Wakazi wa eneo la Salasala wilayani
Kinondoni, Dar es Salaam wamepinga
uamuzi wa serikali kumpatia kibali
mwekezaji wa kampuni ya Mayfair na
kuziba barabara iliyokuwa ikitumika
kwa miongo miwili.
Mwenyekiti wa Kamati ya usimamizi
wa barabara hiyo, Seleman Magingi,
alisema hatua hiyo ya serikali
itawasababishi usumbufu wakazi
zaidi ya kaya 150 na viwanda.
Alisema mazingira ambayo kibali
hicho kimetolewa, yanaonyesha
viongozi wa Serikali ya Mtaa
kushawishiwa na rushwa.
“Kama mazingira hayo hayakuwa
rafiki mbona wananchi na wenye
viwanda hatukushirikishwa,ndiyo
maana mwekezaji huyo amepata
kiburi,” alisema Magingi.
Mmoja wa wakazi hao,Irene Shayo
alisema viongozi hao wanapaswa
kuangaliwa vizuri kupitia mwekezaji
huyo na kupoteza haki ya wananchi
kwa kununuliwa.
Alisema awali mwekezaji huyo
aliwarubuni kuwa atawaboreshea
miundombinu kama barabara,umeme
na maji wakati huduma hizo
zinapatikana kwa msaada wa viwanda
vilivyopo.
“Kufungwa kwa barabara hiyo
kutasitisha huduma zote za kijamii na
kiuchumi,”alisema.
Afisa Mtendaji wa Mtaa wa
Salasala,Ramadhan Ntai,eneo hilo
limefungwa baada ya mmiliki wa
kiwanja hichi kupata kibali kutoka
Wizara ya Ardhi,Nyumba na Makazi.
Alisema Wizara hiyo ilimtaka
Mwekezaji huyo kufanya marekebisho
ya ujenzi wa kubadilisha matumizi ya
kiwanja hicho ili barabara ipatikane.
Naye, Mmiliki wa Kampuni ya Mayfair
ambaye hakupenda jina lake
liandikwe alisema hayupo tayari
kuzungumza na vyombo vya habari.
“Siwezi kuongea na
waandishi,mtendaji anafahamu kila
kitu mtafuteni yeye,”alisema.
Diwani wa Kata ya Wazo, John Morro,
kupitia barua yake ya Oktoba mwaka
2013 yenye kumbukumbu namba
DSM/KN/2013/22, kwenda kwa
Mkurugenzi wa Ramani wa Wizara ya
Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya
Makazi ikiwataarifu kufufuliwa kwa
barabara hiyo.
Barua hiyo ilikitaka kiwanja namba
10/211 Becon YP 366, 362, 849, 847,
kuacha eneo la barabara kwa ajili ya
jamii.
Tuesday, September 30, 2014
WAKAZI WA DAR WAPINGA MWEKEZAJI KUZIBA BARABARA
KURA ZA HAPANA ZAENDELEA KURINDIMA BUNGENI
Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba,
akipiga kura wakati wa zoezi la
kupigia kura Rasimu ya Katiba
inayopendekezwa na bunge hilo mjini
Dodoma jana.Picha/ Khalfan Said.
Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba,
jana walianza kupiga kura kupitisha
Rasimu ya Katiba inayopendekezwa,
huku ikifanyika kampeni kali kusaka
theluthi mbili za wajumbe baada ya
suala la Mahakama ya Kadhi
kushindikana kuingizwa kwenye
rasimu hiyo.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda,
wajumbe watatu wanaowakilisha
madherhebu ya dini na Mwenyekiti wa
Kamati ya Uandishi, Andrew Chenge,
walipewa fursa ya kuzungumza na
kutoa kauli za kuwashawishi wajumbe
wakubali kuipitisha rasimu hiyo huku
suala kubwa likiwa ni Mahakama ya
Kadhi.
KAULI YA PINDA
Kabla ya hatua ya kupiga kura kuanza
jana alasiri, Waziri Mkuu, Mizengo
Pinda, alilazimika kutoa tamko la
serikali kufuatia taarifa kwamba
wajumbe hususan ambao ni waumini
wa dini ya Kiislamu, wamedhamiria
kuipigia kura ya `Hapana' rasimu
hiyo.
Msimamo wa kuipigia kura za
`hapana' rasimu hiyo ulitolewa
mwishoni mwa wiki na baadhi ya
wajumbe kwa nyakati tofauti bungeni
wakati wakihakiki Rasimu ya Tatu
iliyowasilishwa na Mwenyekiti wa
Kamati ya Uandishi, Andrew Chenge,
ambayo haijaingiza suala la
Mahakama ya Kadhi kama ambavyo
walitaka iwe.
Akitoa tamko hilo, Waziri Mkuu Pinda,
alisema linafuatia kikao cha
maridhiano cha pamoja kati yake na
Kamati ya Uongozi wa BMK ambacho
pia kiliwashirikisha pia viongozi wa
dini za Kiislamu na Kikristo.
Alisema suala la Mahakama ya Kadhi
ambalo lilianza tangu mwaka 2005,
lilifikia hatua nzuri kwa waumini wa
dini ya kiislamu kuanzisha mahakama
hizo mikoa yote nchini, mwaka
2011/12.
Hata hivyo, alisema tatizo ambalo
limejitokeza kwa sasa ni utekelezaji
wa maamuzi yanayofikiwa kwenye
mahakama hizo kwa upande wa
serikali.
Alisema: “Taifa hili ukiondoa ubaguzi
serikali na kama nchi tumejitahidi
sana kama serikali, tumejitahidi sana
kama nchi kutenganisha shughuli za
imani za dini na shughuli za serikali.”
Alisema huo ndiyo msingi muhimu
sana kwa sababu serikali haina
dini.“Serikali hii haina dini…nchi hii
haina dini, lakini kwa Mtanzania
mmoja mmoja, lazima tuheshimu sana
yale ambayo yeye anaamini kwa imani
yake,” alisema. Alisema kazi ya
serikali ni kuweka mazingira mazuri
ya kuhakikisha kila mmoja anapata
fursa nzuri ya kuamini imani yake.
Alisema nguzo hii muhimu imesaidia
sana kujenga umoja, amani, utulivu
na mshikamano wa taifa hili kwa
kipindi chote hicho na kwamba ni
matarajio ya Katiba mpya nayo italeta
mshikamano huo kwa miaka mingi
ijayo.
