Tuesday, April 29, 2014

WATOTO WALIOKUFA KATIKA SWIMMING POOL...WAKIWA KATIKA KUFURAHIA SIKUKUU YA MWENZAO

April 27  kulitokea vifo vya watoto 3 ambao walikua na
birthday party nyumbani lakini baada ya kukamilika kwa
taratibu za party ya nyumbani waliamua kuimalizia party
hiyo hotel ya Landmark,walipofika walienda kuogelea
kwenye swimming pool ya watoto lakini baadae watoto hao
walitoka kwenye pool ile ya watoto wakaingia kwenye pool
ya wakubwa na kwa bahati mbaya waliingia sehemu yenye
kina kirefu.
Watoto wenzao walipoona wenzao wanazama walianza
kuwavuta kuwatoa nje lakini hali zao tayari zilikua
mbaya,mmoja wapo hali yake ilikua kidogo afadhari lakini
kwa bahati mbaya nayeye alifia hospital wakati akipatiwa
matibabu katika hospitali ya Masana na kufanya Idadi ya
watoto waliofariki kuwa 3 majina yao ni Janet Zacharia,Eva
na Ndimbuni.
Kamanda Kova amesema>>’Kusema kweli sio mara ya
kwanza kutokea,mara nyingi vifo vya watoto vinatokana na
uangalifu au uzembe kutoka kwa wale wanaotakiwa
kuwaangalia hao watoto wao,hizi hotel zote zenye
swimming pool lile eneo la kuogelewa basi wasiruhusiwe
watoto wadogo kuogelea au kuwe na mtu ambaye anajua
kuogelea au kuokoa ambaye yupo pale’
‘Unajua watoto wana tabia ya kuigana mmoja akiingia
akiogelea pengine anafahamu kidogo wengine wote
wanafata mkumbo wanaona wanaweza,sisi kama jeshi la
Polisi tumeamua hili kosa la uzembe kusababaisha kifo
kisheria mtu anaweza kushtakiwa kwa kuzembea kwa
kutochukua tahadhari mpaka watoto kama wale ambao
hawana hatia uwezo wao mdogo wa kufikiri au kuijiokoa’
‘Tunafatilia kwa umakini lakini jukumu la kufatilia maisha
ya watoto ni la wazazi mia kwa mia wasipofanya hivi
wakiwa hawapo makini matokeo yake ni haya watoto 3
wamefariki,tunaendelea na uchunguzi na baadae tutatoa
taarifa kamili’.


Posted via Blogaway

Tuesday, April 22, 2014

AL-SHABAAB WATOA TISHIA LA KUFA MTU DHIDI YA KENYA

Tishio la kigaidi lina kodolea macho taifa la Kenya baada
ya kundi la kigaidi lililo na makao yake makuu nchini
Somalia kuachia video nyingine kwenye mtandao wa Al-
Kataib wakitishia kutekeleza mashambulizi nchini Kenya
wakati wowote.
kwenye kanda hiyo msemaji wa alshabaab aliye jifunika
uso anasema kwamba hawaoni lolote litakalo wa zuia
kuingia Kenya hasa baada ya kufanikiwa kutekeleza mauaji
katika jengo la west Gate. mwaka uliopita>>’tumekuwa
tukisema tutafika Kenya lakini hivi tayari tushafika si eti
westgate ndio tosha bado kuna mamia na mamia ya watu
wanaongojewa mahala kama hiyo insha Allah’alisema
msemaji huyo.
Huku wakiimbia tutawalipua hadi tuwamalize wanamgambo
hao wamesema kwamba wameamua kuungana na
wasomali kutetea dini ya Allah,Wadadisi wa maswala ya
kiusalama wanahoji kwamba huenda hawa ni baadhi ya
vijana kutoka kwa mataifa ya Afrika mashariki walipewa
mafunzo ya itikadi kali na baadaye kupelekwa somalia
kujiunga na Alshabaab kutokana na wanavyozungumza
lugha ya Kiswahili kwa ufasaha kwenye video hiyo.
Ispekta mkuu wa polisi nchini Kenya bwana David kimaiyo
amesema uchunguzi umeanzishwa kubaini chanzo cha
video hiyo na taarifa kamili kutolewa punde tu watakapo
pata habari zaidi kuhusiana na video hiyo.

EE MUNGU TUJALIE AMANI WAJA WAKO


Posted via Blogaway

BAADA YA TUZO...WEMA APATA COMMENT NEGATIVE...nae ajibu kwa mkwara instagram..

Hata masaa 24 hayajapita tangu akabidhiwe tuzo yake ya
sexiest girl tayari inaonekana ameshakutana na negative
comments baada ya kushinda hiyo tuzo.
Kwenye mashindano hayo alikuwa na warembo wenzake
Jokate,Lulu,Nelly Kamwelu,Jackline Wolper hatimaye
alifanikiwa kushinda tuzo hiyo.
Wema ametumia ukurasa wake wa instagram kutoa yaliyo
moyoni mwake na ameandika,
“If u got it flaunt it….. Ndo nshashinda…. kama hujapenda
kasage chupa kunywa…. maana naona sasa its too much
khaaaaaaaa.!
Ebu mnitue mie mtoto wa watu… And again much love to
y’all dat support me… nawapenda sana…. nimemaliza….
Award yangu ndo hiiiiiiiiooooooooo…… next year tusubiri
mwingine.
Nalala zangu…. tukutane kesho…. najua wengi mnanipenda
ni wachache wenye vijiba vyao vya roho…. Wema atabaki
kuwa Wema tu… Bhaaaaas.”

WEMA hatak mchezo kwakwel


Posted via Blogaway

Sunday, April 20, 2014

STORY...

