, aliyejiunga na Simba dakika za
mwisho kabla ya kufungwa kwa
dirisha la usajili msimu huu akitoka
Yanga, alisababisha mabao yote ya
Simba juzi licha ya mashabiki wa
Yanga kumzomea mwanzo mwisho
jambo analoamini muda si mrefu
watatulia baada ya kurejea katika
makali yake.
Bao la kwanza la Simba lilipatikana
baada ya Okwi kukwatuliwa nje ya
mstari wa eneo la hatari la Coastal
Union, hivyo adhabu hiyo kuzaa
matunda kupitia kwa mpigaji Shabani
Kisiga kabla ya Mganda huyo tena
kutoa pasi ya mwisho ya bao la pili
kwa mfungaji bora wa VPL msimu
uliopita, Mrundi Amissi Tambwe.
Kisiga alifunga kwa 'frikiki'
iliyomshinda kipa wa Coastal, Shaban
Kado wakati mabao ya mabingwa hao
wa Tanzania Bara 1988 yalifungwa na
mtokea benchi Lutimba Yayo na
mshmbauliaji wa zamani wa Gor
Mahia ya Ligi Kuu ya Kenya, Rama
Salim.
Mara tu baada ya mechi hiyo
iliyochezeshwa na refa Jacob Adongo
kutoka Mara kumalizika, Okwi
aliliambia NIPASHE kuwa bado
hajafikia katika kiwango chake cha
kusakata soka.
“Mara nyingi sipendi kuzungumzia
kiwango changu binafsi kuliko cha
timu, tulicheza vizuri kipindi cha
kwanza na Coastal walicheza vizuri
kipindi cha pili,” alisema Okwi.
“Sijafurahishwa sana na kiwango
nilichoonyesha leo (juzi), nitajitahidi
kuongeza mazoezi ili mechi ijayo
niisaidie timu yangu kupata ushindi,”
alisema zaidi Mganda huyo ambaye
muda wote wa mechi ya juzi alikuwa
akizomewa na mashabiki wa Yanga
waliokuwa wameingia uwanjani
kutazama mechi hiyo.
Alipoulizwa juu ya zomea zomea
inayofanywa na mashabiki wa Yanga
dhidi yake, Okwi alisema: “Sina muda
nao, mimi nimeshakuwa mchezaji
halali wa Simba, mambo yote
kuhusiana na Yanga hayanihusu.
Ninaamini nitakapokuwa katika
kiwango changu, hawatanizomea
tena,” alisema.
Okwi, mchezaji wa zamani wa SC Villa
ya Ligi Kuu ya Uganda na Etoile du
Sahel ya Tunisia, amejiunga na Simba
baada ya uongozi wa Yanga
kuwasilisha nyaraka katika Shirikisho
la Soka Tanzania (TFF) zikionyesha
kuwa mkataba wake wa miaka miwili
na nusu na klabu hiyo ya Jangwani
aliousaini Desemba 13, mwaka jana,
umevunjwa.

MAGOLI 18 LIGI KUU YASHINDWA KUVUJA REKODI

Magoli 18 yamefungwa kwenye mechi
saba za ufunguzi wa Ligi Kuu
Tanzania Bara iliyoanza Jumamosi
iliyopita, lakini yameshindwa kuvunja
rekodi ya magoli ya msimu uliopita.
Kwenye mechi za ufunguzi wa Ligi
Kuu msimu uliopita jumla ya magoli
19 yalipatikana.
Ligi ya msimu huu imeanza kwa Azam
FC kuitandika Polisi ya Morogoro
mabao 3-1, Mtibwa Sugar kuichapa
Yanga mabao 2-0, Stand United ya
kutandikwa nyumbani mabao 4-1
dhidi ya Ndanda FC kutoka Mtwara,
wakati Mgambo JKT ya Tanga
iliifunga Kagera Sugar bao 1-0.
Mechi nyingine ilikuwa ni Ruvu
Shooting kupata kipigo nyumbani cha
mabao 2-0 kutoka kwa Prisons ya
Mbeya, Mbeya City kulazimishwa sare
ya bila kufungana dhidi ya JKT Ruvu,
huku Simba ikibanwa mbavu katika
sare ya 2-2 dhidi ya Coastal Union,
hivyo kuzaa mabao 18.
Magoli 19 ya mechi ya ufunguzi
msimu uliopita kwa mujibu wa
kumbukumbu zetu yalipatikana kwa
Yanga kuinyuka Ashanti mabao 5-1,
Mtibwa kutoka sare ya bao 1-1 dhidi
ya Azam, JKT Oljoro ikainyuka
Coastal Union mabao 2-0, Mgambo
ikachapwa 2-0 dhidi ya JKT Ruvu,
Simba ikatoka sare ya mabao 2-2
dhidi ya Rhino ya Tabora, Mbeya City
ikatoka sare ya bila kufungana dhidi
ya Kagera Sugar na Ruvu Shooting
ikaitandaika Prisons mabao 3-0.
Katika hatua nyingine, mchezaji wa
Mgambo Shooting Ramadhani Pera
ameweka rekodi ya kuwa mchezaji wa
kwanza kufunga bao kwenye Ligi kuu
alipofunga bao pekee dhidi ya Kagera
Sugar katika dakika ya 12 kwenye
raundi ya kwanza ya ligi hiyo
Jumamosi.
Mabao yote yaliyopatikana kwenye
mechi nyingine yalifungwa baada ya
dakika hizo.
Shaaban Kisiga wa Simba anashikilia
rekodi ya kufunga bao la mapema
zaidi katika dakika ya saba dhidi ya
Coastal katika mechi ya kufunga
raundi ya kwanza Jumapili.