“Nawaombeni sana wote katika jambo
hili tusitetereke, tukatae hisia zozote
ambazo zitatuletea uvunjifu wa
amani,” alisema.Alisema baada ya
kikao chao cha Jumamosi, viongozi
hao wa dini waliitaka serikali kutoa
ahadi ni lini sasa wataboresha sheria
zake ili maamuzi yanayotolewa na
mahakama hizo yasiendelee
kupuuzwa yanapopelekwa serikalini.
Pinda alisema kwa kuzingatia
umuhimu huo, serikali itaziangalia
sheria zake mbili ambazo ni Sheria ya
Mahakama ya Mahakimu, Sura yua 11
na Sheria ya Kiislamu, sura ya 375, na
wataleta muswada bungeni ifikapo
Januari mwakani.
Alisema kabla ya kuwasilisha
muswada huo utawashirikisha wadau
wengi na ukifikishwa bungeni
wataangalia namna gani bora ya
kutekeleza maamuzi yao. Anasema
awali alikuwa mbumbumbu sana
katika eneo hilo, lakini baada ya
mazungumzo hayo ameelewa vizuri.
SHEIKH THABIT JONGO
Akizungumza baadaye Mjumbe wa
BMK, ambaye anatoka kundi la 201
(dini), Sheikh Thabit Jongo, alisema
wajumbe bungeni humo wanashukuru
kwa tamko lililotolewa na serikali
kupitia Waziri Mkuu.
“Wajumbe humu ndani wathamini
kauli ile iliyotolewa na Waziri Mkuu…
kitu nyeti na kinachoweza kuvuruga
amani ni suala la imani ya dini mtu.
Humu ndani suala la Mahakama ya
Kadhi lilitaka kutuvuruga,” alisema.
Alisema wapo Waislamu ambao
walikuwa hawaipendi mahakama hiyo
na wapo Wakristo pia ambao hawataki
mahakama hiyo.Lakini kutokana na
tamko lililotolewa na Waziri Mkuu
jana, anawaomba wale wote
waliokuwa na mipango ya kuipigia
kura ya hapana rasimu hiyo sasa
mipango hiyo waifute.
Sheikh Thabit alisema maadui wa
bunge hilo ni watatu ambao ni
kwanza kundi la Umoja wa Katiba ya
Tanzania (Ukawa) ambao wangependa
bunge hilo livunjike.
Alimtaja adui wa pili kuwa ni
aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya
Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph
Warioba, ambaye mara kwa mara
amesikika akilipinga bunge hilo na
hata kudai kuwa atakwenda mitaani.
Adui wa tatu kwa mujibu wa Sheikh
Thabit, ilikuwa ni suala la Mahakama
ya Kadhi, lakini kutokana na tamko la
serikali jambo hilo litashughulikiwa
ifikapo Januari mwakani kwa maana
ya kurekebisha sheria ili utekelezaji
wa maamuzi ya mahakama hizo
yaweze kushughulikiwa na serikali.
Sheikh Hamid Jongo
Kwa upande wake, Sheikh Hamid
Masoud Jongo, alisema kwa kuwa
tamko hilo limetolewa na ofisi ya
Waziri Mkuu kwa maana ya taasisi
basi utekelezaji wake usiwe na
kigugumizi tena kesho kutwa.
Alisema Waislamu hawana nia haswa
ya kuvuruga mchakato huo, lakini
akataka ahadi iliyotolewa na Waziri
Mkuu iheshimiwe.
ASKOFU MTETEMELA
Naye Askofu Mkuu Mstaafu wa Kanisa
la Anglikana Tanzania, Donald
Mtetemala, alisema suala la
Mahakama ya Kadhi kwa muda mrefu
lilileta wasiwasi kutokana na hofu ya
kusababisha mpasuko kwa jamii ya
Watanzania.
Alisema upo mpasuko wa kisiasa,
lakini mpasuko wa kidini ni mbaya
sana, hivyo ndiyo maana suala hilo
limechukua muda mrefu ili kulipatia
ufumbuzi.
“Nimeona roho ya kuvumiliana,
ukomavu katika tamko la Waziri Mkuu
Pinda. Alisema rasimu hiyo ina suala
la msingi kwamba serikali na nchi hii
kwa ujumla haina dini.Aliwaomba
waumini wa dini ya Kikristo kuelewa
suala hilo kwa mapana yake.
CHENGE
Mapema Mwenyekiti wa Kamati ya
Uandishi, Andrew Chenge,
akiwasilisha marekebisho ya Rasimu
ya Katiba inayopendekezwa alisema
rasimu hiyo imefuta na kuandika upya
Ibara ya 2(2) ambayo sasa itakuwa
ikisomeka kuwa, “Rais wa Jamhuri ya
Muungano atakuwa na mamlaka ya
kuigawa Jamhuri katika mikoa, wilaya
na maeneo mengine:
Alisema: “Isipokuwa kwa upande wa
Tanzania Bara, Rais atashauriana na
Rais wa Zanzibar kabla ya kuigawa
Tanzania Zanzibar katika mikoa,
wilaya au maeneo mengine.”
Kabla ya marekebisho hayo, rasimu
yake aliyoiwasilisha wiki iliyopita,
ilisema kwamba Rais wa Jamhuri
angekuwa na mamlaka ya kuigawa
mikoa, wilaya Tanzania Zanzibar,
lakini bila kushauriana na Rais wa
Zanzibar.
Aidha, alitaja marekebisho mengine
kuwa ni kuongeza Ibara mpya ya 44A
inayozungumzia Haki za wakulima,
wafugaji, wavuvi na wachimbaji
madini.
Pia, alisema rasimu imeongeza Ibara
mpya 48A kuhusu Haki ya afya na
maji safi na salama na Ibara ya 55
imefanyiwa marekebisho na kuweka
haki kwa wazee.Alisema Ibara
nyingine iliyoongezwa ni ya 100A
inayohusu Makamu wa Kwanza wa
Rais kushindwa kumudu majukumu
yake.
Kuhusu idadi ya mawaziri alisema
rasimu imeweka ukomo kwamba sasa
imeweka idadi ya mawaziri na
manaibu wao wasizidi 40.
Alisema rasimu pia imeunda Tume ya
Uratibu na Uhusiano ya Muungano
ambayo itakuwa ikishughulika na
usuluhishi wa migogoro kati ya pande
mbili za Muungano kabla ya kufikisha
migogoro hiyo Mahakama ya Juu.
Ibara nyingine mpya ni 208A ambaye
inazungumzia Tume za Kisekta
ambayo itakuwa na tume mbalimbali
za huduma. Kadhalika, alisema
rasimu imeongeza ibara nyingine
mpya 242 kuhusu Udhibiti wa rushwa.