Story: BATA MREFU 3
Writter: ALNORD SPORTIEVE
Contact: 0655415200

ILIPOISHIA SEHEM YA 2

Walipita chalinze,morogoro,kibaha hatimaye wakaingia UBUNGO
BUS TERMINAL ambapo ALNORD ndio alichanganyikiwa kabisa
kwani aliyaona majengo makubwa(maghorofa) ambayo alikua
akiyaona kwenye TV tu kule kijijini kwao kwenye mabanda ya
video...
Alihamaki sana had ilibak kidogo agongwe na gari pind
walivokua wanavuka barabara ndipo CHUMA akaona ni bora
achukue tax maana hali ile ilionyesha wazi kabisa kua angeweza
kupata aibu mjini pale...ndani ya lisaa limoja na nusu walifika
nyumban kwa baba ake mkubwa(MR. ABDALLAH
CHUMA)...ambapo alipokelewa kwa furaha sana...na wakampa
mizigo HOUSE GIRL wa pale nyumban...nae akaketi seblen
akisubiri nin kinafuata

ENDELEA
...Alnord alikua akiangaza macho huku na kule ndan ya nyumba ile ambayo kiukwel ilikua ni ya kifahari...hakuweza kufikiria kua atakuja kuiona nyumba nzuri kama ile...sio siri alizubaa kiac kwamba hata kaka yake alivokuja kumuita pale seblen ili akamuoneshe chumba atakachokua analala hakuweza kumsikia had alivompiga begani ndipo akashtuka...

"Dogo mbona umezubaa hivo ndugu yangu? Twende nkakuonyeshe chumba chako kule" alisema CHUMA baada ya kumshtua ALNORD ambae mawazo yake yalimpeleza had akahisi yupo kule kwa obama anaishi maisha ya kizungu baada ya kuona furniture nzuri sana na zilizoonekana ni za gharama...

"Ha..ha..hapana kaka nilikua nakumbuka safari yetu ilivokua ndefu...ila sio siri nyumba yenu ni nzuri sana...yani mi nilidhan na huku nyumba zote ni za udongo kama kijijin kwetu".    Alizuga vile ALNORD huku akiinuka na kumfuata kaka ake ambae alikua ametangulia mbele kidogo...mpaka walipofika kwenye chumba kimoja ambacho kilikua ni self contained...yan choo na bafu ndani,TV na makolobwezo kibao...kilikua ni kizuri sana kwan pia kilikua na sofa set moja ya kawaida..

"Yeleuwiiiiii....hasa kaka umenleta chumban kwa baba mkumbwa kufanya nin?" Aliuliza kijana yule ambae alikua ni mshamba kupita kiasi..

"Aaaaah dogo acha masihara...hik ndio chumba chako,halafu mlango ule pale ni choo,na bafu ipo mulemule...vyote unavyoviona katika chumba hiki kua huru kukitumia na usisite kuniambia ukiwa na tatizo lolote..sawa dogo? Sasa nenda ukaoge halafu uje sebleni tule" aliongea CHUMA huku akiwa amemaliza kumuonyesha kila kitu kilichopo chumbani kule na yeye kuondoka akimuacha ALNORD mule ndan...

ALNORD hakujibu chochote zaid ya kujitupa kwenye gule gukitanda gwenye vipimo vya sita kwa sita...akiwa haamin kua atakua analala kwenye godoro tofaut na kule kijijin kwao ambako alikua analala kwenye mkeka...

Alivua nguo zake kisha akaenda bafuni kule ambako alikuta taulo jeupeeeee,sabuni ya dettol active,sink Kubwaaa ambalo kwa yeye alihisi wenda litakua bwawa lililokauka maji,na kwa pemben juu aliona bomba la mvua na koki chin yake...ambayo haikumpa tabu kujua pale panafungua maji kwan hata kijijin kwao kulikua na bomba moja la kijiji..hivo alifungua na kushangaa maji yanatoka kwa juu alimanusura akimbie ila alijikaza na kuanza kujipaka sabuni ile ambayo harufu yake ilimvutia mnooo...kisha akajisafisha mapovu na kujipukuta na taulo akatoka zake...

Hakujua apake yapi na aache yapi maana alikutana na mafuta ya aina nyingi kwenye dressing table ya chumban kwake...akaamua kuchukua kopo moja lililoandika VASELINE MEN na akajipaka,akabadili nguo zake na kuvaa nguo alizozikuta kitandan kwake na kujua kua kaka yake ndie aliemletea..kiukwel nguo zilipendeza sana mwilin mwa ALNORD hasa ukuzingatia alikua na sura nzuri,pia t-shirt ilimbana na kuonesha kifua chake kilichojaa vizur...

Basi akatoka zake na kuelekea seblen...kwa bahat mbaya kutokana na wingi wa milango ya vyumba na ugeni wake akajikuta badala ya kuingia mlango wa seblen aliingia kwenye chumba cha HOUSE GIRL ambae alikua mtupu kama alivozaliwa kwan alikua ametoka kuoga...
*******

Baba yake alimuandalia kila kilicho cha muhimu katika safari yake ambako alikua anaenda kukaa peke yake(kujitegemea)...aliviandaa kwa siri kwani aliogopa kama mke wake angeviona ingekua balaa jingine kwani alikua hampendi MARRY..

MARRY alienda kwaakina ESTER ili kumjulisha juu ya safari yake..alipofika kule alimkuta ESTER na baba ake wanajadili kuhusu ESTER kwenda DAR kufungua SALOON YA KIKE...baba ake alitaka mwanae akakae kwa baba yake mdogo ambae anaishi MBAGALA jijini DAR...lakin baada ya MARIA kuwaeleza kua nae anaenda kukaa huko dar kwenye nyumba ya marehemu mama ake ndipo wakaona ni bora wakakae wote huko kwani walikua ni marafiki toka utotoni mpaka sasa wote wamefeli kidato cha nne..

Walikubaliana na maandalizi yalipokamilika wakasafirishwa wao na vitu vyao hadi DAR ambapo walifika salama....kwakua nyumba ile hakuishi mtu kwa mda mrefu hivyo walianza kufanya usafi huku vyombo vyao vikiwa nje na walomaliza wakaingiza ndani na kuvipanga katika mpangilio mzuri ambao unadhihirisha kua usafi na ustaarabu unachukua nafasi yake kwa wasichana wale ambao kiuhalisia walikua wazuri tena sio ule uzuri wa make up..ulikua ni uzuri wa asili kwani MARRY alikua ni mweusi kiasi yan ule weusi wa kung'aa,umbo lake zuri na macho madogo ya kijivu na ESTER alikua na ngoz ya maji ya kunde,umbo modo lakin lile lenye mvuto..

Wakiwa wanamalizia kutandika kitanda na sofa mlango uligongwa kistaarabu kidogo....

#ITAENDELEA panapo majaaliwa


Posted via Blogaway

WAUMINI NCHINI KENYA KUSAFISHA BARABARA KWA SABUNI...