TIKETI ZA KIELEKTRONIKI ZAANZA KUJIBU

Mfumo wa tiketi za elektroniki katika
mechi za soka nchini umeanza kuzaa
matunda baada ya jana Shirikisho la
Soka Tanzania (TFF), kuweka wazi
kwamba mapato ya milangoni
yameongezeka.
Akizungumza na waandishi wa habari
jijini Dar es Salaam jana mchana,
Mkurugenzi wa Mashindano wa
shirikisho hilo, Boniface Wambura,
alisema utumiaji wa tiketi za
elektroniki umefanikiwa kudhibiti
hujuma za mapato ya milangoni
kwenye viwanja ambavyo tayari
vimeshasimikwa mfumo huo.
Wambura alisema kwa sasa wanapata
mapato halisi ya mechi husika
kulingana na idadi ya watu waliokata
tiketi.
“Hatutarudi nyuma katika hili,
tutaendelea kutumia tiketi za
elektroniki kwenye viwanja vyote
vilivyosimikwa mfumo huu,” alisema
Wambura na kuongeza: “Kuna viwanja
kama CCM Kirumba jijini Mwanza na
Sheikh Amri Abeid jijini Arusha vina
mfumo huu lakini havitumiwi na timu
za Ligi Kuu.
Tutahakikisha mechi za Ligi Daraja la
Kwanza zinazochezwa kwenye
viwanja hivyo vinatumia tiketi za
elektroniki ili watu waishio katika
majiji hayo pia wauzoee.”
Mkurugenzi huyo alisema watu wote
wanaojaribu kuingia viwanjani kwa
kutumia tiketi feki wamekuwa
wakinaswa kwa kutumia mashine za
utambuzi wa tiketi za elektroniki
(PDA), hivyo kwa sasa hakuna mtu
anayeingia kwenye viwanja vilivyo na
mfumo huo akitumia tiketi bandia.
Akitangaza mapato ya mechi za wiki
iliyopita za Ligi Kuu ya Vodacom
Tanzania Bara (VPL), Wambura
alisema yameongezeka kwa kiasi
kikubwa, sababu kubwa akisema ni
matumizi ya mfumo wa tiketi za
kisasa za kielektroniki.
Wambura alisema mechi ya Mtibwa
Sugar dhidi ya Yanga iliyochezwa
kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini
Morogoro Jumamosi na kumalizika
kwa wenyeji kuibuka na ushindi wa
mabao 2-0, imeingiza Sh. milioni 59
kutokana na viingilio vya mashabiki
11,499 waliokata tiketi za Sh. 5,000.
Mapato hayo ni ongezeko la Sh.
milioni 12 ikilinganishwa na mapato
ya mechi kati ya timu hizo kwenye
uwanja huo msimu uliopita.
Aidha, Wambura alisema kuwa mechi
ya Simba dhidi ya Coastal Union
iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa
jijini Dar es Salaam Jumapili huku
timu hizo zikitoka sare ya mabao
mawili, imeingiza Sh. milioni 124.7
zilizotokana na viingilio vya
mashabiki 22,114 waliokata tiketi
kuingia kwenye uwanja huo wenye
uwezo wa kuketisha watazamaji
57,558.
Simba na Coastal Union ziliingiza Sh.
milioni 36.8 zilipokutana katika mechi
ya ligi hiyo kwenye uwanja huo
msimu uliopita.
Utumiaji wa tiketi hizo za kielektroniki
ni utekelezaji wa mapendekezo
yaliyomo kwenye ripoti ya Kamati
Maalum ya Kudhibiti na Kuboresha
Mapato ya TFF iliyotolewa 2011 na
agizo la serikali lililotolewa katikati
ya mwaka huu.
Mei 2011 Kamati Maalum ya Kudhibiti
na Kuboresha Mapato ya TFF
iliyoongozwa na Rais Mstaafu wa
shirikisho hilo, Leodegar Tenga, ilitoa
ripoti yenye kurasa 95 ikionesha
uhujumu mkubwa wa mapato
utokanao na matumizi ya tiketi za
kawaida, hivyo kamati ikapendekeza
TFF ianze kutumika tiketi za kisasa za
kielektroniki.
Aidha, Juni mwaka huu, serikali
iliiagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania
(TRA) kuiiamuru TFF kutumia mfumo
wa tiketi za kielektroniki kwenye
viwanja mbalimbali vya soka nchini ili
kudhibiti uhujumu wa mapato ya
milangoni.
Akiwasilisha taarifa ya Kamati ya
Bunge ya Uchumi, Viwanda na
Biashara kuhusu utelezaji wa
majukumu ya Wizara ya Fedha na
Uchumi kwa mwaka wa fedha 2014/15
Bungeni mjini Dodoma Juni 4, mwaka
huu, mwenyekiti wa kamati hiyo,
Luhaga Mpina aliitaka TRA kutoa
sharti kwa TFF kutumia mfumo wa
tiketi za elektroniki ili kuongeza
mapato ya nchi.
"Kamati inashauri TRA iweke sharti la
lazima la kuitaka TFF kutumia mfumo
wa tiketi za kielektroniki katika kuuza
tiketi zake ikiwa ni jitihada za
kuongeza mapato ya serikali," alisema
Mpina.
Mbunge huyo wa Kisesa (CCM),
alisema kwa muda mrefu serikali
imekuwa haipati mapato ya kutosha
kutoka katika sekta ya michezo
hususan mpira wa miguu ulio chini ya
TFF kutokana na mfumo dhaifu wa
ukusanyaji fedha kipindi cha kuuza
tiketi.

KIONGERA KUIKOSA YANGA

Mshambuliaji Paul Kiongera wa
Simba huenda akaikosa mechi ya
kwanza dhidi ya watani wao wa jadi,
Yanga msimu huu wa Ligi Kuu ya
Vodacom Tanzania Bara itakayopigwa
kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es
Salaam Oktoba 12 baada ya kuumia
goti katika mechi iliyopita.
Kiongera alitokea benchi dakika ya 67
akichukua nafasi ya mfungaji bora wa
msimu uliopita, Mrundi Amissi
Tambwe, lakini dakika mbili kabla ya
mechi hiyo waliyotoka 2-2 dhidi ya
Coastal Union kumalizika, Mkenya
huyo alilazimika kumpisha Amri
Kiemba baada ya kugongana na kipa
Shaaban Kado wa Coastal na kuumia.
Taarifa zilizolifikia NIPASHE jana
kutoka ndani ya uongozi wa Simba
zilieleza kuwa Kiongera ameumia goti
na jana alipelekwa Hospitali ya Taifa
Muhimbili kufanyiwa vipimo.
Mmoja wa viongozi wa Simba (jina
tunalo) alisema mchezaji huyo ana
maumivu sugu ya goti hilo baada ya
kuumia awali akiwa kwao, Kenya.
Kiongozi huyo alisema Kiongera
anaweza kuwa nje ya uwanja kwa
muda wa kati ya wiki sita hadi miezi
miwili kabla ya kuanza mazoezi
mepesi, hivyo hatacheza mechi ya
Oktoba 12 ya watani wa jadi Simba na
Yanga.
Alibainisha kuwa kumeibuka hali ya
wasiwasi ndani ya Simba kwamba
huenda hawakufanya uamuzi sahihi
kumsajili Mkenya huyo kabla ya
kumfanyia vipimo vya afya.
Majeruhi wengine wa Simba ni beki
wa kushoto Issa Rashid ‘Baba Ubaya’
aliyeumia nyama za paja wiki mbili
zilizopita mazoezini, ambaye
inaelezwa kuwa yuko katika wiki ya
mwisho ya mapumziko na winga
Haruna Chanongo aliyeumia goti pia
Jumapili wakati wakichuana na
Coastal. Imeelezewa kuwa Chanongo
atakuwa nje kwa siku nne tangu
kuumia kwake.
Habari njema zaidi kwa Simba kwa
sasa ni kurejea kwa kiungo
mpambanaji Jonas Mkude, ambaye
Daktari wa Simba, Yassin Gembe
amesema anaweza kuanza kucheza
hata Jumamosi dhidi ya Polisi
Morogoro endapo kocha atampanga.
“Ni uamuzi wa kocha tu, lakini ukweli
ni kwamba Mkude yuko fiti kabisa
kwa sasa na anaweza kuanza
kucheza, uzuri ni kwamba pamoja na
kuwa nje kwa muda mrefu, lakini
hajaongezeka uzito,” alisema Gembe.
Mkude hajawahi kuichezea Simba
chini ya kocha aliyerejea kwa mara ya
tatu nchini kuinoa timu hiyo,
Mzambia Patrick Phiri. Katika mechi
iliyopita kiungo Mrwanda Pierre
Kwizera alicheza nafasi ya Mkude
lakini alionekana wazi kutoimudu.
Baada ya Chanongo kuumia, winga
Uhuru Seleman aliingizwa lakini
baada ya mechi kumalizika huku
Coastal wakirudisha mabao yote,
Phiri aliweka wazi kwamba pengo la
Chanongo halikuzibika ipasavyo.
Kikosi cha Simba kilirejea tena
kambini visiwani Zanzibar kujiandaa
kwa mechi yao inayofuata Jumamosi
dhidi ya Polisi Morogoro.