UPIGAJI WA KURA
Zoezi la upigaji kura lilianza kwa
kusuasua baada ya baadhi ya
wajumbe hasa wa kutokea upande wa
Zanzibar, kuikataa kwa kupiga kura za
wazi.
Hatua ya baadhi ya wajumbe kutoka
Zanzibar kupiga kura ya hapana,
ilitarajiwa kutokana na msimamo wao
wa awali waliouonyesha baada ya
suala la Mahakama ya Kadhi
kutoingizwa kwenye Rasimu hiyo.
Wajumbe hao bila woga walipiga kura
ya wazi na kutamka kuwa hawaungi
mkono ibara zote za Rasimu hiyo.
Hata hivyo, wapo baadhi ya
Saturday, September 27, 2014
HUNA HAJA YA KURUDIA RUDIA WIMBO MPYA WA CHRISS BROWN (NEW FLAMES)..LYRICS ZAKE HIZI HAPA
There can be one only you
And, baby, God can never make two
And I know you came here with your
crew
But I promise you that it feels like it's
just us two, aha.
[Bridge: Chris Brown:]
Oh, I don't know what you had
planned to do tonight
But I just wanna be the one to do
you right, right
And we're standing here looking at
each other, baby, eye to eye
And I'm hoping that you're thinking
about leaving with me tonight
[Hook: Chris Brown:]
Who said you can't find love in the
club?
'Cause I wanna tell them they're
wrong
Come on, just, baby, try a new thing
And let's spark a new flame
You gon' be my baby
Love me, love you crazy
Tell me if you're ready
Baby, come and get it
Try a new thing
And let's spark a new flame
[Verse 2: Usher:]
I can't believe you came here all
alone, baby girl, where's your lover?
Oh, it don't really matter 'cause I got
plans to get to know you better,
yeah.
Baby, baby, baby, baby, let's make
what we got here last forever
Girl, 'cause I don't wanna let you go,
never
[Bridge:]
Oh, I don't know what you had
planned to do tonight
Girl, I just wanna be the one to do
you right, right
And we're standing here looking at
each other, baby, eye to eye
Baby, I hope that you're thinking
about leaving with me tonight
[Hook:]
Who said you can't find love in the
club?
'Cause I wanna tell them they're
wrong
Come on, just, baby, try a new thing
And let's spark a new flame
You gon' be my, baby
Love me, love you crazy
Tell me if you're ready
Baby, come and get it
Try a new thing
And let's spark a new flame
[Verse 3: Rick Ross:]
Home plate, world series, our nigga
sliding in her
Baby, I'm a boss, I'm talking George
Steinbrenner
Panamera, Yogi Berra, my two-seater
Derek Jeter
Got more stripes than all these niggas
Babe Ruth balling in a Beamer
Collar on my Polo, kisses on my
necklace
All my diamonds watching, now my
watches getting jealous
Smoking on a bomb in my autograph
Lebron's
Yeah, she told me I'm the one, that's
when I only hit it once
[Hook: Chris Brown:]
Who said you can't find love in the
club?
'Cause I wanna tell them they're
wrong
Come on, just, baby, try a new thing
And let's spark a new flame
You gon' be my, baby
Love me, love you crazy
Tell me if you're ready
Baby, come and get it
COUNTINHO,JERRY TEGETE KUONGOZA KESHO
Mbrazili Coutinho na Jerry Tegete
watakuwa miongoni mwa wachezaji
wa Yanga watakaoanza pambano la
kesho la ligi kuu ya Bara dhidi ya
Prisons, kwenye Uwanja wa Taifa,
kocha Marcio Maximo amesema.
Akizungumza na Nipashe jana,
Maximo alisema anataraji wachezaji
hao wataleta mabadiliko ya kiuchezaji
Yanga na kupata ushindi baada ya
kuanza kwa kufungwa na Mtibwa
Sugar wiki iliyopita.
"Nimefanyia kazi mapungufu
niliyoyaona (katika mchezo wa
kwanza) lakini furaha yangu ni
kurejea kwa washambuliaji Tegete na
Coutinho ambao naamini wataongeza
nguvu na kutuletea ushindi kwenye
mchezo wa Jumapili (kesho),"
alisema Maximo.
Uwepo wa Coutinho, Tegete na
Mbrazili mwingine 'Jaja' kwenye safu
ya ushambuliaji na kucheza kwenye
Uwanja wa Taifa kunampa Maximo
moyo wa kuibuka na ushindi wake wa
kwanza nchini kama kocha wa klabu
ya ligi kuu ya Bara.
Maximo ambaye alikuwa mwalimu wa
Taifa Stars kwa miaka minne tangu
mwaka 2006, amesema beki wa
kushoto Oscar Joshua aliyeumia
kwenye mchezo dhidi ya Mtibwa na
mshambuliaji Hussein Javu
hawatacheza.
Wote wanauguza maumivu ya nyama
za paja.
"Wachezaji wengine wote wapo katika
hali nzuri na naamini wataniletea
ushindi."
Kukosekana kwa Joshua kunatarajiwa
kumfanya Maximo amrudishe Mbuyi
Twite kucheza beki ya kushoto.
Maximo ambaye pamoja na timu yake
wanapewa nafasi kubwa zaidi ya
kutwaa ubingwa wa Bara msimu huu,
alishindwa kuzuia mwendelezo wa
rekodi mbaya dhidi ya Mtibwa kwenye
uwanja wa Jamhuri kwa miaka ya
karibuni timu yake ilipofungwa 2-0.