Kupitia vyanzo vyetu nchini Kenya riporter wetu anaripoti
kwamba wakazi wa jiji la Eldoret wamemfanya kila alieiona
hii kuvutiwa na pengine kujua imekuaje wakafanya hivi kwa
mara ya kwanza baada ya kujitosa na kupiga deki barabara
ya lami ya Oginga Odinga jijini Eldoret kaunti ya Uasin
Gishu nchini Kenya.
Unaambiwa wameamua kufanya hivi ikiwa ni maandalizi ya
kumlaki nabii Daktari Awuor kwa ajili ya maombi ya leo na
siku ya Jumatatu kuadhimisha pasaka na kumshukuru
jehova kwa kuwasaidia jiji la Eldoret kufanyika uchaguzi wa
amani mwaka 2013
Hata hivyo kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii maoni
yalikotolewa na Wakenya kuhusu hii ishu, maoni mengi
yameonekana kupinga kitendo cha waumini hao wa kanisa
la Jesus is lord kwa kumpa Daktari Awuor heshima kupita
kiasi.
Mkurugenzi mkuu wa Kass media inayo miliki Radio ya
kass fm inayotangaza kwa lugha ya kikalenjin
inayozungumzwa na wakazi wa jiji la Eldoret Julius lamaon,
amesema ‘watu wetu waache kupotoka, jiji letu
limebadilishwa na kuwa jiji la vituko…… Gavana hatakiwi
kuhudhuria mkutano huu’


Posted via Blogaway

STORY: BATA MREFU-SEHEMU YA PILI

Story: BATA MREFU
Writter: ALNORD SPORTIEVE
ILIPOISHIA SEHEMU YA 1
Basi ALNORD alimaliza kujiandaa akiwa kavalia nguo zake
alizonunuliwa katika kusherehekea kuvuka mwaka mpya ali
maarufu kama NEW YEAR na kwenda nje ambapo alikua
akisubiriwa na kaka yake huyo...
Alifika pale na kupewa baraka na wazazi wake huku wakimsihi
kua mwaminifu katika biashara ya baba yake mkubwa na pia
kuwa mnyenyekevu na mtiifu pindi awapo nyumbani kwa baba
yake mkubwa....mama ake alimsisitizia sana kuhusu swala la
kujifanya mjinga kwa kila atakachoambiwa na pia kuepuka
kujiingiza katika mapenzi kwani walikua wakisikia kua dar es
salaam kulikua na vishawishi vingi ambavyo vingepelekea
kupata maambukizo ya UKIMWI...walimsihi sana maana
hawakupenda mwanao wa pekee ambao walimpenda kupita
maelezo kwani ndiye waliebarikiwa na MUNGU...
Alnord aliahidi kuyazingatia hayo kisha wakaagana na huku
wazazi wake wakimpa mikono ya kheri kuashiria kua wanamtakia
safari njema..
ENDELEA
Safari ilianza ambapo walienda kwenye stand ndogo ya pale
MFUMBI ili kuvizia mabasi yatokayo MBEYA maana pale hapakua
na stand kubwa kusema kwamba wangekata ticket ofisin..hasa
ukizingatia kile ni kijiji kidogo sana...
Walisubiri sana pale,baada ya kusimamisha mengi yao bila
mafanikio hatimae mnamo saa mbili kamili walifanikiwa
kupanda bus(ABOOD) ndipo safari ikaanza rasmi..walikata ticket
dakika chache baada ya kuingia ndani ya bus hilo...safari yao
haikua nzuri kiasi kwa upande wa ALNORD maana dereva alikua
akiendesha kwa mwendo kasi kidogo kitu kilichomfanya
ALNORD awe mwoga kwani hakuwahi kupanda mabasi makubwa
zaidi ya daladala na coaster ambapo ilikua nadra pia..aliweza
kupanda magari hayo madogo ya abiria iwapo yeye,mama yake
na baba yake wanaenda LEMBUKA(MNADANI) kununua mahitaji
hasa kipindi ambacho sikukuu zinakaribia,kama tunavyojua
watu wengi hupenda kuvaa nguo mpya kila sikukuu kama
mwanafunzi apendavyo uniform mpya ikiwa ni pamoja na
mahitaji yake yote ya shule pindi shule zinapofungua....
*************
""Marry mwanangu,najua ni kipindi kigum kwako..ila usikate
tamaa mwanangu kwani ni moja ya matokeo...chukulia kama
changamoto na inakubid ukabiliane nayo na sio kumwaga
michoz kwan hata ukijaza jaba huwez kubadilisha
matokeo...kufeli shulen sio kufeli maisha...""
Ilikua ni baba ake MARIA C. NGWILLA akimpa moyo mwanae
baada ya matokeo ya kidato cha nne kutoka na kuonesha kua
mwanae MARIA amepata div. 4 ya alama 38 kitu ambacho
kilimfanya mwanae awe mtu wa kulia tu...ndipo akaamua
kumuita na kumpa moyo...
""Lakin baba we mwenyewe unajua jinc gan nilikua nna uwezo
darasan halafu mwishon matokeo yanatoka kama haya kwel
unadhan mi najickiaje?? Hasa ukizingatia huyu mke uliemuoa
baada ya mama kufa anavoninyanyasa hapa nyumban...ntakuaje
na furaha...yan kila cku ananiambia mimi nishinde apo grocery
niuze halafu mwisho wa siku anasema mi namuibia!!! Mi baba
nimechoka bora niende kukaa kwaakina ESTER tu..""
MARRY alimjibu baba ake maneno mfululizo yenye ukweli ndani
yake kwa sauti ya huzuni iliyoambatana na kilio cha kwiwi
ambayo yalionyesha taswira ya maisha ya tabu alioishi MARRY
pale nyumban kwao baada ya MAMA yake mzazi kufa na baba
yake kuoa mke mwingine ambae kiukweli alikua akimnyanyasa
mtoto huyu amba alitoka kuhitimu kidato cha nne katika shule
ya sekondari EDUCARE ndipo akarudi kwao ambako akakutana
na maisha yale ya shuruba...huku akisisitiza kwenda kukaa kwa
rafiki yake ambae walisoma nae shuleni huko na kua marafiki
wakubwa kiasi kwamba alikua na uwezo wa kwenda kukaa huko
bila kipingamizi kutoka kwa wazazi wa ESTER...
Baba yake alihuzunika sana hadi akafikia hatua ya kutoa machozi
kutokana na maneno yaliomuumiza haswa...ndipo akaona ni
bora amhamishe mwanae na kumpeleka DAR ES SALAAM
ambako kuna nyumba alioacha mkewe ili akaisimamie huku
yeye akikaa nyumba ya ndani na pesa ya wapangaji aitumie
kufanyia kitu kitakachomjengea maisha mazuri...
Walikubaliana na mwanae huyo wa mwisho kati ya wanne
ambao ni wakike wawili na wa kiume wawili... mipango ya safari
ilianza...
******
...safari iliendelea huku CHUMA akimuonesha mdogo wake
huyo mshamba kila kituo walichopita ikiwemo
MAKAMBAKO,IRINGA,RUAHA MBUYUNI hadi waliposimama
katika hotel ya ALJAZEERA ili kupata chakula cha mchana...
Walishuka na kwenda kununua chakula huku ALNORD
akishangaa sana mazingira ya hotel ile ikiwa ni pamoja na
vyakula vizuri...
Walirud kwenye gari had mda wa kuendelea na safari ulipofika
na dereva akakanyaga gear.. #vuuuuuuum wakaianza mikumi
ambapo ALNORD alidhihirisha wazi kua yeye ni mshamba
maana alishangaa huku akipiga kelele kwa saut kumuuliza kaka
ake sehemu ile ni nin had alipoambiwa kua ni HIFADHI YA
MBUGA YA WANYAMA hapo angalau alitulia...
Walipita chalinze,morogoro,kibaha hatimaye wakaingia UBUNGO
BUS TERMINAL ambapo ALNORD ndio alichanganyikiwa kabisa
kwani aliyaona majengo makubwa(maghorofa) ambayo alikua
akiyaona kwenye TV tu kule kijijini kwao kwenye mabanda ya
video...
Alihamaki sana had ilibak kidogo agongwe na gari pind
walivokua wanavuka barabara ndipo CHUMA akaona ni bora
achukue tax maana hali ile ilionyesha wazi kabisa kua angeweza
kupata aibu mjini pale...ndani ya lisaa limoja na nusu walifika
nyumban kwa baba ake mkubwa(MR. ABDALLAH
CHUMA)...ambapo alipokelewa kwa furaha sana...na wakampa
mizigo HOUSE GIRL wa pale nyumban...nae akaketi seblen
akisubiri nin kinafuata
#ITAENDELEA panapo majaaliwa