KATIBA MPYA YATAKA RAIS KUA NA MADARAKA ZAIDI

Rasimu ya Katiba inayopendekezwa
na Bunge Maalum la Katiba,
imeongeza madaraka ya Rais
maradufu na kuondoa matakwa ya
rais kuzingatia masharti ya
uthibitisho wa Bunge katika nafasi za
madaraka na kumuachia uteuzi wa
moja kwa moja.
Akiwasilisha rasimu hiyo bungeni
jana, Mwenyekiti wa Kamati ya
Uandishi, Andrew Chenge, aliyataja
mambo mbalimbali yaliyofutwa,
yaliyoongezwa na yaliyoboreshwa
katika Rasimu ya Jaji Warioba.
Kwa mujibu wa Rasimu iliyotolewa
Desemba 31, 2013 na Mwenyekiti wa
Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji
Mstaafu Joseph Warioba, ilipendekeza
nafasi zote za uteuzi kupendekezwa
na mabaraza ya kisekta kabla ya Rais
kufanya uteuzi miongoni mwa majina
hayo kisha kuthibitishwa na Bunge
Ibara ya 73 (3) ya Rasimu ya Warioba
imependekeza kuwa Katika
utekelezaji wa madaraka kama
ilivyoainishwa katika ibara ndogo ya
(1) na (2), Rais atazingatia masharti
kuhusu uthibitisho wa Bunge katika
nafasi za madaraka na vile vile
ushauri wa mamlaka za Serikali,
Bunge au Mahakama zilizopewa
madaraka ya kumshauri katika
kufanya uteuzi, kuanzisha au kufuta
nafasi za madaraka katika utumishi
wa Serikali.
Aidha, ibara ya 74 (1) ya Rasimu ya
Warioba ilipendekeza kuwa mbali na
kuzingatia masharti yaliyomo katika
Katiba hii, na sheria za nchi, Rais
atakuwa na wajibu wa kufuata na
kuzingatia ushauri atakaopewa na
mamlaka za nchi, na endapo
hakubaliani na ushauri aliopewa,
sharti atoe sababu katika Baraza la
Mawaziri kuhusu sababu ya
kutokubaliana na ushauri aliopewa.
Nafasi pekee ya uongozi ambayo
baada ya uteuzi wa Rais itapaswa
kuthibitishwa na Bunge ni ya Waziri
Mkuu, wakati Rasimu ya Pili ya Jaji
Warioba mbali na Waziri Mkuu,
ilipendekeza, Mwanasheria Mkuu wa
Serikali, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu
wa Hesabu za Serikali, Jaji Mkuu, na
Mkurugenzi na Mashtaka
kuthibitishwa na Bunge.
Nafasi za uteuzi ambazo
hazitathibitishwa na Bunge ni
Mawaziri, Manaibu Waziri, Katibu wa
Bunge, Mwanasheria Mkuu,
Mkurugenzi wa Mashtaka, Katibu
Mkuu Kiongozi, Wakuu wa mikoa wa
Bara.
MAHAKAMA
Rasimu hiyo imependekeza Jaji
Mkuu, Naibu Jaji Mkuu, Jaji wa
Mahakama ya Juu, Naibu Jaji Mkuu,
Mwenyekiti wa Mahakama ya Rufani,
Makamu Mwenyekiti, ambao
watateuliwa na Rais kutoka majina
matatu yaliyopendekezwa na Tume ya
Utumishi wa Mahakama.
Wengine ni Msajili Mkuu wa
Mahakama atateuliwa kutokana na
mapendekezo ya Tume ya Utumishi
wa Mahakama, Mtendaji Mkuu wa
Mahakama atateuliwa kutoka majina
matatu ya watumishi wa umma
yaliyopendekezwa na Tume.
TUME YA HURU YA UCHAGUZI
Rasimu hiyo imependekeza
Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na
wajumbe wengine saba
watakaoteuliwa na rais baada ya
kupendekezwa na kamati ya uteuzi.
Aidha, Mkurugenzi wa Tume Huru ya
Uchaguzi atateuliwa na Rais baada ya
kupendekezwa na Tume ya Utumishi
wa umma.
MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA
Rasimu hiyo imependekeza Msajili wa
Vyama vya Siasa na Naibu Msajili,
watateuliwa na rais kutoka majina
matatu yaliyopendekezwa na Tume ya
Utumishi wa Umma.
TUME YA MAADILI YA VIONGOZI WA
UMMA
Imependekeza Mwenyekiti, Makamu
na wajumbe wa Tume ya Maadili ya
Viongozi wa Umma, wateuliwe na rais
kutoka majina yaliyopendekezwa na
Tume ya uteuzi
TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA
UTAWALA BORA
Rasimu hiyo imependekeza
Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti
watateuliwa na Rais kutoka majina
yaliyopendekezwa na Tume ya uteuzi.
CAG
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu
za Serikali (CAG), atateuliwa na Rais
kutoka majina matatu
yaliyopendekezwa na Tume ya
Utumishi wa Umma.
VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Mkuu wa
Jeshi la Polisi (IGP), Mkurugenzi
Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa,
watateuliwa na Rais.
RASIMU YA JAJI WARIOBA
ILIPENDEKEZAJE?
Rasimu ya Jaji Warioba ilipendekeza
Mawaziri, Naibu Mawaziri,
Mwanasheria Mkuu, Katibu Mkuu
Kiongozi na Makatibu Wakuu, Jaji
Mkuu, Naibu Jaji Mkuu, Mwenyekiti,
Makamu Mwenyekiti na wajumbe saba
wa Tume Huru ya Uchaguzi,
Mkurugenzi wa Tume Huru ya
Uchaguzi, Msajili wa Vyama vya
Siasa, Mwenyekiti na Makamu
Mwenyekiti wa Tume ya Maadili ya
Viongozi na Uwajibikaji.
Wengine ni Mwenyekiti na Makamu
Mwenyekiti wa Tume ya Haki za
Binadamu, CAG.Ambao watateuliwa
na Rais na kutothibitishwa na Bunge
bali kushauriana na Baraza la Ulinzi
na Usalama la Taifa ni Mkuu wa
Majeshi ya Ulinzi, Inspekta Jenerali
wa Polisi (IGP) na Mkurugenzi wa
Idara ya Usalama wa Taifa.
IBARA ZILIZOFUTWA
Kamati ya Uandishi BMK imewasilisha
bungeni Rasimu ya Katiba
inayopendekezwa ambayo imefuta
Ibara 28 zilizokuwemo kwenye
Rasimu ya Pili iliyoandaliwa na Tume
ya Mabadiliko ya Katiba, huku
ikizifanyia marekebisho Ibara 186 na
kuingiza Ibara mpya 41.
Chenge alisema kufutwa kwa ibara
hizo pamoja na marekebisho
yaliyofanyika kwenye ibara nyingine
kunatokana na michango ya idadi
kubwa ya wabunge wa BMK wakati
wa mijadala ya kwenye kamati na
ndani ya Bunge na kutokana na
sababu maalum kuna maeneo ambayo
maoni ya wachache yamezingatiwa.
“Rasimu hii inazo Ibara 274, kati yake
ibara 233 zinatokana na rasimu
iliyowasilishwa kwenye bunge hili na
Tume ya Mabadiliko ya Katiba, ibara
186 zimefanyiwa marekebisho ya
kiuandishi na kimaudhui, ibara 47
hazijafanyiwa marekebisho yoyote,
lakini pia ibara 28 zimefutwa na
tumeingiza ibara mpya 41,” alisema
Chenge.
Rasimu ya pili ya Tume ya Mabadiliko
ya Katiba iliyowasilishwa bungeni na
aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume hiyo,
Jaji Joseph Warioba ilikuwa na sura
17 zenye ibara 271.
Katika Rasimu iliyowasilishwa jana
bungeni na Chenge kuna sura 19
zenye ibara 274, hivyo kuwepo kwa
ongezeko la sura mbili na ibara tatu
ikilinganishwa na Rasimu ya Jaji
Warioba.
MAMBO MAPYA
Kwa Mujibu wa Chenge miongoni
mwa mambo makubwa yaliyoongezwa
katika Sura ya Kwanza, Ibara ya Sita
inayozungumzia misingi ya utawala
bora jambo ambalo halikuwemo
kwenye Rasimu ya Jaji Warioba.
Katika Sura ya Pili kwenye Ibara ya 16
yamewekwa masuala yanayohusu
utafiti na maendeleo na katika ibara
ya 17 kuna Dira ya Maendeleo na
Ibara ya 18 inazungumzia Tume ya
Mipango ya Jamhuri ya Muungano na
matumizi ya masharti ya sura ya pili
yakiwa katika ibara ya 20.
Sura ya Tatu ibara ya 22 inayohusu
ardhi huku matumizi bora ya ardhi
yakizaa ibara ya 23 huku mwanamke
akipewa haki ya kumiliki na kutumia
ardhi kama ilivyokuwa kwa
mwanaume.
Aidha katika sura ya nne,
imeongezwa ibara inayozungumzia
utaratibu wa utwaaji wa mali ya umma