Friday, September 26, 2014
CHEKI VIDEO ZA FIESTA IRINGA NI SHEEEDAH
KAMA ULIKOSA KUANGALIA SHOW ZA FIESTA ILIYOTISHA NDANI YA IRINGA BASI HII NDIO FURSA YAKO
Thursday, September 25, 2014
BRAND NEW VIDEO BY RICH MAVOCKO-PACHA WANGU
MSANII ALIEKUA KIMYA KWA MUDA MREFU KIDOGO BAADA YA KUACHIA WIMBO WAKE WA ROHO YANGU SASA ADONDOKA NA TRACK NYINGINE INAYOENDA KWA JINA LA PACHA WANGU
PATA LYRICS ZA NYIMBO MBALIMBALI KUANZIA SASA TUNAANZA NA WIMBO WA TYGA-FADED
Faded"
(feat. Lil Wayne)
(Intro)
I don't give a fuck
{Tyga tyga tyga nice to see you}
[Tyga]
Young Nino, fuck a bitch in a pea
coat
Carlito, Scarface, AL Pacino
Bun B do, Pimp C, R-PIDO though
I goes deep in that pussy, Dan
Marino
She wanna be the one, fuck her to my
own single
Break a bitch heart, no future miss
cleo
Snap back, au-au-automatic reload
Flyer than a fucking beatle, you can't
beat 'em
Vampire fuck up your evening
I pop up and eat lunch, leave you in
the cement
Don't believe it, stripe like a fucking
Adidas
The gun selena, give a nigga bieber
fever
Real fucking hot, put it in park
Take a shot, higher than a tube sock
You a bop, give me top top, as I load
the guap
Man these niggas say I'm fly but to
her I'm god
[Hook]
I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
And I don't give a fuck
[Tyga]
Fuck is up, nigga's stomping in my
chucks
Yeah, I make it rain, dear, cause I'm
all about my bucks
Use the butt I'm in the front, dick up
in her cunt
And I put it in her hole, hole in one,
putt putt (wahhhhhh)
Super McNasty, why you McLoving
When the bitch call me daddy
Pimp no caddy, she wish she never
had me
Treat her like a dog, called the bitch
lassy
Young savvy, bang her like Cincinnati
Above average, fly like I'm Aladdin
They bend backwards, throw the
pussy at them
I'm Ben Wallace, dunk up in your
basket
Balls in the air, no games,
I'm serious, double dare
There's too many bitches,
Why these niggas wanna stare
Patron up in here
Nigga this ain't no beer
[Hook]
I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
And I don't give a fuck
[Lil' Wayne]
Mama, there go that monster
Abracadabra, magic Johnson
My motherfucking doctor
Said I need a doctor
So I called house,
Now I am a pill popper
Faded like skinnys
Young money we winning
I told her if I change
She won't get a penny
Milking that shit, pregnant bitch
titties
Bringing home the bacon
I'm fucking miss piggy
Loaded like a semi, semi-naked
pictures
She knows my dick, she call it nigga
Richard
Prior to me cummin, I had to stick my
thumb in
Her ass one time, smell my finger
make you vomit
Flyer than a hornet, the shoe fit I
worn it
She tried to jack me off, can't beat it,
join it
Tunechi, coochie that what she call
it,
Flag Scarlett, I killed it, mourn it
[Hook]
Faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
[Lil Wayne:] Young Moolah baby!
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
My nigga I'm faded faded faded
And I don't give a fuck
WASANII WAHAMASISHWA KUSHIRIKI KWENYE SIKU YA SANAA
Viongozi wa mashirikisho ya filamu
na sanaa za ufundi wamewataka
wasanii wa fani mbalimbali kujitokeza
katika kushiriki semina
zitakazoendeshwa katika Siku ya
Msanii Tanzania.
Semina ya Siku ya Msanii inatarajiwa
kufanyika Oktoba 22 na 23 mwaka huu
katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere
(Makumbusho Posta) na wasanii
watafundishwa mambo
mbalimbali.Rais wa Shirikisho la
Sanaa za Ufundi, Adrian Nyangamale,
alisema wasanii wanapaswa
kujiandikisha kwenye semina hizo ili
kupata ujuzi wa mambo mbalimbali.
“Semina hizi ni muhimu kwa sababu
kutakuwa na wataalamu kutoka katika
sekta mbalimbali ambao watakuja
kutoa mafunzo kwenye semina hizo,
jambo ambalo litachangia uelewa na
elimu ya wasanii, tumekuwa
tukilalamika kuwa hatupati fursa za
elimu lakini Siku ya Msanii imetupa
hiyo nafasi sasa tuitumie,” alisema.
Naye Makamu wa Rais wa Shirikisho
la Filamu, Selemani Ling’ande alisema
wasanii wajitokeze kwenye semina
hizo lakini pia aliwataka wananchi
kujitokeza kwa wingi katika kupiga
kura za kupata watu watakaowania
tuzo za Siku ya Msanii.
“Semina ni muhimu lakini kuna suala
la kutambulika mchango wa wasanii,
hapa ndiyo Watanzania
wanapotakiwa kufanya mapendekezo
yao, kuna fomu zinatolewa kwenye
magazeti na mitandao juu ya Tuzo za
Humanitarian Award na Life Time
Achievement ambazo wasanii wote
wanaweza kushindanishwa,” alisema.
Naye Mkurugenzi wa Kampuni ya
Haak Neel Production, Godfrey Katula,
ambaye kampuni yake ndiyo imepewa
jukumu la kusimamia Siku ya Msanii,
alisema Watanzania wajitokeze
kupendekeza majina ya wasanii
wanaostahili kupata tuzo na Kamati
ya Utafiti itakwenda kuhakiki taarifa
zote zilizowasilishwa kwao.
“Kazi za wasanii zinaanza
kutambulika hapo, wananchi
wanawajua hivyo ni fursa yao
kuonyesha kuthamini kazi zao, lakini
pia tunawataka wasanii wajitokeze
kwenye semina ambazo zitafanyika
kwa siku mbili ili kupata elimu
sahihi,” alisema.
Siku ya Msanii inaandaliwa na
Kampuni ya Haak Neel Production
kwa kushirikiana na Baraza la Sanaa
la Taifa (BASATA).
CHADEMA NA POLISI WAENDELEA KUZOZANA
Jeshi la Polisi limeendelea
kusuguana na Chama cha Demokrasia
na Maendeleo (Chadema) wakati
wafuasi wa chama hicho wakitaka
kuandamana huku polisi
wakiwadhibiti.
Mkoani Kagera, Jeshi la Polisi
limepanga askari wake kila mtaa
katika manispaa ya Bukoba kwa lengo
la kudhibiti maandamano hayo.
Kaimu Kamanda wa polisi mkoani
Kagera, Gilles Muroto, alisema
kupangwa kwa askari hao
kumetokana na kutoeleweka
maandamano ya wafuasi wa chama
hicho yataanzia katika mtaa upi.
“Tunafahamu siku ya kwanza tutapata
changamoto kutokana na askari
wengi kupangwa kudhibiti
maandamano hayo, lakini kadri
tunavyoendelea tutajipanga vizuri
hakuna shughuli ya kuhudumia
wananchi itakayokwama,” alisema
Muroto.
Alisema kuwa Septemba 22 mwaka
huu walipokea barua ya Chadema
wakiomba kuandamana kesho yake
kuanzia saa 3:00 asubuhi, lakini
maombi hayo hayakukubaliwa
kutokana na kupigwa marufuku na
makao makuu ya jeshi hilo.