Posted via Blogaway

Saturday, April 19, 2014

STORY MPYA...

Story:BATA MREFU
writter: ALNORD SPORTIEVE

""We ALNORD....anodiiii,,,,,,we mtoto wa mzee mgumba.....hunisikii au ndo kiburi???"

Ilikua ni sauti ya ukali kidogo na utani ndani yake aliokua akiitoa Se Mlowe ambae ni mke wa mzee SPORTIEVE ANYELWISE MGUMBA na mama wa mtoto mmoja(alnord) ambao walikua wakiishi katika kijiji cha MFUMBI kilichopo CHIMALA-MBEYA...aliekua akimuita mwanae mpendwa aliekua amekuja kuchukuliwa na KAKA ake (RAJAB ABDALLAH CHUMA)ambae ni mtoto wa baba ake mkubwa(ABDALLAH  CHUMA) alieshiriki mama mmoja ila baba tofauti na baba ake mzee SPORTIEVE MGUMBA.... ili aende nae mjini DAR-ES-SALAAM kumsaidia kusimamia botique(duka la nguo) ambalo ni la baba ake..

Ilibidi aitwe Alnord kwenda huko baada ya wafanyakazi wengi waliowaajili kutokua waaminifu kwani walikua wakiiba pesa ikiwa ni pamoja na nguo na kukimbia....hivo wakaona kumleta ndugu yao huyo inaweza ikaleta ahueni...maana RAJAB aliezoeleka kwa jina la CHUMA ambao ndio ubini wake alikua bize na masomo na mara nyingi kwenda kwenda kufunga mzigo ambao mara nyingi huenda kufungia CHINA..

Basi ALNORD alimaliza kujiandaa akiwa kavalia nguo zake alizonunuliwa katika kusherehekea kuvuka mwaka mpya ali maarufu kama NEW YEAR na kwenda nje ambapo alikua akisubiriwa na kaka yake huyo...

Alifika pale na kupewa baraka na wazazi wake huku wakimsihi kua mwaminifu katika biashara ya baba yake mkubwa na pia kuwa mnyenyekevu na mtiifu pindi awapo nyumbani kwa baba yake mkubwa....mama ake alimsisitizia sana kuhusu swala la kujifanya mjinga kwa kila atakachoambiwa na pia kuepuka kujiingiza katika mapenzi kwani walikua wakisikia kua dar es salaam kulikua na vishawishi vingi ambavyo vingepelekea kupata maambukizo ya UKIMWI...walimsihi sana maana hawakupenda mwanao wa pekee ambao walimpenda kupita maelezo kwani ndiye waliebarikiwa na MUNGU...

Alnord aliahidi kuyazingatia hayo kisha wakaagana na huku wazazi wake wakimpa mikono ya kheri kuashiria kua wanamtakia safari njema..

#ITAENDELEA panapo majaaliwa
Support yako ni muhimu sana


Posted via Blogaway

Thursday, April 17, 2014

IFUATAYO NI TAARIFA FUPI YA MPIGA GUITAR WA SKYLIGHT BAND ambae kwa sasa amefariki dunia....

Aliyekua mpiga Bass Guitar wa Skylight Band amefariki
dunia usiku wa kuamkia leo April 17,Marehemu Ayubu
songolo ama Chili Chala ambaye alizoeleka kwa jina hilo
amefariki ghafla ambapo taarifa inasema alianguka akiwa
nyumbani kwake.
Marehemu Alikimbizwa hospitali akiwa amepooza mwili na
ameacha Mke na watoto wawili,miongoni mwa bendi
alizowahi kuzifanyia kazi ni bendi ya Akudo Impact,Fm
Academia na mwaka jana alijiunga na Skylight
band,mipango ya mazishi inafanywa nyumbani kwake
Mwanyamala B karibu na msikiti wa Hidaya.
Kuhusu Onyesho ambalo huwa linafanywa kila Alhamisi
Escape One na Skylight Band,wametangaza kuahirisha
kutokana na msiba huu. BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA....JIANA LA BWANA LIHIMIDIWE(INA LILLAH WA INA LILLAH RAJUN)


Posted via Blogaway

Friday, April 11, 2014

DIMPOZ NA WEUSI KUFANYA KAZI MOJA......