iliyotwaliwa na kiongozi aliyefanya
ubadhirifu.
MAMBO YALIYOFUTWA
Chenge aliyataja mambo ambayo
yamefutwa kutoka kwenye Rasimu ya
Jaji Warioba kuwa ni Muundo wa
Muungano wa Serikali tatu uliokuwa
katika Sura ya sita ambao
umebadilishwa na kuependekezwa
kuendelea na Muundo wa Serikali
mbili na nchi moja.
Mambo mengine ni ukomo wa
ubunge, wananchi kupewa mamlaka
ya kumwajibisha mbunge na Mawaziri
kutokuwa wabunge.
Kwa mujibu wa Rasimu
inayopendekezwa, nafasi ya ubunge
haitakuwa na ukomo wa kugombea,
wananchi watamwajibisha mbunge
kupitia uchaguzi baada ya mbunge
kumaliza kipindi chake cha uongozi
cha miaka mitano na mawaziri
wataendelea kupatikana miongoni
mwa wabunge.
YALIYOFANYIWA MAREKEBISHO
Baadhi ya mambo ambayo
yamefanyiwa marekebisho
ikilinganishwa na yalivyokuwa katika
Rasimu ya Jaji Warioba ni Tunu za
Taifa ambazo zimepunguzwa kutoka
saba na kubakia nne.
Tunu zilizowekwa kwenye Rasimu
mpya ni Lugha ya Kiswahili,
Muungano, utu na undugu pamoja na
amani na utulivu.
Katika Rasimu ya Jaji Warioba Tunu
zilizopendekezwa zilikuwa ni utu,
uzalendo, uadilifu, umoja, uwazi,
uwajibikaji na lugha ya taifa.
Chenge alisema marekebisho mengine
yaliyoingizwa katika Rasimu ya
Katiba ni kuongezeka kwa haki za
wanawake, vijana, watoto, watu
wenye ulemavu, wazee na haki za
wasanii.
Marekebisho mengine yapo kwenye
sura ya sita inayohusu uraia, ambapo
watanzania wenye uraia wa nchi
nyingine hawatakuwa na uraia wa
nchi mbili, isipokuwa watapewa
hadhi maalum ya watu wenye asili au
nasaba ya Tanzania, tofauti na
mapendekezo ya Rasimu ya Jaji
Warioba iliyopendekeza watu wa aina
hiyo watakapokuwa ndani Jamhuri ya
Muungano watakuwa na hadhi kama
itakavyoainishwa katika sheria za
nchi.
Katika sura ya nane ya Rasimu
inayopendekezwa na BMK, Rais wa
Zanzibar atakuwa makamu wa pili wa
Rais na Waziri Mkuu atakuwa Makamu
wa tatu wa Rais huku ikitamka
kwamba makamu wa kwanza wa Rais
ni Mgombea Mwenza wa Rais wakati
wa uchaguzi.
Aidha katika sura hiyo ya nane,
Rasimu imependekeza idadi ya
mawaziri kuwa 30 na Naibu Mawaziri
kuteuliwa kutegemeana na mahitaji ya
Serikali.
Katika Rasimu ya Jaji Warioba
ambayo ililenga Muundo wa Serikali
tatu, ilipendekezwa idadi ya Mawaziri
wa Jamhuri ya Muungano na Naibu
Mawaziri haitazidi 15.
Marekebisho mengine yaliyofanywa
kwenye Rasimu inayopendekezwa na
BMK ni suala la Mgombea huru
ambalo katika rasimu hiyo
limewekewa masharti maalum, ikiwa
ni pamoja na idadi ya wapiga kura
wanaohitajika kumdhamini kwa ngazi
ya nafasi anayogomea, kipindi
ambacho amekoma kuwa
mwanachama wa chama chochote cha
siasa kabla ya siku ya uchaguzi,
kutojiunga na chama chochote cha
siasa katika kipindi ambacho atakuwa
kiongozi baada ya kuchaguliwa,
utaratibu wa kuainisha vyanzo vya
ndani na nje vya mapato vya
kugharimia kampeni za uchaguzi,
utaratibu wa kuainisha vigezo na sifa
zitakazotumiwa kuwapata viongozi
wa ngazi za juu kitaifa na kuweka
wazi ilani ya uchaguzi inayoonyesha
mipango ya uendeshaji wa nchi.
Katika Rasimu ya Jaji Warioba,
mgombea huru hakuwekewa mashariti
zaidi ya kuwa na sifa za ujumla
zinazomruhusu kugombea kwa
mujibu wa katiba.
Kwa mujibu wa Chenge, marekebisho
mengine ni idadi ya wabunge wa
Bunge la Jamhuri ya Muungano
ambao wameongezeka kutoka 75
waliopendekezwa na Tume ya Jaji
Warioba hadi kufikia wabunge 360.
Katika Rasimu ya Pili ya Jaji Warioba
ilipendekezwa wabunge 70 wa
kuchaguliwa kupitia majimbo ya
uchaguzi, kati yao 50 kutoka
Tanganyika na 20 kutoka Zanziba,
huku pia ikipendekeza kuwepo kwa
wabunge watano wenye ulemavu
watakaoteuliwa na Rais.
Marekebisho mengine yaliyoingizwa
kwenye Rasimu inayopendekezwa na
BMK ni sifa ya mtu anayestahili
kugombea nafasi za kisiasa kama vile
udiwani, ubunge na urais.
Katika Rasimu ya Jaji Warioba
ilipendekezwa kuwa mtu mwenye sifa
ya kugombea nafasi ya Ubunge ni
lazima awe na elimu ya kidato cha
nne, lakini katika Rasimu
inayopendekezwa na BMK sifa hiyo
imeondolewa na badala yake mtu
anayegombea anapaswa kujua
kusoma na kuandika.
YALIYOFUTWA, KUBORESHWA
MUUNDO WA MUUNGANO
Ibara ya kwanza inayozungumzia
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Bunge Maalum la Katiba limefuta
mapendekezo ya rasimu ya iliyokuwa
Tume ya Mabadiliko ya Katiba kwa
kufuta Muungano wa serikali tatu na
badala yake imependekeza serikali
mbili kama ilivyo kwenye Katiba ya
mwaka 1977.
Katika Ibara 1 (i), Tume ya
Mabadiliko ya Katiba ilieleza kuwa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni
Shirikisho lenye mamlaka kamili
ambayo imetokana na Muungano wa
nchi mbili za Jamhuri ya Tanganyika
na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar
ambazo kabla ya makubaliano ya
Muungano ya mwaka 1964 zilikuwa
nchi huru.
Hata hivyo, Kamati ya Uandishi
imefuta neno 'Shirikisho' kwenye
ibara hiyo kwa maelezo kuwa
wajumbe wengi wamependekeza
Muungano wa serikali mbili.
Mapendekezo ya Kamati hiyo
yanasema kuwa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania ni nchi yenye
mamlaka kamili ambayo imetokana na
Muungano wa nchi mbili za Jamhuri
ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa
Zanzibar ambazo kabla ya Hati ya
Makubaliano ya Muungano ya tarehe
22 Aprili,1964 zilikuwa nchi huru.
Aidha, katika kifungu kidogo cha pili
cha Ibara hiyo, Tume ilipendekeza
kuwa Jamhuri ya Muungano ni
Shirikisho la kidemokrasia linalofuata
mfumo wa vyama vingi vya siasa,
usawa wa binadamu, kujitegemea,
utawala wa sheria na kuheshimu haki
za binadamu; hata hivyo, kamati ya
uandishi imefuta neno 'kujitegemea'
kwa madai kuwa linaleta kasoro ya
mtiririko.
“Kwa msingi huo, Kamati ya Uandishi
imeiandika upya Ibara hii kama
inavyosomeka kwenye Ibara ya 1 ya
Rasimu hii ya Katiba
inayopendekezwa. Neno hilo
(shirikisho), lilifutwa kwa kuwa
mapendekezo yaliyotolewa na
Wajumbe walio wengi ndani ya
Kamati zote kumi na mbili za Bunge
Maalum yalilenga kuwepo kwa
Muundo wa Serikali Mbili," alisema
Chenge.
Kadhalika, Kamati ya Uandishi
imeongeza ibara ndogo mpya ya (3)
kwa kutoa mamlaka kwa Bunge
kutunga sheria itakayoainisha na
kufafanua mipaka ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania.
Kamati hiyo pia imeongeza sikukuu
za taifa kwa kuongeza maadhimisho
ya kitaifa katika Ibara ya tatu ya
rasimu.
“Katika Ibara hii, Kamati sita kati ya
Kamati Kumi na mbili zilipendekeza
kufanya marekebisho kwenye Ibara ya
(3)(1) kwa kuongeza aya mpya ya (d)
kwa ajili ya kuongeza maneno na
maadhimisho ili mbali na Sikukuu za
Taifa zilizoainishwa katika Ibara hii,
kuwapo pia na maadhimisho mengine
ya kitaifa."