Jijini Dar es Salaam, jana polisi
walizizingira ofisi za Chadema makao
makuu kudhibiti wafuasi wa chama
hicho wasiandamane.Askari hao
wakiwamo wa Kikosi cha Kutuliza
Ghasia (FFU), walikuwa katika doria
wakiwa kwenye magari mawili aina ya
Land Rover pamoja na silaha za moto.
Hali hiyo iliwafanya wafuasi wa
Chadema kukaa katika vikundi
wakijadili hali ilivyo katika maeneo ya
kuingilia katika makao makuu ya
chama hicho.Afisa Habari wa
Chadema, Tumaini Makene alisema
wanalishukuru jeshi hilo kwa
kuwasaidia kuandamana katika
maeneo mbalimbali ya nchi.
Aliongeza kuwa wana njia 198 za
kuandamana ikiwa ni pamoja na
kuwatumia ujumbe mfupi viongozi wa
Bunge Maalumu la Katiba kuwaeleza
kuwa hatufurahishwi na
kinachoendelea bungeni.
Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es
Salaam, Suleman Kova, alisema
wamejipanga kudhibiti fujo
zitakazotokea. Jijini Mwanza,
Mwenyekiti wa Chadema wa mkoa wa
mwanza, Adrian Tizeba, jana alitiwa
mbaroni na Polisi, baada ya kufanya
mkutano wa waandishi wa habari
kuzungumzia maandamano.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa huo,
Valentino Kilowoko, alithibitisha
kukamatwa kwa Tizeba na kusema
walikuwa wanaendelea kumhoji.
Kabla ya kukamatwa, Tizeba alilitaka
Jeshi la Polisi mkoani humo
kushirikiana nao katika maandamano
ya amani yatakayofanyika leo kupinga
Bunge la Katiba linaloendelea mjini
Dodoma.
Alisema licha ya polisi wilaya zote za
mkoa wa Mwanza kukataa barua za
taarifa za kuwapo maandamano hayo,
lakini wamekusudia kuandamana na
kuwaomba polisi nao washiriki.
“Haya ni maandamano ya amani,
tunaomba hata polisi washiriki nasi
kesho (leo) ili kufikisha ujumbe wa
matumizi mabaya ya pesa za umma
katika bunge hilo linaloendelea
Dodoma hivi sasa,” alisema Tizeba.
ZITTO KABWE KUWAPATANISHA DIAMOND NA ALI KIBA
Mbunge wa Kigoma Kaskazini
(Chadema), Zitto Kabwe, amejitosa
kusuluhisha ugomvi wa muda mrefu
wa wasanii wawili wa muziki wa
kizazi kipya nchini, Ali Kiba na
Nasibu Abdul 'Diamond'.
Zitto alitoa kauli hiyo juzi wakati
akihojiwa katika Kipindi cha Mkasi
kinachorushwa na Kituo cha
Televisheni cha EATV baada ya
kuulizwa kuwa ni jitihada gani
amezifanya kusuluhisha ugomvi wa
wasanii hao akiwa kama mlezi wa
wasanii wanaotoka mkoani Kigoma.
Alisema anafahamu kuwapo kwa
ugomvi wa kutoelewana kati ya
wasanii Ali Kiba na Diamond na
kwamba alishawahi kufanya jitihada
za kuwaita kila mmoja kwa nyakati
tofauti.
Alifafanua kuwa katika kuhakikisha
anawasuluhisha wasanii hao,
anaifanya kazi hiyo kwa umakini kwa
sababu hataki kuonekana anaingilia
maisha ya watu na kwamba ana imani
atafanikiwa kuwapatanisha.
Kuhusu madai kwamba ana uhusiano
wa kimapenzi na msanii Mwasiti
Almas, alisema ni kweli kumekuwapo
na uvumi huo lakini kimsingi hana
uhusiano wowote wa kimapenzi na
msanii huyo.
"Nasikitishwa na madai hayo
yanayotolewa na baadhi ya watu,
Mwasiti ni kama dada yangu ambaye
nimekuwa nikimsaidia katika kazi
zake, kuhusishwa naye kimapenzi ni
jambo linalonisononesha,"alisema.
Zitto alisema wanaomhusisha katika
suala la mapenzi na msanii huyo ni
kwa sababu Mwasiti ameimba wimbo
ambao amemtaja yeye (Zitto) lakini
kiukweli hana uhusiani naye wa
kimapenzi.
Alipoulizwa ni lini ataoa, alisema
bado 'yupo yupo' na kwamba kuna
mwanamke aliyemtaja kwa jina la
Jack ambaye amezaa naye mtoto
ambaye kwa sasa miaka nane na
anasoma darasa la pili nchini Uganda.
KAMPUNI YA LEKA DUTIGITE
Kuhusu Leka Dutigite inayounganisha
wasanii wa Kigoma All Stars, alisema
ni kampuni ambayo kila msanii
anayetoka mkoani Kigoma ana hisa
na ikipata faida wanagawana.
Zitto alisema Leka Dutigite pia
inamiliki kampuni nyingine ambayo
imekuwa ikipata kazi mfano katika
Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa) na
yeye kama mlezi amekuwa akitoa
fedha zake kusaidia.
WAREMBO WA MISS TANZANIA WATALII MTO WA MBU
Warembo wanaotarajia kushiriki
shindano la urembo la taifa mwaka
huu "Redd's Miss Tanzania 2014" leo
wanatarajia kutembelea eneo la Mto
wa Mbu kushuhudia maajabu yaliyoko
kwenye mto huo ulioko Karatu
mkoani Arusha ikiwa ni sehemu ya
kufanya utalii wa ndani
Akizungumza na gazeti hili jana kwa
njia ya simu, Ofisa Habari wa Kamati
ya Miss Tanzania, Haidan Rico,
alisema kuwa wakiwa eneo hilo,
warembo walipewa maelezo muhimu
kuhusiana na mto huo na dhumuni la
kuwatembeza warembo hao katika
vivutio mbalimbali ni kutaka
kushawishi jamii kufanya utalii
Rico alisema kuwa wanaamini
warembo hao watafikisha ujumbe
katika familia zao na kubadili mawazo
kwamba utalii ni kwa ajili ya wageni
pekee.
Alisema kuwa kesho Jumanne
warembo hao wataelekea Ngorongoro
Crater kuona jinsi eneo hilo
lilivyobonyea kufuatia mlipuko wa
volkano.
Alisema kuwa tayari warembo hao
wameshatembelea katika lango la
kupanda mlima Kilimanjaro na
kuelezwa mazingira yanayozunguka
eneo hilo, Tarangire na kufanya kazi
za kijamii kwenye hospitali za Kilema
na Marangu ambapo walitoa misaada
ya sabuni, vyandarua, dawa ya meno,
miswaki na mafuta ya kujipaka kwa
watoto na wanawake waliolazwa
kwenye hospitali hizo.