Kutokana na ile ishu ya wizi wa vitu mbalimbali kwenye
gari la Ommy Dimpoz ambao ‘inadaiwa’ ulifanywa na
rapper kutoka WEUSI (Lord eyez) labda ulihisi kunaweza
kusiwe na uhusiano mzuri kati ya Ommy Dimpoz na
WEUSI.
Nakumbuka siku kadhaa baadae Nikki wa II aliongea na
Chanzo chetu na kuwaonya wale mashabiki wa Arusha
waliosambaza comments kwenye baadhi ya post za
mitandao mbalimbali, kuacha kusambaza vitisho dhidi ya
Ommy Dimpoz kutokana na ripoti aliyoitoa kuhusu hilo
tukio.
Good news kwenye usiku wa April 10 2014 Ommy Dimpoz
amepost picha akiwa studio na WEUSI ambao ni G Nako na
Nikki wa II na kuandika haya maneno yafuatayo hapa chini
ambayo yanaonyesha uhusiano wao uko poa kwa sasa.


Posted via Blogaway

Wednesday, April 9, 2014

MZUNGU KICHAA AMPONDA ALLY KIBA KWA KUDAI KUA ATALIPWA PESA NDEFU KWENYE SHOW YAKE HUKO UJERUMAN....

Kati ya vitu ambavyo husaidia kuongeza thamani ya msanii katika
macho ya mashabiki ni pamoja na watu kuona akipata dili kubwa
na kulipwa pesa nyingi katika shows.Lakini kumekuwepo baadhi
ya wasanii ambao wakati mwingine hutengeneza mazingira ya
uongo hasa kupitia mitandao ya kijamii, na wengine hata kufanya
na Interviews ili tu kufanya watu waamini kuwa thamani yao pia
iko juu.
Mzungu Kichaa yuko tofauti kidogo katika hilo, sababu haoni
sababu ya msanii kudanganya kwa kitu ambacho sio kweli.
Msanii huyo wa Denmark aliyeishi Tanzania kwa miaka mingi
alizunguzungumzia swala hilo katika kipindi cha Sporah.
“Mimi siwezi kwenda kwenye vyombo vya habari na kusema ooh
nimetengeneza milioni 100 kwenye show halafu media zote
ziseme ‘oooh wow’…kama alivyofanya Alikiba kipindi fulani”
Alisema Mzungu Kichaa. “Alisema alikuwa anataka kwenda
kufanya show Ujerumani, na alikuja kusema ameahirisha kwenda,
tena aliahirisha siku moja kabla, na kusema kuwa angelipwa
shilingi milioni 100…Kwahiyo akadai kwamba alikuwa anapewa
hiyo hela lakini mikataba haikwenda kama ilivyotakiwa so
aliahirisha show siku moja kabla, na kama mwanamuziki mimi
najua jinsi mambo ambavyo hua yanakuwa, siamini watu
waliokuwa tayari kumlipa kiasi cha pesa kama hicho…na kwa wao
kutafuta media publicity kupretend we are getting big money to
perform nadhani hilo ni kosa.” Alimaliza


Posted via Blogaway

KWA MARA YA KWANZA DIAMOND APIGA SHOW KATIKA UKUMBI WA NGUVU ambao....

KWA MARA YA KWANZA DIAMOND ANAFANYA
SHOW KATIKA UKUMBI MKUBWA HUKO TEXAS
AMBAO JAY Z,P DIDDY,RICK ROSS,TI,YOUNG
JEEZY,P SQUARE NA WENGINE WENGI
WALIKWISHA UTUMIA...!!
LIMITED ADVANCE TICKETS ONLINE NUNUA YAKO MAPEMA
MLANGONI
ZITAONGEZEKA….BOFYA WWW.DIAMONDUSATOUR.COM
KWA MARA YA KWANZA KABISA SHOW HII  ITAFANYIKA KATIKA
UKUMBI AMBAO JAY Z,P DIDDY,RICK ROSS,TI,YOUNG JEEZY,P
SQUARE NA WENGINE WENGI WALISHA UTUMIA KUANGALIA
UKUMBI HUO


Posted via Blogaway

KATIKA KUADHIMISHA SIKU HII YA KIFO CHA KANUMBA,LULU AFUNGUKA

Leo ni siku muhimu ya kumuenzi The late Kanumba(KANUMBA THE GREAT) wapo wasanii
na watu maarufu walioonyesha hisia zao katika siku hii ya
kumuenzi kanumba kutokana na mapinduzi makubwa na jitihada
zake alizozionyesha katika sanaa ya uigizaji. kwa maneno
machache Lulu amemuezi hivi!!
Nukuu "Bado siamini kama mwaka wa pili unakatika bila kukuona
wala kukusikia baba...!! ila naamini bado tupo wote kiroho na
Ninaamini zaidi nafsi yako huko ilipo inasimama kunitetea na
kunipigia, inaweza kunichukua miaka na miaka kukuelezea,,.. u
still liv in me daddy and your dearly missed .... R.I.P daddy
angu." alimalizia kwa kusema hivo.


Posted via Blogaway

Sunday, April 6, 2014

PASTOR ANASWA AKIFANYA UFUSKA KWENYE DANGURO.....