Bunge Maalum pia limefuta Ibara ya
tano ya rasimu ya Katiba iliyokuwa
inazungumzia Tunu za Taifa kwa
madai kuwa mambo yaliyotajwa kuwa
Tunu ni msingi wa utawala bora.
Katika Ibara hiyo, Tume ilipendekeza
kuwa Jamhuri ya Muungano itaenzi
Tunu saba ambazo ni (a) utu, (b)
uzalendo (c) uadilifu, (d) umoja, (e)
uwazi, (f) uwajibikaji na (g) lugha ya
Taifa.
Badala yake, Kamati ya Uandishi
imesema: “Kuwa Tunu na misingi ya
utawala bora ni mambo mawili tofauti,
Kamati inapendekeza kuifuta Ibara ya
5 na kuiandika upya.”
Baada ya kufuta, Kamati hiyo
imependekeza Tunu ziwe ni (a) amani
na utulivu, (b) haki na usawa wa
binadamu, (c) usawa wa jinsia na (d)
Lugha ya Kiswahili.
Kamati imeongeza Ibara ya 6
inayoeleza misingi ya utawala bora
ambayo ni (a) uadilifu; (b)
demokrasia; (c) uwajibikaji;(d)
utawala wa sheria; (e) ushirikishwaji
wa wananchi; (f) haki za binadamu;
(g) usawa wa jinsia; (h) umoja wa
kitaifa; (i) uwazi; na (j) uzalendo.
Hata hivyo, Chenge alisema baadhi
ya Ibara za Rasimu za Katiba zimebaki
kama zilivyo kwa kuwa maudhui yake
yanajitosheleza na nyingine
zimefutwa kwa kuwa maudhui yake
yamezingatiwa katika Ibara nyingine.
Sababu nyingine ya kufuta ni kwa
kuwa maudhui yake yamebebwa
katika mapendekezo mengine;
maudhui yake yanapaswa kuzingatiwa
katika sheria za nchi; maudhui ya
Ibara nyingine yamehamishiwa
kwenye Ibara nyingine ili kuweka
pamoja maudhui yanayofanana; na
maudhui mengine yamegawanywa
katika Ibara ndogo tofauti kwa lengo
la kuyaweka wazi zaidi.
MAADILI NA MIIKO YA VIONGOZI WA
UMMA
Katika rasimu ya Tume, Ibara ya 14 (i)
(a), (b) na (c), pamoja na mambo
mengine, ilipendekeza kuwa kiongozi
wa umma atatakiwa kulinda hadhi ya
ofisi yake na kuhakikisha
hatosababisha mgongano wa maslahi
ya umma na binafsi; lakini Kamati ya
uandishi imefuta na kupendekeza
sharti hilo lijumuishwe kwenye
sheria.
Kamati hiyo inapendekeza kufuta na
kuiandika upya Ibara hiyo ili
kubainisha miiko ya msingi katika
uongozi wa umma na kuacha mambo
mengine ya kiutendaji yazingatiwe
katika Sheria itakayotungwa na
Bunge.
“Sababu ya mapendekezo haya ni
kuwa, maudhui ya Ibara hii ya Rasimu
ya Tume, yanaelezea mambo mengi
yakiutendaji na kiutawala ambayo ni
muhimu yakaainishwa katika Sheria
zitakazotungwa na Bunge ili
kurahisisha utekelezaji pindi
kunapotokea mabadiliko."
“Lengo la maboresho ni kuhamishia
masuala haya kwenye sheria za nchi
kutokana na ukweli kwamba
yanabadilika mara kwa mara kutokana
na wakati.”
Bunge Maalum pia limeongeza sura
mbili mpya ambazo hazikuwamo
katika rasimu ya Tume ambazo ni ile
inayohusu Ardhi, Maliasili na
Mazingira na Sura inayohusu Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar, Baraza la
Mapinduzi la Zanzibar na Baraza la
Wawakilishi la Zanzibar.
Aidha, Sura ya Pili ilikuwa na sehemu
moja sasa inapendekezwa kuwa na
sehemu tano na pia Ibara nyingine
mpya zimependekezwa katika Rasimu
ya Katiba inayopendekezwa.
Kamati hiyo imeeleza sababu za
kuridhia kuongeza sura hiyo ni
umuhimu wa ardhi, maliasili na
mazingira katika maendeleo ya nchi
kwa kuwa ni vitu vinavyogusa maisha
ya kila siku ya Watanzania wengi
wakiwamo wafugaji, wakulima,
wavuvi na wachimbaji wa madini.
Alisema lengo ni kuhakikisha raia wa
Tanzania pekee ndiyo wenye haki ya
kumiliki ardhi.
SIFA YA KUGOMBEA UBUNGE
Sifa ya elimu kwa mtu anayegombea
ubunge imependekezwa kuwa awe
anajua kusoma na kuandika Kiswahili
au Kiingereza.Pendekezo hilo linafuta
sharti la awali la kuwa na elimu ya
kidato cha nne, lililopendekezwa na
rasimu ya katiba iliyowasilishwa
katika Bunge Maalumu la Katiba na
aliyekuwa Mwenyekiti wa iliyokuwa
Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji
Joseph Warioba.
Pendekezo la kufuta sharti hilo
lililomo kwenye ibara ya 117 (1) (b)
lilitolewa na Kamati ya Uandishi ya
Bunge hilo kupitia Mwenyekiti wake,
Andrew Chenge, bungeni jana.
Chenge, ambaye ni Mbunge wa
Bariadi Magharibi, alisema pendekezo
hilo limetolewa na kamati yake ili
kutoa fursa kwa watu wenye uwezo
wa kugombea wafanye hivyo, ikiwa ni
pamoja na kuondoa dhana ya uwapo
wa nchi washirika na kulifuta neno
hilo kila linapojitokeza ili kuendana
na mfumo wa serikali mbili
unaopendekezwa kwa sasa.
Pia alisema kamati imeridhia
pendekezo la kuwapo mgombea huru
katika nafasi ya ubunge na kwamba,
pendekezo la kumzuia mtu mwenye
madaraka kugombea nafasi hiyo,
limezingatiwa na kamati kwa kufuta
sharti hilo, ili lizingatiwe katika ibara
nyingine.
Alisema kamati saba za Bunge hilo
zimependekeza aya ya (d) ya ibara
ndogo ya (1) ifutwe na kamati tano
zimependekeza Ibara hiyo ifanyiwe
marekebisho madogo, yakiwamo
kuongeza ibara ndogo ya (1) (g) ili
kutoa fursa kwa Rais kutengua uteuzi
wa mbunge wa kuteuliwa.
Chenge alisema kamati yake baada ya
kupitia mapendekezo hayo,
imeongeza aya mpya ya (h)
inayoweka sharti la mbunge
aliyetokana na mgombea huru
kupoteza sifa za kuwa mbunge
kutokana na kujiunga na chama
chochote cha siasa.
Kuhusu ibara ya 129 inayohusu haki
ya wapiga kura kumwajibisha
mbunge, alisema kamati moja
imependekeza Ibara hiyo ibaki kama
ilivyo kwenye rasimu ya tume, lakini
kamati saba zimependekeza ifutwe na
kamati nne zimependekeza
marekebisho madogo, ikiwamo
kuwapo kwa haki ya wapigakura
kumwajibisha mbunge, ambaye
ameshindwa kuwasilisha au kutetea
kero za wapigakura wake.
Alisema kamati yake baada ya
kutafakari maoni hayo, inapendekeza
ibara hiyo ifutwe kwa kuwa haki
inayopendekezwa inaweza kutumika
vibaya, ikiwamo kumwekea vikwazo
vya kiutendaji mbunge aliyeko
madarakani.
Pia wapigakura wanayo haki ya
kumwajibisha kwa kutompigia kura
mbunge katika kipindi cha miaka
mitano endapo wananchi wataona
mbunge anayewawakilisha hafai,
wanaweza kumwajibisha.
“Kwa kuzingatia mapendekezo hayo
Kamati ya Uandishi inapendekeza
Ibara hii ifutwe,” alisema Chenge.
IBARA YA 132 KUHUSU SPIKA
Chenge alisema kamati yake
imependekeza kuwa ibara hiyo ibaki
kama ilivyo kwenye rasimu ya tume
kwa kuwa maudhui yake
yanajitosheleza.
Hata hivyo, alisema baada ya
kuchambua na kuzingatia
mapendekezo ya kamati za Bunge na
mijadala bungeni, kamati yake
imeifuta na kuiandika upya ibara
ndogo ya (1) ili kumuwezesha Spika
wa Bunge kuchaguliwa kutoka
miongoni mwa wabunge au watu
wenye sifa za kuwa wabunge.
Pia alisema kamati yake imekubaliana
na pendekezo la kufuta neno
“Mbunge” katika ibara ndogo ya (2) ili
kumwondoa mbunge katika orodha ya
watu wanaokosa sifa za kugombea
nafasi ya Spika.
Imeandaliwa na Emmanuel Lengwa,
John Ngunge, Jacqueline Massano na
Editha Majura, Dodoma na Salome
Kitomari, Muhibu Said na Restuta
james (Dar).