Pia washiriki hao walitembelea
Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa
Kilimanjaro (KIA) na wakiwa hapo
walijifunza mbinu ambazo askari
wanatumia kukagua abiria ambao
wanasafiri na bidhaa zisizoruhusiwa
kama vile dawa za kulevya.
Pia alisema washiriki watamtembelea
Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mjini na
baadaye Hifadhi ya Mbuga ya Arusha.
Warembo hao 30 kutoka mikoa
mbalimbali nchini ambao wako katika
ziara hiyo ni pamoja na Dorice Mollel,
Sofia Masey, Lilian Timothy, Junes
Ndalima, Maureen Godfrey, Martha
John, Naba Magambo, Raisa Julius,
Happiness Samuel, Evelyn Baasa,
Lilian Kamazima, Elizabeth Tarimo,
Nidah Katunzi, Lucy Diu, Mariam
Hussein, Maria Shilla, Camilla John,
Queen Latifa Hashim na Dorren Beno.
Warembo wengine ni Sitti Mtemvu,
Salama Saleh, Patricia Pontain,
Rachel Clavery, Mary Emmanuel,
Nicole Sarakikya, Dorren Robert,
Jihan Dimachk, Nasreen Abdul,
Sabina Thomas na Happinness
Sosthenes.
Happiness Watimanywa kutoka
mkoani Dodoma ndiye mrembo
anayeshikilia taji hilo la taifa na
baadaye mwaka huu ataiwakilisha
nchi kwenye fainali za urembo za
dunia.
TANZANIA YASHUKA VIWANGO FIFA
Tanzania imeporomoka tena kwenye
viwango vya soka vinavyotolewa kila
mwezi na Shirikisho la Soka la
Kimataifa (Fifa), baada ya kuanguka
kwa nafasi tano katika viwango
vilivyotolewa jana.
Tanzania, ambayo ilifungwa 2-0 na
Burundi katika mechi ya kimataifa ya
kirafiki iliyopita, sasa inakamata
nafasi ya 115 duniani na 33 barani
Afrika ikiwa nyuma ya Uganda
wanaoongoza Afrika Mashariki
wakiwa nafasi ya 79 duniani na 19
Afrika, Rwanda walioko nafasi ya 93
duniani na 25 Afrika na Kenya
walioporomoka kwa nafasi saba
wakiwa nafasi ya 30 Afrika na 111
duniani.
Aligeria waliopanda kwa nafasi nne,
wanaongoza barani Afrika wakiwa
nafasi ya 20 duniani wakifuatwa na
Ivory Coast walioshuka kwa nafasi
tatu baada ya kukubali kichapo cha
mabao 4-1 kutoka kwa Cameroon
waliopanda kwa nafasi 12 na
kukamata nafasi ya nane Afrika na 42
duniani.
Nafasi ya tatu barani Afrika inakaliwa
na Tunisia (31) wakipanda kwa nafasi
11 wakifuatwa na Ghana (33), Senegal
(36), Nigeria (37) na Cape Verde (41).
Guinea waliopanda kwa nafasi 16
wanakamata nafasi ya tisa barani
Afrika na 48 duniani huku Burkina
Faso waliopanda kwa nafasi 10
wakifunga pazia la 10 bora barani
Afrika wakifungana na Guinea katika
nafasi ya 48 duniani.
Uganda pia ni wa kwanza katika
Ukanda wa Cecafa wa Afrika Mashariki
na Kati wakifuatwa na Rwanda,
Kenya, Tanzania, Burundi, Ethiopia
(39, 132), Sudan (40, 133), Shelisheli
(47, 172), Sudan Kusini (50, 185),
Eritrea (52, 202), Somalia (53, 204)
huku Djibouti wakifunga mlango
Cecafa na Afrika wakiwa 54 Afrika na
205 duniani.
Mabingwa wa dunia, Ujerumani
wanaongoza 10 bora ulimwenguni
wakifuatwa na Argentina, Colombia
waliopanda kwa nafasi moja
wakiwashusha Uholanzi, Ubelgiji,
Brazil, Uruguay, Hispania, Ufaransa
na Uswis.
Wednesday, September 24, 2014
OKWI ADAI KUA YANGA WATATULIA TU
Licha ya kupika mabao yote ya Simba
katika mechi yao ya kwanza ya Ligi
Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL)
msimu huu waliyotoka 2-2 dhidi ya
Coastal Union kwenye Uwanja wa
Taifa, Dar es Salaam juzi,
mshambuliaji Emmanuel Okwi
amesema hakuwa katika kiwango
chake.
Okwi, aliyejiunga na Simba dakika za
mwisho kabla ya kufungwa kwa
dirisha la usajili msimu huu akitoka
Yanga, alisababisha mabao yote ya
Simba juzi licha ya mashabiki wa
Yanga kumzomea mwanzo mwisho
jambo analoamini muda si mrefu
watatulia baada ya kurejea katika
makali yake.
Bao la kwanza la Simba lilipatikana
baada ya Okwi kukwatuliwa nje ya
mstari wa eneo la hatari la Coastal
Union, hivyo adhabu hiyo kuzaa
matunda kupitia kwa mpigaji Shabani
Kisiga kabla ya Mganda huyo tena
kutoa pasi ya mwisho ya bao la pili
kwa mfungaji bora wa VPL msimu
uliopita, Mrundi Amissi Tambwe.
Kisiga alifunga kwa 'frikiki'
iliyomshinda kipa wa Coastal, Shaban
Kado wakati mabao ya mabingwa hao
wa Tanzania Bara 1988 yalifungwa na
mtokea benchi Lutimba Yayo na
mshmbauliaji wa zamani wa Gor
Mahia ya Ligi Kuu ya Kenya, Rama
Salim.
Mara tu baada ya mechi hiyo
iliyochezeshwa na refa Jacob Adongo
kutoka Mara kumalizika, Okwi
aliliambia NIPASHE kuwa bado
hajafikia katika kiwango chake cha
kusakata soka.
“Mara nyingi sipendi kuzungumzia
kiwango changu binafsi kuliko cha
timu, tulicheza vizuri kipindi cha
kwanza na Coastal walicheza vizuri
kipindi cha pili,” alisema Okwi.