OPARESHENI Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishers
inaendelea! Wiki hii ilifanya kazi nyingine nzito, kumnasa
Pastor John Paul Simon Rubanguka wa kanisa la kiroho la
Maximum Deliverance lililopo Masaki, Dar ambaye alinaswa
akichezewa utupu na wanawake watatu ambao ni kama
waumini wake kwa sababu wote ni Wakristo.
Pasta John Paul Simon Rubanguka wa kanisa la kiroho la
Maximum Deliverance lililopo Masaki, Dar baada ya
kunaswa na wanawake watatu wakimchezea utupu.
OFM YATONYWA UCHAFU WA PASTOR Ilikuwa Jumanne ya
Aprili Mosi, 2014, saa 4:14 asubuhi, chanzo cha habari
kilipiga simu chumba cha habari cha Global na kuwataka
makachero wa OFM ambapo alipounganishwa nao alisema:
“Jamani kama kweli hapo ni OFM nina malalamiko. Mimi
nimeshtukia mchezo mchafu unaotaka kufanywa na pastor
(mchungaji) mmoja anaitwa Rubanguka.
Pasta John Paul Simon Rubanguka akijaribu kujitetea.
“Huyu pastor amempa dili dada mmoja kumtafutia
wasichana wazuri watatu na kuwapeleka kwenye nyumba
moja hivi kisha wawe wanamchezea utupu wake huku wao
wakiwa kama walivyozaliwa, ndiyo furaha yake ilipo.
Wasichana wameshapatikana.”
Makamanda wa Polisi wakimbananisha na kumtuliza
Pasta huyo ili apunguze munkari.
MSHIKO WA NGUVU NA SAFARI JUU Mtoa habari huyo
aliendelea kudai kuwa, pastor huyo alisema wasichana
watakaokuwa wakichezea utupu atawafanyia usaili wa kwenda
kuwauza kwenye kasino moja iliyopo Uarabuni ambayo yeye
ni wakala wa kuwapelekea malaya huko.
Pastor
akiwa na mmoja wa wanawake waliofumaniwa naye.
Chanzo hicho kiliendelea kudai kuwa, pastor huyo aliwaahidi
wanawake hao kitita cha shilingi 300,000 kila mmoja kwa
wale watakaofaulu kumchezea vizuri, sanjari na kuwakatia
hati za kusafiria ‘passport’.
Makamanda wa OFM wakimtuliza Pasta.
OFM YAWEKA MTEGO Baada ya kupata ishu nzima, OFM
ilifanya ukachero na kugundua mahali ambapo tukio hilo
lilipangwa kufanyika, ni kwenye danguro moja lililopo
Kinondoni jijini Dar.
Wanawake walionaswa katika tukio hilo wakivaa viwalo
vyao.
OFM ilifika kwenye nyumba hiyo na kufanya ushushushu
wake ambapo walifanikiwa kuweka mitambo yao sambamba
na kulishirikisha jeshi la polisi kwa ajili ya kumnasa
mtumishi huyo wa Mungu akifanya vitendo hivyo.
Saa 8:11 mchana, OFM wakiwa wamejibanza eneo hilo
waliwashuhudia warembo watatu, weupe wakielekea kwenye
nyumba ambayo mtoa habari wetu aliielekeza.
Kitambulisho cha Pasta.
PASTOR AWASILI KWA MBWEMBWE Saa 11:23 jioni, OFM
wakiwa hawajaanza hata kujisikia kuchoka, walimwona pastor
huyo akiwasili kwa mbwembwe akiwa ndani ya gari dogo na
kugeuza kwa staili ya kupiga ‘norinda’ kisha akashuka.
Mkononi alishika maji makubwa. Alipokelewa na mmoja wa
wanawake hao.
Bango lililopo Kinondoni Mkwajuni, Dar likieleza lilipo
kanisa la Pasta huyo.
MCHEZO WAANZA Saa 11:40 jioni, makachero wa OFM
walifanya uchunguzi wa kina na kubaini kuwa, tayari mchezo
ulishaanza ambapo waliwataarifu polisi na kuungana nao
kwenda kuvamia nyumba hiyo.
Msafara wa OFM na polisi hao ulifika nje ya chumba
kilichokuwa kikidaiwa kufanyika uchafu huo. Sauti ya muziki
na wanawake waliokuwa kama wapo kwenye darasa la siri
zilisikika.
Polisi waligonga mlango na kujitambulisha kisha wakaomba
wafunguliwe mlango haraka ndani ya sekunde chache.
PASTOR APATA MCHECHETO Pasta John na wanawake hao
walitii amri kwa kufungua mlango ambapo mchungaji huyo
alikumbwa na mchecheto na kutaka kurukia juu ya dari lakini
polisi walimtafadhalisha kutulia pamoja na wanawake hao
kama walivyo.
OFM ikiwa chumbani humo iliwashuhudia wanawake hao
wakiwa watupu mbele ya pastor huyo ambapo walikuwa
wakimnengulia viuno.
Baada ya kupewa kibano, warembo hao walimwanika pastor
huyo kwamba ndiye aliyewatuma wamchezee wakiwa watupu
ili awalipe shilingi laki tatu kila mmoja, pia kuwapeleka
Uarabuni kwenye kasino.
UTETEZI WA PASTOR Kwa upande wake, Pastor John alijitetea
kuwa anaomba asamehewe kwa gharama zozote ili taarifa
hizo zisifike popote kwani ishu hiyo ilikuwa si amri yake bali
shetani alimpitia.
“Jamani naomba tumalize humuhumu ndani, mnajua mimi
ni Pastor wa Kanisa la Maximum Deliverance, sasa ukweli ni
kwamba waumini wangu hawatanielewa, chondechonde
ilindieni kazi yangu jamani,” alijitetea.
Mpaka OFM inaondoka eneo la tukio, pastor huyo na
wanawake ‘wake’ walikuwa kwenye harakati za kupelekwa
mbele ya vyombo vya sheria kwa ajili ya hatua zinazostahili.
KUTOKA MEZANI KWA MHARIRI Siku zote kazi ya OFM ni
kuwajibikia matendo maovu na si kuwaonea watu  kwa lengo
la kuwachafua. OFM inapopata habari huichunguza ukweli
wake kwanza kabla ya kuchukua hatua ya kuifanyia kazi moja
kwa moja, yaani kufika kwenye eneo la tukio.


Posted via Blogaway

BABA AMTESA MWANAE KISA HAPENDI WATOTO WA KIUME...