SANAA ZA UTAMADUNI WA TANZANIA ZAENDELEA KUBADILIKA

Licha ya kuwapo mawimbi ya
utandawazi yanayoyumbisha sanaa za
ufundi za tamaduni mbalimbali dunia,
Tanzania imeendelea kuwa imara
kwani sanaa zenye utamaduni wake
zimeendelea kukubalika maeneo
mengi duniani.
Ndiyo maana michoro na vinyago vya
marehemu George Lilanga na Edward
Tinga Tinga vinaonyeshwa katika
mataifa mengi duniani.
Hata hivyo kazi za wasanii hao zina
thamani zaidi ng’ambo hasa Ulaya
kuliko nchini.
Profesa wa Sanaa kutoka Uingereza,
Augustus, Casely, alisema hayo juzi
kwenye semina iliyokutanisha
wataaluma wa magwiji wa sanaa
wakiwamo wanahistoria ya sanaa,
wasanii na wapenda kazi za kisanii
iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Semina hiyo ni sehemu ya kuenzi kazi
za msanii nguli hayati George Lilanga,
ambaye Nyumba ya Makumbusho ya
Taifa jijini Dar es Salaam, imeandaa
maonyesho ya kimataifa ya sanaa
zake.
Profesa Casely alisema kazi za
wasanii wa Tanzania zimekubalika
Ulaya ambako watu wana uga na
kumbi za kazi za Lilanga
wanazozitangaza kwenye miji
mbalimbali hasa Uingereza. Hayati
Lilanga kwa mujibu wa Mkurugenzi
Mkuu wa Makumbusho ya Taifa,
Profesa Audax Mabulla, alifanyakazi
nyingi za kisanii katika miaka 1970 na
1980, akichora, kuchonga na
kufinyanga vinyago maarufu vya
‘mashetani.’
“Lilanga alikuwa na kazi za kisanii
zilikuwa zinawafanya watu
wachemshe bongo, wafikirie na
kujifunza ili kuelewa zaidi. Ukiangalia
‘mashetani’ unalazimika kutumia
kichwa kutafsiri na kuujua ujumbe
uliopo,” alisema Profesa Mabulla.
Semina hiyo ambayo ilihudhuriwa na
Profesa gwiji wa historia ya sanaa
Elias Jengo wa Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam, ilijadili mada kadhaa kuhusu
hali ya kazi za sanaa za ufundi za
kileo na zile za kitamaduni.
Akijibu swali la NIPASHE kwanini kazi
hizo ziwe na mapenzi zaidi na
wageni, Mhifadhi Mkuu wa
Makumbusho ya Taifa, Achiles Bufure,
alisema ni matokeo ya kutofuatilia na
kuhamasiha umma, lakini sasa
Makumbusho ina ari mpya ya
kuendeleza sekta hiyo.
Alitaja mikakati ya kuendeleza kazi za
sanaa kuwa ni kuwakusanya wasanii
pamoja na kazi zao ili kuwaendeleza
na kwamba hatua mojawapo
zilizochukuliwa ni kuwaandalia uga
maalumu ndani ya jumba hilo.
Aliwasifu wasanii kwa kuhifadhi
sanaa za asili za kudumisha
utamaduni na pia usanii wa kisasa
kwa ajili ya biashara na kupata
masoko sehemu mbalimbali kama
ilivyo kwa Lilanga

KERO YA UMEME MWISHO 2015

Shirika la Umeme nchini (Tanesco),
limesema hadi kufikia Agosti, mwaka
2015, Tanzania haitakuwa na kero ya
shida ya umeme kutokana na
mabadiliko makubwa yanayofanywa
na shirika hilo ikiwamo kuongeza
mitambo ya uzalishaji umeme.
Aidha, shirika hilo limesema
limejipanga kumaliza tatizo la umeme
kutokana na mradi wa kuzalisha
umeme kwa gesi, makaa ya mawe na
kuimarika upatikanaji maji.
Hayo yalisemwa na Mkurugenzi
Mtendaji wa Tanesco, Felchesmi
Mramba, wakati akikagua miradi ya
ujenzi wa vituo vya Mbagala, Gongo
la Mboto na Kinyerezi 1, jijini Dar es
Salaam inayotarajia kukamilika kati ya
Juni na Agosti, mwaka 2015.
Alisema wakazi wanaozunguka eneo
la Mbagala matumizi yao ya umeme ni
Megawati (MW) 70 na kwamba kituo
hicho kitakapokamilika kitakuwa na
uwezo wa kuzalisha MW 100 kwa
gharama ya Dola milioni 35 za
Marekani.
Kwa mujibu wa Mramba, jijini la Dar
es Salaam pekee linatumia MW 600
kati ya 920 zinazozalishwa kwa sasa
ikifuatiwa na jiji la Arusha, Mwanza,
Tanga na mikoa mingine.
Meneja Mradi Usambazaji Tanesco,
Emmanuel Manirabona, alisema kituo
cha Gongo la Mboto kitakachokuwa
na uwezo wa kutoa MW 50 kinatarajia
kukamilika Desemba mwaka huu.
Akizungumzia kituo uzalishaji umeme
wa gesi Kinyerezi 1, kitakachozalisha
MW 150 alisema miradi hiyo yote
itakapokamilika kero ya umeme nchini
itakwisha.