“Sijafurahishwa sana na kiwango
nilichoonyesha leo (juzi), nitajitahidi
kuongeza mazoezi ili mechi ijayo
niisaidie timu yangu kupata ushindi,”
alisema zaidi Mganda huyo ambaye
muda wote wa mechi ya juzi alikuwa
akizomewa na mashabiki wa Yanga
waliokuwa wameingia uwanjani
kutazama mechi hiyo.
Alipoulizwa juu ya zomea zomea
inayofanywa na mashabiki wa Yanga
dhidi yake, Okwi alisema: “Sina muda
nao, mimi nimeshakuwa mchezaji
halali wa Simba, mambo yote
kuhusiana na Yanga hayanihusu.
Ninaamini nitakapokuwa katika
kiwango changu, hawatanizomea
tena,” alisema.
Okwi, mchezaji wa zamani wa SC Villa
ya Ligi Kuu ya Uganda na Etoile du
Sahel ya Tunisia, amejiunga na Simba
baada ya uongozi wa Yanga
kuwasilisha nyaraka katika Shirikisho
la Soka Tanzania (TFF) zikionyesha
kuwa mkataba wake wa miaka miwili
na nusu na klabu hiyo ya Jangwani
aliousaini Desemba 13, mwaka jana,
umevunjwa.
MAGOLI 18 LIGI KUU YASHINDWA KUVUJA REKODI
Magoli 18 yamefungwa kwenye mechi
saba za ufunguzi wa Ligi Kuu
Tanzania Bara iliyoanza Jumamosi
iliyopita, lakini yameshindwa kuvunja
rekodi ya magoli ya msimu uliopita.
Kwenye mechi za ufunguzi wa Ligi
Kuu msimu uliopita jumla ya magoli
19 yalipatikana.
Ligi ya msimu huu imeanza kwa Azam
FC kuitandika Polisi ya Morogoro
mabao 3-1, Mtibwa Sugar kuichapa
Yanga mabao 2-0, Stand United ya
kutandikwa nyumbani mabao 4-1
dhidi ya Ndanda FC kutoka Mtwara,
wakati Mgambo JKT ya Tanga
iliifunga Kagera Sugar bao 1-0.
Mechi nyingine ilikuwa ni Ruvu
Shooting kupata kipigo nyumbani cha
mabao 2-0 kutoka kwa Prisons ya
Mbeya, Mbeya City kulazimishwa sare
ya bila kufungana dhidi ya JKT Ruvu,
huku Simba ikibanwa mbavu katika
sare ya 2-2 dhidi ya Coastal Union,
hivyo kuzaa mabao 18.
Magoli 19 ya mechi ya ufunguzi
msimu uliopita kwa mujibu wa
kumbukumbu zetu yalipatikana kwa
Yanga kuinyuka Ashanti mabao 5-1,
Mtibwa kutoka sare ya bao 1-1 dhidi
ya Azam, JKT Oljoro ikainyuka
Coastal Union mabao 2-0, Mgambo
ikachapwa 2-0 dhidi ya JKT Ruvu,
Simba ikatoka sare ya mabao 2-2
dhidi ya Rhino ya Tabora, Mbeya City
ikatoka sare ya bila kufungana dhidi
ya Kagera Sugar na Ruvu Shooting
ikaitandaika Prisons mabao 3-0.
Katika hatua nyingine, mchezaji wa
Mgambo Shooting Ramadhani Pera
ameweka rekodi ya kuwa mchezaji wa
kwanza kufunga bao kwenye Ligi kuu
alipofunga bao pekee dhidi ya Kagera
Sugar katika dakika ya 12 kwenye
raundi ya kwanza ya ligi hiyo
Jumamosi.
Mabao yote yaliyopatikana kwenye
mechi nyingine yalifungwa baada ya
dakika hizo.
Shaaban Kisiga wa Simba anashikilia
rekodi ya kufunga bao la mapema
zaidi katika dakika ya saba dhidi ya
Coastal katika mechi ya kufunga
raundi ya kwanza Jumapili.
TIKETI ZA KIELEKTRONIKI ZAANZA KUJIBU
Mfumo wa tiketi za elektroniki katika
mechi za soka nchini umeanza kuzaa
matunda baada ya jana Shirikisho la
Soka Tanzania (TFF), kuweka wazi
kwamba mapato ya milangoni
yameongezeka.
Akizungumza na waandishi wa habari
jijini Dar es Salaam jana mchana,
Mkurugenzi wa Mashindano wa
shirikisho hilo, Boniface Wambura,
alisema utumiaji wa tiketi za
elektroniki umefanikiwa kudhibiti
hujuma za mapato ya milangoni
kwenye viwanja ambavyo tayari
vimeshasimikwa mfumo huo.
Wambura alisema kwa sasa wanapata
mapato halisi ya mechi husika
kulingana na idadi ya watu waliokata
tiketi.
“Hatutarudi nyuma katika hili,
tutaendelea kutumia tiketi za
elektroniki kwenye viwanja vyote
vilivyosimikwa mfumo huu,” alisema
Wambura na kuongeza: “Kuna viwanja
kama CCM Kirumba jijini Mwanza na
Sheikh Amri Abeid jijini Arusha vina
mfumo huu lakini havitumiwi na timu
za Ligi Kuu.
Tutahakikisha mechi za Ligi Daraja la
Kwanza zinazochezwa kwenye
viwanja hivyo vinatumia tiketi za
elektroniki ili watu waishio katika
majiji hayo pia wauzoee.”
Mkurugenzi huyo alisema watu wote
wanaojaribu kuingia viwanjani kwa
kutumia tiketi feki wamekuwa
wakinaswa kwa kutumia mashine za
utambuzi wa tiketi za elektroniki
(PDA), hivyo kwa sasa hakuna mtu
anayeingia kwenye viwanja vilivyo na
mfumo huo akitumia tiketi bandia.
Akitangaza mapato ya mechi za wiki
iliyopita za Ligi Kuu ya Vodacom
Tanzania Bara (VPL), Wambura
alisema yameongezeka kwa kiasi
kikubwa, sababu kubwa akisema ni
matumizi ya mfumo wa tiketi za
kisasa za kielektroniki.
Wambura alisema mechi ya Mtibwa
Sugar dhidi ya Yanga iliyochezwa
kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini
Morogoro Jumamosi na kumalizika
kwa wenyeji kuibuka na ushindi wa
mabao 2-0, imeingiza Sh. milioni 59
kutokana na viingilio vya mashabiki
11,499 waliokata tiketi za Sh. 5,000.
Mapato hayo ni ongezeko la Sh.
milioni 12 ikilinganishwa na mapato
ya mechi kati ya timu hizo kwenye
uwanja huo msimu uliopita.