Mtoto Amos Baya mwenye umri wa miaka minne ambaye
toka kuzaliwa kwake amekuwa akipata mateso kutoka
kwa baba yake kisa kwanini kazaliwa wa kiume,hali
iliyosababisha mtoto huyo kudhoofika mwili na kupata
ugonjwa wa utapiamlo Vidole vya mtoto Amos Baya vinavyoonekana hapo
vimevunjwa haviwezi kunyooka Wakati watu wengine wanakesha kutafuta watoto lakini
pia wadau mbalimbali wakiendelea kupiga vita ukatili dhidi
ya watoto,vitendo vya ukatili dhidi ya watoto vimeendelea
kujitokeza katika jamii ambapo huko katika kijiji cha
Senane wilayani Maswa mkoa mpya wa Simiyu mwanamme
mmjoa aitwaye Baya  Seni amekuwa akimpa mateso makali
mtoto wake wa kiume mwenye umri wa miaka minne ili afe
kwa madai kuwa hapendi watoto wa kiume.
Baya Seni ambaye ni mkazi wa kijiji hicho cha Senane
amekuwa akimpa mateso makali mtoto huyo anayejulikana
kwa jina la Amos Baya mwenye umri wa miaka minne toka
kuzaliwa kwake hali  iliyoelezwa kusababisha mtoto huyo
kudhoofika mwili na kupata ugonjwa wa utapiamlo.
Miongoni mwa mateso aliyoyapata mtoto huyo ni pamoja
na kuvunjwa vidole vya mkono wa kushoto, kutelekezwa
shambani siku zaidi ya mbili bila kula na kuning'inizwa juu
ya mti.
Imeelezwa kuwa Mwanamme huyo hapendi watoto wa
kiume kwa madai kuwa wanaleta umaskini kwa sababu
wakikua watataka kuoa na kuchukua mali, lakini mtoto wa
kike akikua ataolewa na kuleta mali nyumbani.
Taarifa za mtoto huyo kupata mateso kutoka kwa baba
yake mzazi zilitolewa na msamaria mwema   siku ya tarehe
31 mwezi Machi mwaka huu  ambaye alikwenda katika
shughuli za mazishi katika kijiji hicho na kumwona mtoto
huyo ndipo akapiga simu ofisi ya ustawi wa jamii wilaya ya
Maswa na kufuatia taarifa hizo ofisi hiyo iliwataarifu polisi
na wakaenda kumchukua mtoto huyo na kumuweka chini
ya ulinzi baba mzazi wa mtoto huyo.
Afisa ustawi wa jamii wilayani maswa Bwana Husein
Mshana amethibitisha kutokea kwa tukio hilo
Hivi sasa mtoto huyo amelazwa wodi namba nane ya
watoto katika hospitali ya wilaya ya Maswa akipatiwa
matibabu.
Mama mzazi wa mtoto huyo  Elizabeth Paul amekiri kuwa
mtoto huyo amekuwa akifanyiwa vitendo vya ukatili na
baba yake mzazi na kwamba hata yeye  amekuwa akipewa
vitisho kuwa endapo atasema atauawa.
Tayari baba mzazi wa mtoto huyo Amos Baya anashikiliwa
na jeshi la polisi wilayani maswa kwa hatua za kisheria.


Posted via Blogaway

Friday, April 4, 2014

WATU WALIOFUNIKWA NA KIFUSI LEO HUKO BUNJU-MBWENI DSM WAFARIKI DUNIA.....

Inasemekana watu watatu waliotambuliwa kwa majina ya
Msagala,Jacob na Mhando ambao ni  wakazi wa Bunju jijini
Dar es Salaam wamefariki dunia mchana wa April 04
baada ya kufukiwa na kifusi wakati wakichimba kokoto.
Watu hao walikua wakichimba kokoto hizo kwenye
machimbo ya Mtanzania mwenye asili ya Kiasia
aliyefahamika kwa jina la Kara Arjan machimbo yaliyopo
eneo la Bunju-Mbweni Dar es salaam.
Taarifa inasema kuwa machimbo hayo yalishapigwa
marufuku kutokana na watendaji wake kufanya kazi katika
mazingira hatarishi ambapo wachimbaji hao wakiwa
kazini,sehemu ya machimbo hayo iliporomoka na
kuwafukia.
Picha za kwenye tukio ambazo zinaonyesha pia juhudi za
watu wakiendelea na uokoaji pamoja ndugu wa waliopoteza maisha


Posted via Blogaway

KAJALA APEWA ZA USO NA TEAM WEMA INSTAGRAM.....

Hehehe kweli ushoga wa mujini kazi jamani sasa huyu bibie
na BFF wa madame Wema alipiga picha na hawa wadada
wawili wanaodaiwa kuwa maadui wa Wema. Yeye binafsi
hakuipost picha hiyo Instagram bali alipost picha hiyo hapo
chini akiwa na Profesa Jay lakini wajuaji wameisaka hadi
kuipata na ndipo kasheshe ikaanza kama ifuatavyo mpaka
kumtukania mwane:
usipojipangantakupanga:
KIUKWELI NAJUA HUWEZI KULAZIMISHA MTU AWE NA
USHOGA NA FULANI, LAKINI USTAARABU UNAPOACHA
USHOGA NA MTU YAACHE NA MAMBO YAKE!SIO WEWE
KAJALA UMEAMUA KUJITOA KWA WEMA SASA HABARI
ZAKE UNAZIONGEA ZA NINI KWA WATU?KWA WEWE
WEMA HANA SIRI ZAKO??SO ULICHOKIFUATA KWA WEMA
NI HICHO TU KUDAKA MAKOMBO ANAYOYAACHA?
UNADHANI HUYO CLEMENT ATAKUPA UTAJIRI WA
MILELE?WATU MATAJIRI WA KUZITAFUTA NA
WANAFILISIKA UTAKUWA WEWE MTEGEMEA VYA
KUHONGWA NA MABWANA ZA WENZIO??HUKO
ULIKOENDA KUKUTANA NA PENNY NA WOLPER
ULIDHANI WATU HAWATOJUA?BUHAHAHA WOLPER
KAPOST PICS NYINGI SANA LKN HII HAKUPOST KWA
NINI?WHY?BUHAHAHA!NA WAKATI UNAPIGWA PICHA YA
GAFLA KWANINI ULIKUWA UNAZIBA SURA?HAHAHA
TUSHAKUELEWA ANA WAIT FOR YOUR TURN!DHIKI
INAKUPONZA SANA WEWE!UMEITIA AIBU FAMILIA YAKO
KWA ULICHOMFANYIA WEMA!HAO WANAOJIFANYA
MARAFIKI ZAKO NOW WALIKUWA WAPI ULIPOTAKA
KUFUNGWA MPK WEMA AKAKUTOLEA HIZO PESA?WOLPER
ALIWAHI KUJA KUKUONA HUKO JELA WKT UNAFIRWA NA
MAASKARI ?NA HUYO PENNY ALIKUJA??YAANI SOON
KIBAO KINAKUGEUKIA JUST WAIT!!
LEO UMEUMBUKA MPK UNAONA AIBU!UMEPOST PIC
ULOPIGA NA PROFESA JAY MBONA ULOPIGA NA PENNY
NA WOLPER HUKUPOST?ULIJUA ITAKUWA SIRI EEH??
HAKUNA SIRI HAPA UMEUMBUKA NA BADO
TUTAKUUMBUA SANA!!!POST NA HIYO ULOPIGA NA
PENNY BASI USIOGOPE TUSHAKUJUA WEWE MNAFKI!!
SASA HIVI TUNAKUWEKA PENDING!TUNAANZA KUDEAL
NA MWANAO PAULA NAE KAWA MA**** KM WEWE
MAMA AKE ANAT*****A NA KUF****A NA DOGO JANJA
NA EEWE AHAAA UNAFURAHIA TU!! HESABU MASAA TU
SOON TUNAANZA KUPOSI UCHI NA MKUNDU WA
MWANAO PAULA SI UBAMFUNDISHA AJIBINUE UPOST PIC
APATE WANAUME!MWAKA WAKO HUU MAMAE!MSHAMBA
MKUBWA EEWE! TANGU HUONGWE HILO GARI KILA
PICHA UNAPIGIA KWENYE GARI BUHAHAHA MAGARI
WATU TUMEKUA NAYO ACHA USHAMBA!NA M****
UKISHAEXPIRE CLEMENT ANAKUNYANGANYA HILO GARI!!
MUUZA M**** WE NDIO MAANA PFUNK ALIKUTEMA KWA
TAMAA ZAKO HIZO!