JUMLA YA Tshs. BIL. 6 YATENGWA KWAAJILI YA MIKOPO YA VIJANA

Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni
na Michezo, imetenga Sh. bilioni 6.0
kwa mwaka wa fedha 2014/2015 ili
kuwasaidia vijana kupata mikopo.
Mikopo hiyo itawawezesha vijana
kujiajiri wenyewe na kutengeneza
ajira kwa vijana wengine.
Mkurugenzi wa Uwezeshaji wa wizara
hiyo, Dk. Kissui Steven Kissui,
aliyasema hayo jijini Dar es Salaam
jana wakati akizungumza na
waandishi wa habari.
Alifafanua kuwa fedha hizo zitatolewa
kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Vijana
kwa lengo la kuwasaidia kupata
mikopo yenye masharti nafuu ili
kuwajengea uwezo kiuchumi kwa
kuanzisha na kuimarisha miradi yao
na kuwawezesha kujitegemea katika
kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja
na hatimaye nchi nzima.
“Kwa mujibu wa Sera ya Taifa ya
Maendeleo ya Vijana ya mwaka 2007,
kijana ni mtu yeyote mwenye umri
kati ya miaka 15 na 35, hivyo vijana
wote walio katika umri huo ni
walengwa wa mfuko huu,” alifafanua
Dk. Kissui.
Aidha, alisema kutokana na
changamoto zilizojitokeza hususani
katika urejeshaji na usimamizi wa
mikopo inayotolewa, serikali iliamua
kubadili utaratibu wa utoaji mikopo
hiyo na kuunda utaratibu mpya
ambao ulianza kutumika Aprili, 2013.
Alisema mikopo ya mfuko huo
hutolewa kupitia miradi ya vijana
iliyoidhinishwa kwa pamoja kati ya
wizara, mikoa, halmashauri na
hatimaye fedha hizo kupitishwa
saccos za vijana.
“Mwaka 2013/2014, mikopo yenye
thamani ya Shilingi 415,919,000
ilikopeshwa kwa vikundi vya vijana 67
kutoka katika halmashauri 25 za
Tanzania bara na wizara bado
inaendelea kupokea na kuchambua
maandiko ya miradi kutoka katika
halmashauri mbalimbali,” aliongeza.
Aidha, alisema wizara inaendelea
kuwahamasisha vijana kujiunga
katika vikundi vya ujasiriamali ikiwa
ni pamoja na kusajili vikundi hivyo na
hatimaye kujiunga na saccos za
vijana zilizoanzishwa.
Dk. Kissui alisema pia fedha za Mfuko
wa Maendeleo ya Vijana ni kwa ajili
ya vijana wote nchini, hivyo kila
kijana anayo haki ya kunufaika na
mkopo kutoka katika mfuko huo ikiwa
ni pamoja na kukopa na kurejesha.
Hata hivyo, aliwaomba wananchi
kutohusisha fedha hizo na masuala
ya kisiasa wakidhani kuwa ni zawadi.

Monday, September 22, 2014

TAKWIMU ZA MAUAJI YA ALBINO ZI

Shirikisho la Vyama vya Watu wenye
Ulemavu Tanzania (Shivyawata),
limeitaka serikali kupitisha adhabu
ya kunyongwa kwa wale wanaohusika
na mauaji ya Albino.
Akizungumza katika maadhimisho ya
Siku ya Amani Kimataifa ya Albino
jana jijini Dar es Salaam, Rais wa
Chama cha Albino Tanzania (Tas),
Joseph Tona, alisema kauli hiyo
imetokana na ongezeko la idadi ya
mauaji dhidi yao.
Kadhalika, takwimu za kutoka mwaka
2006 zinaonyesha kuwa Albino 74
wameshauawa kikatili, huku 56
wakinusurika kifo, na kati yao 11
wameongezewa ulemavu mwingine
wa kudumu.
“Tunaadhimisha siku ya amani
Tanzania, lakini hatuna amani kabisa,
wenzenu tunakatwa viungo na
kuuawa kama kuku bila huruma,
kingine cha ajabu makaburi 18 ya
albino wenzetu yamefukuliwa na miili
yao imetolewa, picha hii inaashiria
nini?” alihoji Tona.
Alisema hofu hiyo imesababisha
maziko yao kutokuwa na heshima
kama wengine kutokana na baadhi ya
familia kuwazika wapendwa wao kwa
siri na wengine ndani ya nyumba, au
kuweka zege nzito katika makaburi
kuzuia ufukuaji wa miili yao.
Alisema licha ya serikali kuweka
vikosi kazi katika kudhibiti mauaji
hayo, bado haisaidii kitu kutokana na
baadhi ya polisi na maofisa kuwa
miongoni mwa vinara wa kupokea
rushwa.
Kwa mujibu wa Tona, matukio zaidi
ya 120 ni kesi za mauji ya albino, kati
yake 11 ndiyo yaliyofikishwa
Mahakama, ambapo kati ya hizo kesi
tano tu zimeweza kutolewa hukumu
hadi sasa.
Akitoa ushuhuda mmoja kati ya
waathirika ambaye mikono yake
miwili imekatwa, Mariam Stanford,
mkazi wa Ngara, mkoani Kagera,
aliwataka wauaji wa albino
wanyongwe hadharani ili iwe
fundisho kwa wengine wenye tabia
kama hizo.
“Japokuwa Tanzania inasifika ndani
na nje kama kisiwa cha amani, tafsiri
hiyo ni kinyume kwani ni miongoni
mwa nchi zinazoongoza kwa mauaji
ya kikatili, hivyo mwito wangu kwa
viongozi wa dini tumieni midomo
yenu kupinga hali hii kwa sababu na
sisi tumeumbwa na Mungu na
tunastahili kuisha kama wengine,”
alisema Miriam.
Mkurugenzi wa Shirika la Under The
Same Sun, Vicky Ntetema, aliishauri
serikali kupitia vikosi kazi
vilivyochukua jukumu la kuchunguza
mauaji na ukatwaji wa viungo kwa
albino, kutangaza matokeo kwa umma
ili wahusika wachukuliwe hatua za
kisheria.
Pia, iuelezee umma matokeo ya kura
za siri zilizopigwa katika mikoa
tangu mwaka 2009 hadi sasa
zibainishwe wazi kwani nyingi
zimeonyesha waganga wa jadi
kutumiwa na na viongozi wa kubwa
katika kuwania nyadhfa mbalimbali
serikalini.
Kutokana na hofu hiyo, ameitaka
serikali kurejea mkakati wa mwaka
2009 uliotolewa na Waziri Mkuu
Mizengo Pinda, ili kupiga marufuku
leseni za waganga wa kienyeji na
wale wa jadi.
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii,
Dk. Seif Rashid, alizitaka taasisi
zilizopewa jukumu la kusimamia
vitendo hivyo vya kikatili dhidi ya
walemavu hususani albino kutekeleza
majukumu waliyopewa kisheria kwa
uadilifu mkubwa jamii ya Watanzania
ione haki inatendeka ili kudumisha
amani ya nchi.