Aidha, Wambura alisema kuwa mechi
ya Simba dhidi ya Coastal Union
iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa
jijini Dar es Salaam Jumapili huku
timu hizo zikitoka sare ya mabao
mawili, imeingiza Sh. milioni 124.7
zilizotokana na viingilio vya
mashabiki 22,114 waliokata tiketi
kuingia kwenye uwanja huo wenye
uwezo wa kuketisha watazamaji
57,558.
Simba na Coastal Union ziliingiza Sh.
milioni 36.8 zilipokutana katika mechi
ya ligi hiyo kwenye uwanja huo
msimu uliopita.
Utumiaji wa tiketi hizo za kielektroniki
ni utekelezaji wa mapendekezo
yaliyomo kwenye ripoti ya Kamati
Maalum ya Kudhibiti na Kuboresha
Mapato ya TFF iliyotolewa 2011 na
agizo la serikali lililotolewa katikati
ya mwaka huu.
Mei 2011 Kamati Maalum ya Kudhibiti
na Kuboresha Mapato ya TFF
iliyoongozwa na Rais Mstaafu wa
shirikisho hilo, Leodegar Tenga, ilitoa
ripoti yenye kurasa 95 ikionesha
uhujumu mkubwa wa mapato
utokanao na matumizi ya tiketi za
kawaida, hivyo kamati ikapendekeza
TFF ianze kutumika tiketi za kisasa za
kielektroniki.
Aidha, Juni mwaka huu, serikali
iliiagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania
(TRA) kuiiamuru TFF kutumia mfumo
wa tiketi za kielektroniki kwenye
viwanja mbalimbali vya soka nchini ili
kudhibiti uhujumu wa mapato ya
milangoni.
Akiwasilisha taarifa ya Kamati ya
Bunge ya Uchumi, Viwanda na
Biashara kuhusu utelezaji wa
majukumu ya Wizara ya Fedha na
Uchumi kwa mwaka wa fedha 2014/15
Bungeni mjini Dodoma Juni 4, mwaka
huu, mwenyekiti wa kamati hiyo,
Luhaga Mpina aliitaka TRA kutoa
sharti kwa TFF kutumia mfumo wa
tiketi za elektroniki ili kuongeza
mapato ya nchi.
"Kamati inashauri TRA iweke sharti la
lazima la kuitaka TFF kutumia mfumo
wa tiketi za kielektroniki katika kuuza
tiketi zake ikiwa ni jitihada za
kuongeza mapato ya serikali," alisema
Mpina.
Mbunge huyo wa Kisesa (CCM),
alisema kwa muda mrefu serikali
imekuwa haipati mapato ya kutosha
kutoka katika sekta ya michezo
hususan mpira wa miguu ulio chini ya
TFF kutokana na mfumo dhaifu wa
ukusanyaji fedha kipindi cha kuuza
tiketi.
KIONGERA KUIKOSA YANGA
Mshambuliaji Paul Kiongera wa
Simba huenda akaikosa mechi ya
kwanza dhidi ya watani wao wa jadi,
Yanga msimu huu wa Ligi Kuu ya
Vodacom Tanzania Bara itakayopigwa
kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es
Salaam Oktoba 12 baada ya kuumia
goti katika mechi iliyopita.
Kiongera alitokea benchi dakika ya 67
akichukua nafasi ya mfungaji bora wa
msimu uliopita, Mrundi Amissi
Tambwe, lakini dakika mbili kabla ya
mechi hiyo waliyotoka 2-2 dhidi ya
Coastal Union kumalizika, Mkenya
huyo alilazimika kumpisha Amri
Kiemba baada ya kugongana na kipa
Shaaban Kado wa Coastal na kuumia.
Taarifa zilizolifikia NIPASHE jana
kutoka ndani ya uongozi wa Simba
zilieleza kuwa Kiongera ameumia goti
na jana alipelekwa Hospitali ya Taifa
Muhimbili kufanyiwa vipimo.
Mmoja wa viongozi wa Simba (jina
tunalo) alisema mchezaji huyo ana
maumivu sugu ya goti hilo baada ya
kuumia awali akiwa kwao, Kenya.
Kiongozi huyo alisema Kiongera
anaweza kuwa nje ya uwanja kwa
muda wa kati ya wiki sita hadi miezi
miwili kabla ya kuanza mazoezi
mepesi, hivyo hatacheza mechi ya
Oktoba 12 ya watani wa jadi Simba na
Yanga.
Alibainisha kuwa kumeibuka hali ya
wasiwasi ndani ya Simba kwamba
huenda hawakufanya uamuzi sahihi
kumsajili Mkenya huyo kabla ya
kumfanyia vipimo vya afya.
Majeruhi wengine wa Simba ni beki
wa kushoto Issa Rashid ‘Baba Ubaya’
aliyeumia nyama za paja wiki mbili
zilizopita mazoezini, ambaye
inaelezwa kuwa yuko katika wiki ya
mwisho ya mapumziko na winga
Haruna Chanongo aliyeumia goti pia
Jumapili wakati wakichuana na
Coastal. Imeelezewa kuwa Chanongo
atakuwa nje kwa siku nne tangu
kuumia kwake.
Habari njema zaidi kwa Simba kwa
sasa ni kurejea kwa kiungo
mpambanaji Jonas Mkude, ambaye
Daktari wa Simba, Yassin Gembe
amesema anaweza kuanza kucheza
hata Jumamosi dhidi ya Polisi
Morogoro endapo kocha atampanga.
“Ni uamuzi wa kocha tu, lakini ukweli
ni kwamba Mkude yuko fiti kabisa
kwa sasa na anaweza kuanza
kucheza, uzuri ni kwamba pamoja na
kuwa nje kwa muda mrefu, lakini
hajaongezeka uzito,” alisema Gembe.
Mkude hajawahi kuichezea Simba
chini ya kocha aliyerejea kwa mara ya
tatu nchini kuinoa timu hiyo,
Mzambia Patrick Phiri. Katika mechi
iliyopita kiungo Mrwanda Pierre
Kwizera alicheza nafasi ya Mkude
lakini alionekana wazi kutoimudu.
Baada ya Chanongo kuumia, winga
Uhuru Seleman aliingizwa lakini
baada ya mechi kumalizika huku
Coastal wakirudisha mabao yote,
Phiri aliweka wazi kwamba pengo la
Chanongo halikuzibika ipasavyo.
Kikosi cha Simba kilirejea tena
kambini visiwani Zanzibar kujiandaa
kwa mechi yao inayofuata Jumamosi
dhidi ya Polisi Morogoro.