Posted via Blogaway

LULU AIMBA WIMBO WA BASI NENDA KATIKA SAUTI YA KIMAHABA...

Mtoto Mrembo Elizabeth Michael "Lulu" akiimba wimbo
"Basi Nenda" kwa pozi kali la Kimahaba.
Jamani huyu mtoto ni shidaaa sana.... kabarikiwa sauti
na uzuri pia..na ameonekana akiimba wimbo huo wa basi nenda na kuacha gumzo kwa mashabiki wake na watanzania wote kiujumla...chanzo hiki cha princenordy hakikuweza kupata sababu ya mrembo huyu kufanya hivi...

Wewe wasemaje kuhusu hili?


Posted via Blogaway

NEY WA MITEGO AELEZA SABABU YA KUTAKA KUMUOA SIWEMA....

MWANAMUZIKI Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’
amesema yupo kwenye mikakati ya kufunga pingu za
maisha na mpenzi wake anayejulikana kwa jina la
Siwema baada ya kumtundika mimba.
Nay akiwa na mpenzi wake Siwema.
Akipiga stori na paparazi wetu hivi karibuni, Nay
alisema anajivunia kukaribia kuitwa baba na kizuri ni
kwamba msichana aliyempa mimba alikuwa na ndoto za
kumuita mke wake hivyo ndoa itafungwa kabla ya mtoto
kuzaliwa.
“Kikubwa naomba Mungu mipango yangu iende kama
nilivyopanga kwa sababu nataka kabla mtoto hajazaliwa
tuwe ni wanandoa tunaotambulika kwa Mungu kwa
kufunga pingu za maisha,” alisema Nay.
Akizungumzia kubebeshwa mimba na msanii huyo,
Siwema aliliambia Ijumaa: “Najisikia furaha sana
kumbebea mimba Nay, tumetoka mbali naamini ndoto
yetu ya kuoana itatimia siku si nyingi.”
at Editor  8:43 PM


Posted via Blogaway

HIVI NDIVO SHOW MPYA YA DADA WA DADA AKE RAPA VICTORIA KIMANI ITAKAVOKUA....

Dada wa Rapa Bamboo wa Kenya Victoria
Kimani ameanzisha reality show yake ambayo
itakua na baadhi ya show alizowahi kuzifanya
kipindi cha nyuma,interviews za radio na
wakati wa kurekodi studio (studio session).
Reality show hii mbali na kuonekana kwenye
king’amuzi pia itaonekana kwenye kwenye
chaNnel yake ya Youtube kila wiki,tarehe
rasmi ya kuanza kuonekana ni April 08 na
zitaanza kuonekana kuanzia Jumanne kupitia
Youtube,jina la show hii inaitwa The rise of
the Queen.
Hivi ndivyo itakavyokua.


Posted via Blogaway

MICROSOFT HAVE LET GO OF OTHER INTERNET APPS.....

Developing wearable tech and other ideas
for the Internet of Things just got a lot
cheaper. Microsoft announced at their Build
conference on Wednesday that they will give
away licenses for their Windows operating
system for free on any device with a screen
of less than nine inches. That means
manufacturers of small tablets, phones and
any other small devices won't have to buy a
license from Microsoft to use Windows,
making it a lot more competitive with the
Google Android operating system.
The announcement of the new policy
accompanied a whole host of other news
from Microsoft involving the new Windows
Phone 8.1 and other software updates but
for the free Windows licenses will likely
stand out to startup companies and device
makers as the biggest news since they will
be able to spend money that would have
gone to a license on other ways of
improving their product.
"The news today shines a light on continued
Windows innovation in ways that benefit our
customers, partners and developers alike,"
said Terry Myerson, executive vice
president of Microsoft's OS group during
the keynote where the announcement was
made. " Our commitment is to make
Windows more personal and accessible to
individuals, and to ensure a vibrant
ecosystem through closer collaboration with
our industry partners."
The Internet of Things is a pretty broad
term but Microsoft was proud to show off
some of the possibilities of Windows on tiny
devices and applied to the growing "maker"
market in areas like 3D printing. Of course
part of the draw to the Internet of Things is
how it's possible to connect numerous small
devices, phones, wearable technology that
tracks vital signs, even to smart appliances
in the home. It's easier to build applications
for them if they run on the same system
and if that system is both widely known like
Windows and free to license as it will be
now, developers could easily turn to
building with Windows in big numbers.
Microsoft has been attempting to build a
market in smaller devices like tablets and
smartphones where iOS and Android have
continually dominated. Encouraging
manufacturers to switch to Windows with a
free license may be the solution especially
when phone makers, although able to use
Android for free, still have to pay Google to
put Google apps on the phone.
It's easy to get caught up in the hype of the
Internet of Things but when a juggernaut
like Microsoft starts making real
commitments to building on it, the
predictions of economists and the
projections of entrepreneurs building smart
devices look a lot more certain


Posted via Blogaway