  BOFYA HAPA KUUNGANA NASI INSTAGRAM

Tuesday, September 16, 2014

WANAFUNZI JIJINI DAR WADAI KUA WANATONGOZWA NA WALIMU WAO

Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya
Mwanalugalo, jijini Dar es Salaam,
wamelalamikia uongozi wa shule
kutowaonya baadhi ya walimu wa
kiume wenye tabia ya kuwataka
kimapenzi wanafunzi wa kike.
Wanafunzi hao walitoa malalamiko
hayo wakati wakizungumza na
NIPASHE katika wiki ya ukaguzi wa
shule nchini jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wanafunzi waliozungumza
kwa masharti ya kutotajwa majina
walisema baadhi ya walimu katika
shule hiyo wamekuwa wakiwataka
kimapenzi wasicha kwa kuwapa ahadi
nyingi ikiwamo kuwalipia usafiri wa
pikipiki kila siku na kuhakikisha
wanafaulu masomo
wanayowafundisha.
“Walimu hapa wanakutonga na
kukuahidi kufaulu, ukiwa mjinga
unakubali, lakini wengi tumewazoea
kazi yao nikutongoza kila mtu,”
alisema mwanafunzi mmoja.
“Ikitokea umekataa kutembea na
mwalimu ujue kama anakufundisha
somo lake darasani atakuchapa
mpaka ukome, lakini inabidi tuvumilie
tu,” alisema mwanafunzi mwingine.
Katika ukaguzi huo uliofanywa na
Mkurugenzi na Mkaguzi Mkuu wa
Shule za Sekondari, Marrystala
Wasena, alisema kitendo hicho ni cha
kinyama na kuahidi kuhakikisha
anawashughulikia walimu wote
watakaohusika kufanya vitendo hivyo.
“Hatuwezi kulivumilia tabia hii
iendelee, ni bora shule ibaki na
walimu wa chache kuliko kuwa na
walimu waiana hii,” alisema.
Akizungumzia tuhuma hizo, mkuu wa
shule hiyo, Aron Ndunguru, alisema
tuhuma hizo hazina ukweli wowote.
“Wanafunzi ni waongo wenyewe
ndiyo wanawatongoza walimu wao ili
watembee nao halafu wanasema wao
ndiyo wanatongozwa,” alisema
Ndunguru.

MAKUNDI MATANO YA DANCE 100% YATINGA NUSU FAINALI

Safari ya shindano la Dance 100% imefikia patamu baada ya juzi makundi matano kati ya makundi kumi yaliyochuana vikali katika nusu fainali kwenye uwanja wa Don Bosco Oysterbay jijini Dar es Salaam kutinga fainali.

Shindano hilo linaloandaliwa na kituo cha televisheni cha East Africa (EATV) na kudhaminiwa na Vodacom Tanzania limeleta mapinduzi makubwa katika tasnia ya kudansi nchini na kuwavutia vijana wengi kushiriki.

Makundi ya wachezaji wa miondoko mbalimbali ya muziki yaliyoingia fainali ni Wazawa Crew, Best Boys Crew, The W.T, Wakali Sisi na The Winners Crew.

Mratibu wa mashindano hayo, Happy Shame, alisema kuwa katika kinyang’anyiro cha nusu fainali hiyo wamepata makundi matano yaliyoingia fainali itayofanyika baadaye.

“Huu ni mwaka wa tatu EATV tunaandaa mashindano haya chini ya udhamini wa Vodacom Tanzania. Mwaka huu mashindano haya yamekuwa na umaarufu mkubwa na ushindani wa hali ya juu na kuwavutia vijana wengi ambao hujitokeza kushiriki,”alisema Shame.

Shame aliongeza kuwa kundi litakaloibuka na ushindi katika mashindano haya ambayo pia yamekuwa yakioneshwa na kituo cha EATV kila Jumatano saa moja kamili usiku, litajishindia kitita cha Sh. milioni 5.

Naye Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania ambao ni wadhamini wakuu wa shindano hilo, Matina Nkurlu aliwapongeza vijana wote walioshiriki katika shindano hilo na kuwapa moyo wale ambao hawakufanikiwa kuingia fainali kuwa wasife moyo kwani asiyekubali kushindwa si mshindani bali wajipange upya na wawe wabunifu zaidi na kuweza kushiriki tena mwakani.

DR. REGNALD MENGI AINGIA KWENYE TUZO ZA MFANYA BIASHARA BORA AFRIKA MASHARIKI

Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Dk.
Reginald Mengi, ni miongoni mwa
wafanyabiashara wanne waliofikia
fainali ya kuwania Tuzo ya Mwaka ya
Mfanyabiashara Bora Afrika (AABLA)
kundi la Afrika Mashariki.
Sherehe za tuzo za AABLA, kundi la
Afrika Mashariki zitafanyika Septemba
20, mjini Nairobi na zitarushwa
hewani na runinga barani Afrika.
Kwa mujibu wa chaneli ya televisheni
ya masuala ya fedha na biashara
Afrika (CNBC Africa), ambao ndiyo
waandaaji wa sherehe hizo, tuzo hizo
za kila mwaka zimebuniwa kwa ajili
ya kutambua utendaji uliotukuka
katika biashara, wenye mafanikio
makubwa kwenye sekta zao za
biashara na vilevile kwenye jamii
ambapo biashara hizo zinaendeshwa.
“Tuzo hizo ni kutambua uongozi wa
watu hao katika kubadilisha sekta ya
biashara kwa kuendeleza ubora wa
shughuli zao kwa kuzingatia desturi
njema za kufanyabiashara na
ubunifu.”
“CNBC Africa inajivunia kuendeleza
utamaduni uliowekwa na tuzo hizi
unaotambua na kusherehekea
mtazamo, msukumo wa mafanikio na
ubora mkubwa wa viongozi
wafanyabiashara katika bara la Afrika.
AABLA iinawatambua kipekee na
kuwaheshimu viongozi ambao
wamechangia katika kuboresha
uchumi wa Afrika na waelekezi wa
biashara zinazoongoza wakati wa
sasa.
Washindi wa tuzo hizi ni mfano mzuri
zaidi katika uongozi Afrika. Wao ni
uthibitisho wa thamani halisi wa
kiongozi aliyefanikiwa, - mafanikio,
nguvu, ubunifu, ustadi, ujuzi na
uwezo wa kuona mbali thamani
ambazo ni muhimu katika kuunda
biashara kubwa katika uchumi wa
Afrika na ulimwengu.
AABLA ni tuzo moja kubwa zaidi ya
biashara barani Afrika na hutolewa
katika kanda za Afrika Magharibi,
Afrika Mashariki na Kusini mwa
Afrika.
Wafanyabiashara wengine watatu
wateule wa tuzo hiyo ni Ofisa
Mtendaji wa BRITAM, Benson Wairegi,
(Kenya), Ofisa Mtendaji wa CENTUM,
James Mworia, (Kenya) na Ofisa
Mtendaji wa CROWN PAINTS, Rakesh
Rao (Kenya).
Watanzania wengine walioteuliwa
katika tuzo hizo kwa makundi tofauti
ni Ofisa Mtendaji wa Helvetic Solar
Ltd, Patrick Ngowi, (EA Young
Business Leader) na Ofisa Mtendaji
wa Techno Brain Ltd, Manoj Shanker,
(Entrepreneur of the Year).